Video ya mtoto wa Rayvanny na Fahyma akiwa na Diamond Platnumz

Jaydanvanny ambaye ni mtoto wa kwanza wa mkali wa Wasafi records Rayvanny na mpenzi wake Fahyma ni miongoni mwa watoto maarufu Tanzania.

Ingawa bado yeye ni mchanga, mtoto huyu akona mashabiki wengi mitandaoni na hivi karibuni alipata fursa ya kukutana na mjomba wake, Diamond Platnumz huku wengi wakitamani maisha yake.

Kwenye video hiyo, Jaydan anaonekana kutulia huku Platnumz akicheza na yeye. Tazama video hiyo hapa;

https://instagram.com/p/BYTrlHvAnDB/

Mpenzi wa Rayvanny arudisha mwili wake wiki kadhaa baada ya kujifungua mtoto wa Kiume

Fahyma ambaye ni mpenzi na mama ya mtoto wa Rayvanny amekuwa akiwaekea mashabiki wake picha huku akionesha umbo lake ambalo limerudi wiki kadhaa baada ya kujifungua mtoto wake wa kwanza, Jaydan.

Mrembo huyu ambaye amejitambulisha kama teen mom amewapa wengi nafasi ya kufikiria kuwa bado hajafikisha miaka 20 na ikiwa ni ukweli basi inaonekana kuwa ameharakisha maisha yake.

Hata hivyo Rayvanny bado anampenda kulingana na mambo ambayo huyaweka kwenye mtandao wake wa Instagram. Tukiyaacha hayo, picha ambazo Fahyma ameziweka zinamuonesha kama amevalia nguo za kuogelea na kwa kweli amependeza sana.

Zitazame hapa.

Rayvanny aweka picha akiwa na mwanae, huu ndio ujumbe aliomwandikia

Msanii kutoka label ya Wasafi records Rayvanny sasa hivi ni baba ya mtoto mmoja wa kiume, Jayden. Jayden ambaye alizaliwa na Fahyma mwezi wa Aprili mwaka huu amewaletea wazazi wake furaha na Rayvanny hawezi ficha mapenzi aliyonayo kwa mtoto huyu.

Kupitia mtandao wake wa Instagram Rayvanny aliweka picha akiwa na mtoto wake huku akiandika kusema,

Mimi na pacha wangu @jaydanvanny

Japo bado Fahyma na Rayvanny hawaonyesha uso wa Jaydan wengi wana imani kuwa mtoto huyu anafanana na babake kwani rangi yao pia inafanan. Lakini mashabiki wao wanangojea Arobaini ya Jaden kuona kama watamuonyesha mtoto huyu.

Hata hivyo, tazama picha hiyo hapa:

Rayvanny akiwa na mwanae