Harmonize azungumzia kuhusu mjengo wake

Muimbaji kutoka label ya WCB, Harmonize amefunguka kuhusu mjengo wake ambao ni wa ghorofa akizungumza kwenye mahojiano hivi karibuni.

Kulingana na Harmonize mjengo wake unawezekano wa kukamilika mwishoni wa mwaka huu. Hata hivyo, Harmonize alikataa kufunguka kuhusu gharama aliyotumia kutengeneza ghorofa hiyo.

Harmonize alisema;

“Kwa hiyo flow ya kwanza tayari bado ya pili, kidogo kidogo tunajikongoja tukipata 200 tunaweka. Sio kitu kizuri kusema (gharama) nadhani lakini imetumia hela nyingi”

Harmonize aliendelea kwa kudai….

“Siwezi nikakadiria lakini imekula hela nyingi, show zenyewe hizi kwa mwaka sita/saba na usawa wenyewe ulivyo mgumu lakini nashukuru sio show pekee zinazonipatia hela kuna mishe nyingine, kwa hiyo siwezi kujua ni kiasi gani imekula lakini imekula hela nyingi,”

Ben Pol aweka wazi kwa nini hataki kuongelelea maisha yake ya kibinafsi kwa sasa

Muimbaji wa bongo, Ben Pol amefunguka kudai kuwa kwa sasa hataki watu wamuulize kuhusu maisha yake ya kibinafsi wala mahusiano yake, Ebitoke na mtoto.

Hii ni kwa sababu ya kazi anayoifanya kwa sasa. Akizungumza kwenye mahojiano, Ben Pol alisema;

“Kwa series ya kazi zangu zinazokuja ningependa sana vitu binafsi nisiviongelee zaidi au hadi pale nitakapokuwa tayari kuzungumzia Ben Pol anafanya nini sasa hivi nianze kuzungumzia,”

Akaendelea kwa kusema;

“kwa hiyo sipo comfortable sana kusema vitu binafsi mahusiano, sijui mtoto nataka kupunguza kuvizungumzia hivyo vitu kwa sasa hivi kusema kweli,”

 

Daktari maarufu Bongo adai kuwa Wolper ni ‘Wife material’

Japo Wolper bado hajapata mtu ambaye anaweza kumuoa mrembo huyu wa muvi za bongo sasa hivi anatoka na mwanaume ambaye anasemekana ni mdogo kumshinda.

Hii iliwafanya watu wengi kumchana lakini Daktari mmoja kutoka Bongo, Dk Fadhili Emily ameonekana kuwa na maoni tofauti. Akizungumza katika mahojiano alisema kuwa mrembo huyu akona uwezo wa kuwa mke mzuri kwam tu yeyote.

“Nimeona kwenye mitandao, wanamuandama kuwa hajatulia na kwamba ana msururu mkubwa wa wanaume ambao ametembea nao, kimsingi huyu mrembo hajapata tu mtu sahihi lakini anafaa kuwa mke wa kulea familia kabisa,”

Hata hivyo daktari huyu pia anasemekana kuwa hapo awali alitoka kimapenzi na Wolper lakini wakamwagana kwa sababu ambazo sio wengi wanajua.

 

Zari Hassan na Diamond Platnumz washerehekea siku ya kuzaliwa ya mtoto wao, Princess Tiffah

Diamond na mpenzi wake Zari The Bosslady walisherehekea siku ya kuzaliwa ya Princess Lattifah Jumapili hii iliyopita kwa kumuandikia ujumbe ambao umewaacha wengi wakifurahia kupitia mitandaoni yao ya Instagram.

Hii ni baaad ya Zari alipojifungua mtoto wa kwanza wa miaka miwili iliyopita. Kupitia mtandao wa instagram, wazazi hao walionyesha furaha zao kupitia ujumbe wao.

Zari aliandika,

“It’s princess world…happy birthday my one and only princess_tiffah.”

Na akaongeza kusema;

“My Princess….. May God see you through with nothing but the best. May you be blessed from this day forward. Most of all, May you be a Godly child. Without God we are nothing. Happy birthday @princess_tiffah,”

Diamond Platnumz naye akaandika;

“Happy 2 years mama, Words Can’t express how much i love you my Tee….

Tiffah ni miongoni mwa watoto maarufu Africa yote.

 

Jini Kabula aeleza familia yake ilivyomtemga baada ya kuugua ugonjwa wa akili

Miriam Jolwa anayetambulika Kama Jini Kabula ni muigizaji aliyepata umaruufu kupitia tamthiliya ya Jumba la Dhahabu. Hata hivyo kwa hivi sasa anaonekana hali ya akili haiko sawa.

Baada ya Wolper kujitokeza na kuwaomba wasanii wenzake kumsaidia Jini, Global TV online iliweza kukutana na yeye Bamaga- Mwenge jijini Dar es Salaam ambapo walizungumza na yeye na kulingana na walichotangaza, ni kweli Jini anapitia wakati mgumu.

Mrembo huyu alifunguka kudai kuwa wetu ana tatizo kwenye akili yake na akaendelea kukiri kuwa ndugu zake walimpeleka Muhimbili ambako alilazwa kwenye wodi ya wagonjwa akili kwa zaidi ya mwezi mmoja na kumtenga.

Kwa Sasa hana sehemu ya kuishi na ndugu, jamaa na marafiki zake, wamemtenga kutokana na matatizo aliyonayo na kumbidi kutangatanga mitaani.

Tazama mahojiano yao hapa;

Faiza Ally aachia picha za mtoto wake, Lil Junior

Muigizaji wa Bongo muvi ambaye pia ni mwanabiashara , Faiza Ally, alijifungua mtoto wa kiume na amempa jina la Lil Junior.

Faiza Ally

Mrembo huyo pia hivi Leo amewachia picha kadhaa kumuonesha mtoto wake ambaye anaaminika kuwa muindi au mzungu. Kupitia mtandao wake wa Instagram aliandika kusema;

“Asanteni sana ndugu zangu Watanzania nimeishiwa na maneno kwa mapenzi yenu. Najiona kila kona kwenye kurasa mbalimbali za marafiki, umbea, habari yaani najihisi kupendwa. Na nimezidi kutambua kuwa uwepo wangu upo, naomba niwaambie nawapenda sana, natambua uwepo wenu wote, natamani ningejibu kila comment , nipite kila kurasa, nijibu msg zote DM na WhatsApp ndiyo usipime yote hayo ni mapenzi, najisikia baraka kwa kweli, furaha yangu inazidi mara dufu ALHAMDULILLAH. Nawatakia kila la kheri na baraka tele kwenu, wanaotafuta watoto Mwenyezi Mungu awajaalie kila la kheri mpate, na waliopata INSHAALLAH, Mwenyezi Mungu awatunzie wawe watoto wenye baraka kwenu AMEN YARAB. Nawapenda Watanzania, naipenda Tanzania, Mungu tubariki sisi na vizazi vyetu AMEN.”

Tazama picha hiyo hapa;

Wolper awasihi raia na wasanii wa Bongo movie kumsaidia Jini Kabula anaye Ugua

Jackline Wolper ambaye ni malkia wa bongo movie amejitokeza kuwaomba wasanii wenzake na raia pia kumsaidia Mariam Jolwa anayejulikana kama Jini Kabula aneyeugua ugonjwa wa akili.

Kupitia mtandao wake Wa a Instagram Wolper aliandika kusema;

Natamani niongee mambo mengi sana juu yako lakini natamani ata kukusaidia urudishe akili yako swali ni kwamba nimechelewa??nakama nimewahi je nitafanikiwa kweli. sasa tuzungumze jambo jamani maana siju hizi tarfa tunazipata insta naona nalangu niliongelee insta wanatasnia wenzangu tunamsaidiaje mwenzetu nini kimekuta kipi je nayoyasikia ndio hayo????nakama ndio mbona kuna wataalam wakusena nae naakakaaa sawa. Basi watanzania wenzangu naombeni tuchangie maoni yenu hapa nakama nim2 uwezi toa ushauri hapa basi tuma msg kwakupitia cm hii 0765776776 basi tuweze kumrudisha kabula jamani. naandika msg hii huku nalia namoyo mdogo sana usiweza kuvumilia naumivu nakumbuka nimishawahi kumwambia kabula we nimwanamke mzuri sana bongo movie lkn natamani kujua tatizo nini kacheka tuu akachukua nguo akaondoka sikupata muda wakuzungunza nae ….sasa npo safarini hope kesho au kesho kutwa nikijaliwa tukutane kwaoamoja .. Bongo movie tumfwate alipo jamani tujue tunamsaidiaje nimeona vdio anaongea sjui niamechanganyikiwa masikn me ata nashindwa kuandika jamani ….

Nuh Mziwanda akiri kubadili dini

Mkali wa Bongo Fleva Nuh Mziwanda amesema kuwa Sasa yeye ameirudia dini yake ya kwanza, Mkristo, baada kuachana na aliyekuwa mke wake.

Nuh alisema haya baada ya kuzungumza na XXL ya Clouds FM, huku aliendelea kusema ni kweli alikuwa kanisani Jumapili hii iliyopita na kukiri kuwa habari zinazoenea mitandaoni ni za kweli. Msanii huyu alisema;

“Nimerudi kwa Mungu wangu ili mambo yangu yaende vizuri maana tunafanya muziki wa dunia anatusamehe ila kurudi kwake pia ni jambo la kawaida sana.”

Aliendelea kwa kujibu tariffs zilizotolewa na aliyekuwa mke wake kuwa ameacha kumjali mtoto wake. Nuh alisema;

“Mara ya mwisho nilikuwa na Anyagile kwenye photoshoot ya ngoma yangu mpya jana kwa Mx Carter, inayotoka hivi karibuni sasa yeye anavyosema sijamuona mtoto muda mrefu sijui anamaanisha nini. Anaongea vibaya kwenye media sio vizuri, mimi na fan base yeye mwanamke anatakiwa ajue anaongea nini, ila muache aongee akikua ataacha, vile vile mimi sina tatizo naye kama kaolewa, yeye si ndio kaamau mimi bado kijana na kila mtu anafanya anachotaka mimi nimemrudia mungu huwezi jua atanipatia mke mwingine mwema”.

Faiza Alley ajifungua mtoto wa pili (video)

Mrembo wa Tanzania na pia malkia wa Filamu Faiza Alley amejufingua mtoto wa pili kulingana na ujumbe alioweka mtandaoni wake wa Instagram.

Faiza Ally
Faiza Ally

Faiza ambaye anatambulika na wengi kutokana na mavazi yake ya kushangaza alitangaza habari hizi kwa kuweka video fupi ya mtoto huyo akiwa hospitalini, na kuandika

“ALHAMDULILLAH @lijunior_ well come to the world baby.”

Faiza amejiunga na wanawake maarufu bongo waliobahatika kupata watoto mwaka huu. Tazama video hiyo hapa;

https://instagram.com/p/BXUSHSigswW/

Hamisa Mobetto aachia picha mpya kuonesha ujauzito wake

Mrembo wa Tanzania Hamisa Mobetto leo ameachia picha mpya huku akionekana kuonesha ujauzito wake kupitia mtandaoni wake wa Instagram.

Hamisa Mobetto aliambatanisha picha zake kwa kuweka wazi kuwa amemfungulia mtoto anayemtarajia akaunti mpya ya Instagram ambayo ameiweka jina la ‘Tanzanian baby’ na kufikia saa hii imepata followers/mashabiki 4702.

Hata hivyo Hamisa ameweka picha mbili ambazo amevalia nguo nyekundu huku akionekana amekumbatia mimba yake. Tazama picha hizo hapa;

Abdu Kiba adai hajamuona wa kushindana na Ali Kiba

Msanii wa bongo Abdu Kiba amefunguka kudai kuwa kaka yake, Ali Kiba, ni msanii ambaye bado hajapata mtu ambaye anaweza kumfikia ikifikia wakati wa kutunga na kuachia nyimbo.

Akizungumza na kipindi cha XXL cha Clouds Fm hivi karibuni Abdu Kiba alisema kuwa yeye na Ndungu yake hawapendi kuhusishwa na team za kimuziki au kuonekana wanajipanga kushindana na watu fulani.

Aliendelea kwa kusema kuwa yeye na Kaka yake bado wanafanya kazi ambazo bado hawajapata watu wa kushindana nao.

“Sisi tunachukulia ni changamoto kwa sababu sisi hatushindani, tunafanya kazi na hatujaona bado wa kushindana nao, hakuna mtu wa kushindana na sisi, yaani sijamuona wa kushindana naye na hakuna wa kushindana na sisi na sisi hatushindani,”

 

Shetta hatimaye awajibu mashabiki wake

Msanii wa bongo Shetta aliachia ngoma yake mpya ‘Wale Wale’ hivi karibuni na kulingana na YouTube inaonekana kuwa Shetta aliangusha wimbo ambao umewaacha mashabiki huku kama wamefurahi.

Hata hivyo, Shetta ameonekana kuwajibu mashabiki wanaodai asikae kipindi kirefu bila kutoa ngoma.

Shetta

 

Hii ni baada ya kukawia zaidi ya miezi 10 bila  kutoa wimbo. Akizungumza na E-Newz ya EATV Shetta alisema;

“Mimi naamini katika kitu ambacho nakifanya, nimeshauriwa nifanye back to back lakini hata hiyo itaongezeka ngoma moja au mbili, sidhani kama natakiwa nifanye vitu ambavyo watu wanasema au wanafikiri ni sawa, mimi natakiwa niamini katika kitu ambacho nafanya,”

Aliendelea kwa kusema;

“Lakini kutokana mashabiki wanataka pia nafuata kile wanachopenda nitajaibu kubadilika ila katika moyo wangu siamini katika kutoka nyimbo nyingi. Bajeti pia huwa inabana kutokana kitu ninachotaka kukifanya pia ni kikubwa,”

Hii ndio sababu Barnaba hataki kufanishwa na mtu yeyote

Msanii wa Bongo Fleva, Barnaba amesema kuwa hakuna msanii yeyote Bongo anayeweza kufananishwa naye kwa sababu yeye anauelewa muziki ambao anaoufanya.

Akizungumza na Mikito Nusunusu , Barnaba alisema kuwa kipaji chake amekitoa kwa mungu na anamshukuru Mungu kwa kumjalia kipaji cha kipekee kwenye muziki na kwamba ataendelea kukitendea haki. Alisema;

“Mimi ni mwanamuziki na si msanii, lazima kwanza utofautishe mambo hayo mawili, ndiyo maana ninaweza kutunga na kuimba na hata kutumia vyombo vyote vya muziki, hiyo ndiyo maana halisi ya mwanamuziki. Naomba sana nisifananishwe na mtu kwenye eneo hilo. Nilizaliwa kuburudisha watu na ninafanya muziki kama sehemu ya maisha yangu, siangalii fedha na masilahi, muziki uko kwenye damu,”

Shilole atangaza harusi baada ya kutolewa posa

Kuna fununu kuwa msanii wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ au ‘Shishi Baby’ ametolewa posa na mchumba wake ambaye bado hajamjulisha kwa mashabiki wake.

Kulingana na chanzo kilicho ongea na Ijumaa Wikienda inasemekana kuwa shishi hataki watu wakimjua mwanaume wake kwa ajili anataka kuiweka ndoa yake iwe Siri, chanzo hicho kilisema;

“Si unawajua tena mastaa wetu? Hawachelewi kufanya yao ndiyo maana Shishi hataki kumwanika mwanaume wake kwa madai kwamba anaogopa wajanja wasije wakapita naye kama ilivyo kwa yule aliyekwapuliwa na Nisha (mwigizaji Salma Jabu).”

Aliendelea kwa kusema;

“Baada ya mbilingembilinge nyingi za mjini, hatimaye Shishi sasa anaolewa na hapa tunapoongea ndiyo kwanza watu wamerudi Dar kutoka Igunga (Tabora) nyumbani kwa akina Shishi kupeleka posa. Kwanza ishu ilikuwa ni kumtambulisha mwanaume kwao ndipo wakaona wamalize kabisa na suala la posa hivyo kifuatacho ni kufunga ndoa ambayo nasikia itakuwa ndani ya mwaka huu,”

Hata hivyo Ijumaa Wikienda ilipompigia Shishi kujua kama ni ukweli alifunguka kusema;

“Wewe ujue tu ni kweli nimechumbiwa lakini kuhusu kumwanika mtarajiwa wangu, kwa kweli sipo tayari. Maana kwa upande wa wanaume wanaonyatia wanawake wa watu wanaitwa Team Fisi, sasa sijui kwa upande wa wanawake. Au tuseme Team Fisi kwa upande wa wanawake.”

Aliendelea,

“Lakini kimsingi mchumba wangu ni mtu wa kawaida sana na siyo staa,” alisema Shishi na kutoa mwanya kwa mahojiano zaidi kuhusu ishu hiyo.

Kuhusu harusi yake Shishi alisema,

“Mashabiki wangu wajue tu itakuwa soon na itakuwa ya aina yake kwani itafanyika uwanjani na mashabiki wataingia kwa kadi. Mchango utakuwa mdogo ili watu wengi zaidi wahudhurie.”

“Nisipobahatika kupata mtoto nitafunga uzazi” Wema Sepetu asema

Tanzanian sweetheart Wema Sepetu hi karibuni alifunguka kuhusu suala la kupata mtoto katika mahojiano aliyofanya na gazeti la Ijumaa Wikienda hivi karibuni.

Mrembo huyu ambaye ni mmoja wa waigizaji ambao wamefanya vizuri kwenye industry ya Tanzania amedai kuwa kwa sasa akona mpenzi ambaye wametulia pamoja na pia wanajaribu kupata mtoto pamoja.

Wema Sepetu

Aliendelea kwa kudai kuwa baada ya kupoteza mapacha wake imemchukua muda kuwasahau lakini kila kitu hufanyika kwa nguvu za mwenyezi mungu.

Hata hivyo aliweka wazi kuwa asipopata mtoto kabla ya kufikia miaka 32 basi atafunga kizazi. Lakini akona uhakika kuwa atapata mtoto kwani amepata ufumbuzi wa kitaalam na kujua tatizo lake ni lipi. Alisema;

Ndiyo na tena safari hii nisipobahatika kupata mtoto hadi ninafikisha umri wa miaka 32 (kwa sasa ana 29), nitafunga kizazi.

 

Aunty Ezekiel avunjika moyo baada ya ‘mama’ yake kufariki

Wikendi hii iliyopita mrembo wa filamu za bongo Aunty Ezekiel alimpoteza nyanya yake ambaye alimlea toka utotoni na kulingana na habari zinazoenea, bibi yake alikuwa kama mama na baba kwake baada ya wazazi wake kufariki.

Picha zinazoenea mitandaoni Aunty Ezekiel anaonekana kuwa na majonzi mengi lakini marafiki zake walikusanyika kumfriji huku wengi wakiandika ujumbe kupitia nguvu kumtia nguvu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Aunty Ezekiel aliandika kusema;

Kweli la mungu halina muhamuzi mungu akuweke mahari pema peponi bibi