Video ya mtoto wa Rayvanny na Fahyma akiwa na Diamond Platnumz

Jaydanvanny ambaye ni mtoto wa kwanza wa mkali wa Wasafi records Rayvanny na mpenzi wake Fahyma ni miongoni mwa watoto maarufu Tanzania.

Ingawa bado yeye ni mchanga, mtoto huyu akona mashabiki wengi mitandaoni na hivi karibuni alipata fursa ya kukutana na mjomba wake, Diamond Platnumz huku wengi wakitamani maisha yake.

Kwenye video hiyo, Jaydan anaonekana kutulia huku Platnumz akicheza na yeye. Tazama video hiyo hapa;

https://instagram.com/p/BYTrlHvAnDB/

Nay wa Mitego adai Diamond Platnumz na Alikiba hawamtishi, hii ndio sababu yake

Msanii wa bongo Nay wa Mitego ni mmoja wa wasanii ambao wanafanya vyema kwenye muziki. Hivi sasa anafanya vyema na wimbo wake mpya ‘Makuzi’ ambayo anaamini kuwa itafanya vizuri.

Akizungumza hivi karibuni kwenye show ya Radio One Nay alifunguka kudai kuwa yeye hana hofu kuwa wimbo wake utafanya vizuri licha ya ishu ya Diamond Platnumz na King Kiba inayowafanya wasanii wengi kutoachilia nyimbo zao kwa sababu wanahofia hazitawafikia mashabiki wao.

Nay alisema;

Watu wanaogopa kutoa nyimbo kwa sababu ya vungu vungu hili, kwangu huwa naona ni vitu ambavyo huwa vinapita haraka sana na huwa siviweki katika akili, ndio maana nikiwa na kitu changu ambacho nahisi kwa wakati huo kinatikiwa kwenda bila kuangalia kuna nini kinaendelea huwa natoa.

Aliendelea kwa kusema;

Muziki wangu una nguvu kuliko vitu vingine, mashabiki wangu ambao wanaamini kwenye kile ambacho nakifanya, so kelele za watu au purukushani za huko na kule hazinizui nikiwa na kitu changu nataka kukifanya.

Chidi Benz azungumza kuhusu ishu ya kukamatwa na dawa za kulevya

Mwanamziki Chidi Benz sasa hivi yuko huru baada ya kudaiwa kukamatwa na polisi baada ya kupatikana na madawa ya kulevya hivi karibuni.

Akizungumza na showbiz Etra ya bongo, Chidi Benz alidai kuwa kwa sasa hana ruhusa ya kuzungumzia ishu hiyo huku akisema kuwa vijana wanapaswa kuwacha kwani zikona madhara yake.

Tazama mahojiano yao hapa kwa hisani ya Showbiz.

Showbiz Extra: Sawa, na hili la wewe kukamatwa na dawa za kulevya liko vipi? Ni kiki ya kutoka na video ya wimbo au kuna ukweli upi ambao umejificha ikizingatiwa wewe umewahi kukiri mara kadhaa kuachana na dawa za kulevya?

Chid Benz: Kuhusu hilo nina ushauri kutoka kwa mama watoto wangu kwamba nisilizungumzie zaidi. Lakini kwa ufupi ni kwamba mtu kukamatwa na dawa za kulevya ni sawa na mtu aliyekamatwa na bangi, mirungi ama chochote kile ambacho kinaonekana kuvunja sheria za nchi! Kwa hiyo nisiingie huko sana lakini jambo la msingi ni kwamba vijana wa Kitanzania wasijaribu na wanaotumia dawa za kulevya waachane nazo, siyo nzuri zaidi wajenge taifa kwa manufaa ya kizazi chetu.

Vanessa Mdee aandikiwa ujumbe huu na Juma Jux

Hata baada ya kuachana na Vanessa Mdee, msanii kutoka bongo Juma Jux ameonekana kuwa bado na hisia za kumpenda mremboh huyu.

Hivi karibuni kupitia mtandao wake wa kijamii, Jux aliandika ujumbe ambao umewaacha mashabiki wakifikiria kuwa ujumbe huo ulikuwa wa Vanessa Mdee.

Aliandika kusema;

Nakumbuka mara ya mwisho kufanya party ya Birthday yangu ilikuwa 2013, Miaka minne iliyopita. Sikuwahi kufanya party yoyote tena sababu nilikuwa na rafiki, mpenzi na mtu wa karibu kuliko mtu yoyote kwenye maisha yangu. Miaka yote iliyofata nilikuwa na yeye mpaka sasa atuko tena karibu kama mwanzo, Tumebaki kuwa marafiki wa kawaida tu. Uwepo wake tu ulikuwa ni zaidi ya chochote kwenye siku yangu ya kuzaliwa, Kuongea na yeye au txt yake tu ilitosha kukamilisha siku yangu. Ila sasa sidhani kama itakuwa kama mwanzo. Nitafarijika sana kama nitamuona hiyo siku. This time nataka kuparty na watu wangu nani anataka kuparty na mimi katika siku ya birthday yangu ?

Zari adaiwa kupungua mwili Kisa na sababu, Hamisa Mobetto

Mrembo na mama watoto wa Diamond Platnumz, Zari Hassan anasemekana kuwa na mawazo mengi ambayo yamemfanya kupungua kimwili sababu ya kufikiria sana.

Habari hizi ziliwekwa wazi na chanzo kimoja kilichozungumza na Global Publisherz kueleza hali ya Zari inavyoendelea tangu Hamisa Mobetto kuweka wazi kuwa Abdul Naseeb ni mtoto wa Diamond Platnumz. Chanzo hicho kilisema;

“Zari kapungua mwili kweli jamani. Mobeto amemponza. Amemsababishia watu wamtukane sana Zari kiasi ambacho amekosa amani kabisa. Masikini mtoto wa watu kakonda kweli sasa hivi.Ukitazama picha za Zari sasa hivi si Zari yule aliyetoka kujifungua. Tena kwa kawaida tunajua mtu ukitoka kujifungua unanenepa lakini kwa Zari mambo yamekuwa tofauti. Ngoja niwatumie picha yake ya sasa muone,”

 

Hata hivyo maneno haya yanauwezekano ya kuwa ya kweli kwani kwenye picha za Sasa, Zari anaonekana kupugua mwili sana.

 

 

Zari
Zari

Juma Jux afunguka kuhusu suala la kujiunga na Wasafi Records

Jux  ambaye ni msanii mkubwa bongo anaonekana kufanya vyema na wimbo wake mpya utaniua.

Hatah ivyo akizungumza na Planet Bongo ya EA Radio msanii huyo alisema kuwa Wasafi record ni label nzuri lakini hajawahi kufikirikia kujiunga na label hiyo.

Ni kitu kizuri sio kibaya kwa sababu ile ni record label, hiyo nafasi ikipatika sio mbaya lakini kwa mimi sikuwahi kufikiria kwa hapa Tanzania au kwa Africa kwa kweli.

Hata hivyo yeye binafsi hana shida yoyote ya kujiunga na label hiyo iwapo watazingatia mkataba wake kwa sababu hafanyi muziki peke yake.

Iwe ni kampuni au sehemu ambayo itanichukua mimi kama kunimeneji pale nilipokuwa wafanye vitu extra zaidi. Sawa wanaweza ikawa wanaweza kwa mkataba kama watakuja na mkataba ambao nitautaka na vitu vyangu ambavyo navihitaji naweza nikasaini kwa sababu mimi ni mfanyabiashara lakini kwa sasa hivi hatukuwahi kuongea au kufikiria.

Aunt Ezekiel hana mipango ya kuolewa na Mose Iyobo, hii ndio Sababu yake

Muigizaji wa muvi za Kibongo Aunt Ezekiel ambaye sasa anatoka kimapenzi na Mose Iyobo hivi karibuni alifunguka kueleza mambo kadhaa kuhusu mapenzi yao huku akiwaacha wengi na maswali mingi.

Aunt Ezekiel alisema kuwa kuna wakati Mose Iyobo amemfumia na kupata meseji kutoka watu wanaomtaka na pia yeye amewahi kuzipata meseji hizo lakini anaelewa kuwa vitu kama hizo hufanyika.

Nilishawahi kumfumania mara mingi nyingi na yeye alishawahi kubamba meseji kwenye simu yangu lakini inaonesha labda mtu alikuwa ananipenda na mimi nikampotezea na ishu kama hiyo ya kufumania ni lazima itokee hasa kwa sisi tuna majina

Kuhusu swala la kuolewa, Aunt aliambia Risasi hana mipango ya kuolewa na Iyobo huku alisema:

Unajua ishu ya ndoa ni mwanaume ndiyo anaamua kuoa mtu f’lani lakini pia kufunga ndoa ni makaratasi tu kikubwa zaidi ni jinsi gani unaishi na mwenzako na mnaelewana kiasi gani.

 

Mwana FA afunguka kuhusu kumhonga mwanamke iliampende

Rapa mkali kutoka Tanzania Mwana FA ni mmoja wa wasanii wanaofanya vizuri katika muziki. Ameweza kuachia nyimbo ambazo zimevuma Afrika Mashariki.

Kwa mara ya kwanza msanii huyo alifunguka kuhusu ishu ya wanaume kuwahonga wanawaka ili wawapende. Kulingana na yeye, hajawai kumhonga mwanamke yeyote katika maisha yake.

 

Akiongea na Risasi Vibes, Mwana FA alisema;

“Nihonge ili nipate nini, sijawahi kuhonga hata siku moja najua wengi wanaweza wasiamini lakini ndiyo hivyo, tabia hizo naishia kuziona kwa washkaji zangu huku mtaani lakini kwangu hazijawahi kuwepo maana kitendo hicho nakichukulia kama biashara ya kikahaba ambayo binafsi naichukia” alisema Mwana FA

Shamsa Ford afunguka kwa nini anatamani kuokoka lakini anashindwa

Muigizaji wa filamu za Bongo Shamsa Ford kwa Sasa anatamani sana kuzifuata nyayo za Mzee Yusuf kwa kuokoka na kuacha mambo ya dunia.

Mrembo huyu anadai kuwa siku za mwisho zimekaribia na ndio maana anaonelea kubadilisha mienendo Yale. Akizungumza na Risasi Jumamosi, Shamsa alisema kuwa,

Shamsa Ford

Nimejaribu kusali sala tano kila siku. Kuna wakati ninasahau lakini kuna siku ninasali zote, ninaamini taratibu nitakuwa kama Mzee Yusuf, ninamuomba sana Mungu.

Baada ya Seduce me ya Alikiba kufikisha 2M YouTube, Christina Shusho amuandikia King Kiba ujumbe huu

King Kiba anaonekana kuwa yeye ndiye Mfalme Wa Nyimbo za bongo na hii ni baada ya msanii huyo kuachia wimbo wake mpya Seduce me ambao umefikisha milioni 2 siku tatu baada ya kuiwachia.

Mashabiki wake pia wameonekana kupenda wimbo huu ikiwemo Wema Sepetu na wengine Kama muimbaji wa nyimbo za injili, Christina Shusho. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Christina alionyesha mapemzi yake kwa wimbo huu wa King Kiba kwa kuandika;

“Leo unaweza kukuta mtu kaitwa kanisani aongoze wimbo wa sifa halafu akalianzisha Seduce Me, Eeh jamani Kiba we noma, wimbo ni mzuri sana kitaaluma kama anavyopenda kusema bosi Ruge. Hauna picha za aibu , naweza kuuangalia nikiwa na familia, labda sijui maana ya Seduce Me. Timu Kigoma Wamanyema oyeeeee. Cha mwisho Ali Kiba basi siku nyingine tutembelee kanisani ukiwa mfalme huchagui dini wote wako”

Hata hivyo kwa sasa ameweka rekodi mpya ya kuwa msanii wa kwanza Afrika Mashariki kufikisha 2 Million view YouTube na siku tatu.

Harmorapa akana kumdiss Majani kwenye wimbo wake mpya

Rappa kutoka bongo, Harmorapa ameachia nyimbo mpya itwaayo Ajitokeze hivi karibuni lakini wimbo huo umezua ngumzo mitandaoni kwani Harmorapa anasemekana kuwa alimdiss aliyekuwa meneja wake wa zamani, P Funk Majani. Kwenye wimbo huo anaskikaa kisema;

“Nishakuwa mfagizi chini ya miti, nazijua kero za majani, maana majani hayafadhiliki, ndiyo maana sipatani na majani”

Hata hivyo Harmorapa amefunguka kuhusu ishu hii na kukana kuwa wimbo huo unamlenga Majani. Harmorapa alikiri kuwa Sasa hivi Majani sio meneja wake lakini hii sio sababu ya kumdiss kwenye wimbo Kama wengi wanavyodai.

“Ni kweli kwa sasa P Funk Majani siyo meneja wangu, ila siyo kweli kwamba nimemdiss kwenye ngoma yangu, kwa sababu hatuko pamoja kikazi ila bado tuna mahusiano mazuri na hatuna ugomvi, wala hajawahi kunitimua hizo ni fununu tu. Ngoma yangu ya Ajitokeze ni ngoma inayonizungumzia mimi, kwamba hakuna anayeweza kutokea akawa kama mimi na kama yupo basi ajitokeze, ila siyo dongo kwa Majani,”

King Kiba atisha baada ya kuweka rekodi mpya YouTube

Alikiba ama ukipenda King Kiba ameweka rekodi mpya Afrika Mashariki kama msanii ambaye video yake imepata kutazamwa na watu milioni masaa 38 baada ya kuiwachia.

Seduce me imeweka rekodi ya kipekee ambayo hata wakalik ama Diamond Platnumz na Vanessa Mdee bado hawajaweza kufikisha. Kupitia ukurasa wake wa instagram, King Kiba aliweka post akiwashukuru mashabiki wake kwa kufanikisha kuvunja rekodi hiyo. Aliandika;

“Ahsanteni sana kwa upendo, nisingebarikiwa zaidi na kupendelewa bila nyinyi, nyinyi ni wa maana sana kwangu na nafanya haya kwa ajili yenu”,

kampuni ya Rockstar ambayo inamsimamia Kiba pia iliandika ujumbe kusema kuwa wimbo huu umevunja rekodi ya kipekee na ni video zinazotrend Tanzania na Kenya.

“Historia ya kunjwa rekodi imewekwa, Mfalme Kiba na wimbo wake mpya wa ‘Seduce me‘ umekuwa wa kwanza na kipee kwa msanii wa Afrika Mashariki kufikia kutazamwa mara milioni 1 kwenye Vevo/YouTube ndani ya masaa 38 tu, ina ‘trend’namba 1 Tanzania na namba 1 Kenya kwa ‘weekend’ nzima, rekodi imevunjwa.”

Aunt Ezekiel afunguka kuhusu mapenzi yake na Mose Iyobo

Muigizaji wa filamu za bongo Aunt Ezekiel hivi karibuni alifunguka kueleza mambo kadhaa kuhusu mapenzi yake na Mose Iyobo na sababu hawezi achana na yeye.

Akizungumza na Over ze Weekend ya Tanzania, mama cookie alidai kuwa yeye na Mose wanasikizana sana kwa mazungumzo na pia ndoto zao za kimaisha zinaambatana.

Mose Iyobo na Aunty Ezekiel

Tazama mahojiano yao hisani ya Over se weekend;

Over Ze Weekend: Mara nyingi mastaa huwa hawadumu na wapenzi lakini wewe na Iyobo mpaka sasa mna takribani miaka mitatu na miezi unaweza kutuambia siri ni nini?

Aunt: Kikubwa ni kuzungumza na moyo wako ulipotua ni mahali sahihi na je, unapata faraja unapokuwa hapo? Mi na Iyobo tunasikiliza sana.

Over Ze Weekend: Ni kitu gani kabisa ulikipenda kwa Iyobo?
Aunt: Unajua napenda sana mwanaume asiyekuwa na kero, asiyependa kuzungumza sana yaani kiufupi sipendi gubu, sasa kwa Iyobo vitu vyote hivyo hana.

Over Ze Weekend: Zamani ulikuwa gumzo kwa kubadilisha wanaume, mara Hatman, Silver, Joff na Jack Pemba nini kimekufanya ukaamua kutulia?

Aunt: Teknolojia sasa imekua, nimetulia na nina mtoto huyu Cookie (anamshika begani), anaweza kufungua kwenye mitandao na kumkuta mama yake ana skendo mbaya itakuwa siyo poa kabisa hivyo kila kitu kina wakati wake.

Over Ze Weekend: Unahisi kwa Iyobo umefika?

Aunt: Ndiyo, kwanza kabisa nasema hivyo kwa sababu kubwa amekuwa ni baba bora kwa mtoto wetu, mara nyingi nasikia malalamiko kwa baadhi
ya marafiki zangu kwa waume zao kutowajali watoto lakini mimi naweza kumuacha mtoto wangu na baba yake na nisiwe na wasiwasi hata kidogo.

Over Ze Weekend: Ikitokea aliyekuwa mumeo, Sunday akatokea na kuja kukuchukua kama mke wake wa zamani utafanyaje?

Aunt: Kisheria ya dini na hata kibinadamu nisingeweza kukaa muda huo ambao anatumikia kifungo na hata yeye mwenyewe alishawahi kuniambia hawezi kunilaumu kwa maamuzi yoyote ambayo ningechukua, kwa sababu hata alivyopata matatizo nilikuwa nikijaribu kuyashughulikia karibia mwaka mzima ndipo nikaendelea na mambo mengine.

Over Ze Weekend: Ulishawahi kupigwa hata kofi na Iyobo?

Aunt : Siyo kofi tu tunapigana kabisa lakini baadaye kama akigundua kama alinipiga kwa hasira basi anajirudi tunaombana msamaha na maisha yanaendelea.

Over Ze Weekend: Mara nyingi Iyobo, kazi zake ni za kusafiri na anakutana na watu mbalimbali hilo halileti shida kwenye uhusiano wenu?

Aunt: Yaah inasumbua sana mpaka kuna wakati unahisi unataka kushindwa lakini ukija hata kuangalia meseji anazotumiwa kupitia mitandaoni unagundua wazi kuwa wanampenda tu kwa sababu ni mtu f’lan.

Over Ze Weekend: Ulishawahi kumfumania Iyobo au yeye kukufumania?

Aunt: Nilishawahi kumfumania mara nyingi, na yeye alishawahi kubamba meseji kwenye simu yangu lakini inaonesha labda mtu alikuwa ananipenda na mimi nikampotezea na ishu kama hiyo ya kufumania ni lazima itokee hasa kwa sisi ambao tuna majina. Risasi: Kuna mipango ya kuolewa na Iyobo?

Aunt: Hapana.

Over Ze Weekend: Kwa nini wakati inaonekana mnapendana sana?

Aunt: Unajua ishu ya ndoa ni mwanaume ndiyo anaamua kuoa mtu f’lan lakini pia kufunga ndoa ni makaratasi tu kikubwa zaidi ni jinsi gani unaishi na mwenzako na mnaelewana kiasi gani.

Over Ze Weekend: Kwa kipindi ambacho upo na Iyobo hakuna ushawishi uliwahi kupata kutoka kwa mapedeshee mbalimbali?

Aunt: Hata kama wapo sasa hivi siwezi kurubunika kwa sababu hakuna gari ambalo sijaendesha, viwanja ambavyo sijaenda na hela gani ambayo sijashika hivyo mwisho wa siku unaona yote ni mapito tu.

Over Ze Weekend: Mna mpango wa kuongeza mtoto mwingine?

AUNT: Ndiyo, mmoja lakini siyo kwa sasa hivi.

“Hakuna mtu anayeninunulia nguo wala kunipa pesa” Agnes Masogange ataja sababu asizoogopa kuuza mwili wake

Aliyekuwa video vixen mkali kutoka Bongo Agnes Masogange amefunguka kuhusu maisha yake huku akigusia kuwa watanzania wengi wanapenda kumponda bure.

Katika mahojiano yake na Gazeti la Mwanaspoti mrembo huyu alisema Kuwa hana dhiki ikiwa atafikia kiwango cha kuuza mwili wake ili ajitafutie. Masogange alisema,

Agnes Masogange
Agnes Masogange

“Watu bana!, mimi sina dhiki ya kufikia kuuza mwili wangu eti nipate pesa na kuhusu zile picha kipindi kile nilizopiga hazikuwa za utupu sema basi tu watanzania tunapenda kuzusha sana. Na mtu kuenda Sauzi ndio ameenda kujiuza?,” Masogange aliliambia Gazeti la Mwanaspoti.

Aliongeza kuwa hakuna mtu anayemnunulia mavazi anayovaa wala kumpa pesa ya matumizi yake kwa hivyo hakuna anayeweza kumwambia chochote.

“Mimi nilikuwa na biashara zangu nafanya na wanaosema hivyo hawanisaidii chochote,hakuna mtanzania anayeninunulia nguo,hayupo anayenipa pesa waongee tu. Unajua sisi wadada tuna tabia ya kuoneana wivu akiona unafanya vizuri anaanza kukusemea vitu vya ajabu pembeni,”

Hamisa Mobetto aendelea kudai kuwa maisha yake na ya Abdul Naseeb yako mashakani

Hamisa Mobetto anaendelea kuhofia kuwa maisha yake na mtoto wake aliyezaliwa Agosti 8, mwaka huu.

Kulingana na marafiki wake wa karibu, Hamisa Mobetto anaishi na wasiwasi kutokana na vitisho anazozipata kila siku kutoka kwa baba ya mtoto wake. Chanzo kimoja kutoka familia ya Hamisa kilisema;

“Unajua baada tu ya kujifungua kulienea habari nyingi kuwa mtoto huyo ni wa msanii huyo hasa baada ya Hamisa kumpa mwanaye jina hilo. Kilichofuata, kwanza msanii huyo alikimbilia kwenye media (vyombo cha habari) kukanusha habari hizo ambazo zimekuwa zikizagaa kwa kasi ya moto wa kifuu. Unajua jamaa (msanii huyo) alidhani kuna siri chini ya jua kuwa anaweza kuficha jambo hilo maana watu walikuwa wakimchomea kwa mpenzi wake ambaye amezaa naye.

Aliendelea kusema,

“Ili kumziba mdomo Hamisa, msanii huyo aliona ni bora amkane mapema lakini Hamisa siyo wa mchezomchezo maana aligoma kuficha ishu hiyo. Baada ya kuona anaweza akabumburua ishu, msanii huyo alimpiga biti asizungumze na vyombo vya habari kabla ya kumwekea ulinzi wa chinichini kuhakikisha waandishi hawamfikii Hamisa. Sehemu pekee ambayo Hamisa aliona jamaa huyo hawezi kumzuia ni kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii hasa Instagram na Snapchat ‘so’ akawa anaposti vipande vya baadhi ya viungo vya mtoto huyo. Sasa baada ya kuona hivyo, msanii huyo ambaye alikwenda mara moja tu kumuona mtoto huyo alianza kumpigia simu na kumtumia meseji za vitisho. Wewe fikiria Hamisa na kichanga chake sasa anaishi kwa hofu maana jamaa amemuambia kama atafunguka kuwa amezaa naye atamuondoa uhai yeye na mtoto wake. Hali hiyo imeifanya family ya Mobeto iwe na hofu kubwa na ili kujiweka salama, aliona ni bora aende polisi kuripoti ili kama kutakuwa na jambo lolote baya litakalomkuta yeye na mwanaye, basi mhusika atakuwa ni msanii huyo. Mwanzoni tulidhani ni ishu ndogo lakini kwa vitisho anavyopokea Hamisa, vinamnyima raha na kumfanya alie tu.

Akaongeza kuwa…

Hamisa Mobetto na mwanae
Hamisa Mobetto na mwanae

“Kiukweli Hamisa anatia huruma sana na anahitaji msaada kwa sababu mbali na msanii huyo pia anapata vitisho kutoka kwa mpenzi wa jamaa huyo. Sasa watu wanajiuliza, wakati anatembea naye hakujua kuwa kinaweza kupatikana kiumbe? Na kwa ustaa wake anashindwa nini kulihendo suala hilo kwa busara ili lisimchafulie kuliko kutoa vitisho hivyo?” kilifunguka chanzo chetu hicho na kuongeza. Hata kwenye ukurasa wake wa Snapchat, Hamisa ameshatahadharisha juu ya kutishiwa kuuawa yeye na mwanaye.”
Baada ya kunyetishiwa ubuyu huo, Ijumaa liliperuzi kwenye ukurasa wake huo na kukutana na ujumbe wa Hamisa uliosomeka:
“Mlidhani atafia tumboni enh…au mlijua nitafia leba…. nyie siyo Mungu na hamtakaa kuwa kamwe…& if anything bad and I mean anything bad happens to me or my son hatutawaacha salama!!!”

 

Hamisa na yeye aka sema;

‘MIMI NA MWANANGU TUNAUAWA WAKATI WOWOTE’ Ni kweli mimi na mwanangu tunauawa muda wowote. Nina ushahidi wa kutosha wa vitisho so nimeona ni vyema nitoe taarifa kwenye vyombo vya usalama,”

Alikiba awachia video mpya – seduce me

King Kiba ameachia video ya wimbo wake mpya Seduce me hivi leo miezi kadhaa baada ya kukawia kimya.

Msanii huyo amewachia wimbo huo wakati kuna tetesi kadhaa za kuchambuliwa na Diamond Platnumz kwenye mix ya Fresh.

Wimbo huu umewaacha mashabiki wake kama wameridhika baada ya kusubiriwa kwa hamu. Wimbo huu umetengezwa chini ya kampuni ya Rockstar4000 Music Entertainment and Rockstar Television inayommiliki.

Itazame hapa