Wema Sepetu awazingua wengi na picha mpya, ni kweli ameumbwa akaumbika!

Mrembo wa Tanzania Wema Sepetu amewapa mashabiki wake kitu kipya cha kuongelea baada ya kuachia picha zake mpya kupitia mtandao wake wa instagram.

Picha hizi zimekuja baada ya Wema Sepetu kwenda kimya kwa muda mrefu lakini kulingana na maoni walioacha wafuasi wake inaonekana kuwa bado wanampenda muigizaji huyu.

Ingawa pia hakuwachia picha nyingi kama anayvopenda, Wema Sepetu alihakikisha kuwa mashabiki wake wana sababu ya kuongea mitandaoni.

Tazama picha hizo hapa chini na utoe maoni yako.

Rais wa Tanzania atuma pole na salamu za rambirambi kwa familia ziliopoteza wapendwa wao kwa ajali

Rais wa Jamhuri Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewaunga wengi kuwapa pole wazazi na familia ambazo zimewapoteza wapendwa wao baada ya ajali ambayo ilitokea Jumamosi saa 3 asubuhi.

Rais wa Tanzania
Rais wa Tanzania

Ajali hiyo ilisababisha vifo vya wanafunzi 32 wa darasa la saba, walimu 2 na dereva wagari la shule ya msingi iitwayo Lucky Vicent ya Arusha. Hii ilitokea baada ya gari waliokuwa wakisafiria kuacha njia eneo la Rhotia Marera na kutumbukia korongoni.

Kulingana na habari inayoenea mitandaoni watu watatu waliepuka na majeruha na kupelekwa hospitali. Rais Magufuli amezitoa rambirambi zake kupitia barua hii.

Baada ya kuachia nyimbo mpya, Rich Mavoko afunguka kuhusu kitu anachokifanya kwa sasa

Rich Mavoko ambaye anafanya muziki chini ya Wasafi records hivi sasa anajipanga kuachia album mpya hivi karibuni baada ya collabo yake ya Show me na Harmonize.

Ingawa umaarufu wake sio kama wa Rayvanny na Harmonize muimbaji huyu anajikaza kufikia kiwango ambacho wasanii wote wa Wasafi records wako.

Akizungumza kupitia kipindi cha Top 20 cha Clouds FM kuwa, Rich Mavoko alisema kuwa yeye mwenyewe hufika saa 12 jioni studio ilikufanya kazi hadi saa 12 asubuhi kwa sababu hivi sasa anamipango ya kuachia album ambayo itakuwa yake ya kwanza. Alisema,

“Hii itakuwa albam yangu ya kwanza kubwa kufanya, nilishawahi kutengeneza na watu wangu wa mwanzo ila haikufanikiwa kutoka.”

Hata hivyo kuna matumaini kwamba Rich Mavoko ataendelea kuwavutia mashabiki kwa wingi baada ya project hii yake mpya.

Linah achanwa mitandaoni baada ya kuachia picha hii

Linah ambaye akokaribu kumkaribisha mtoto wake wa kwanza hivi karibuni amewacha wengi wakiongea mitandaoni baada ya kuachia picha ambazo zinaonyesha uchi wa tumbo lake.

Muimbaji huyo aliwaacha wengi kama wamechanganikiwa baada ya rangi yake iligeuzwa na kuwekwa nyeusi huku akikaa nikama amepakwa mafuta mingi mwilini. Mmoja wa mashabiki wake aliandika kusema,

jumalokole2Kwanza najuwaga linna ni mweupe sasa sijui kapakwa nini na tarick,, pili aya mafuta ni ya kula au ya Nazi? . Maana umekandikwa ukakandikika haswaa. Kwani ukivaa dera tumbo alionekani? ?

Ingawa huu ndio mtindo ambao wanawake wengi wanaiga siku hizi, inaonekana Linah akufanya inavyotakikana. Tazama picha hiyo hapa.

Gabo afunguka kuhusu uhusiano wake na Wema Sepetu

Baada ya Wema Sepetu kuachia picha za kimapenzi akiwa na Gabo Zigamba, wengi hivi sasa wanaamini kuwa wawili hao wanatoka kimapenzi kitu ambacho Gabo amekana.

Gabo Zigamba pia amekuwa akizipata habari ambazo zinadai kuwa hivi sasa anamchumbia wema lakini kwa mara ya kwanza ameweza kufunguka kuhusu uhusiano wao. Muigizaji huyu amefunguka kwa kusema kuwa picha zake na Wema Sepetu ni za kikazi wala sio kimapenzi.

Alisema kuwa picha hizi zinaonekana kuwa zakimahaba kwa sababu hivi karibuni wanapanga kuachia movie itwayo Heaventsent ambayo inazungumzia mapenzi. Alisema,

“Movie tunayoifanya na Wema iko very tomantic ndio maana hata picha zenyewe lazima ziwe hivo sasa watanzania naona wao washarasimisha kwamba kuna kitu kinaendelea kumbe hakuna pale tupo kazini na niwaahidi mashabiki zangu naanda kitu kikali sana mara mbili za jinsi wanavyonifahamu.”

Muigizaji huyu amesema haya wiki kadhaa baada ya Wema Sepetu pia kukana mahusiano yake na Gabo.

Hizi ndizo pesa Harmonize anapata kupitia YouTube

Harmonize ambaye ni msanii kutoka Bongo amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu pesa ambazo yeye hupata kupitia mtandao wa Youtube kwa Mwezi. Muimbaji huyu ambaye anafanya na Wasafi records alikuwa akiongea na Clouds FM alipotaja pesa mbazo kwa hivi sasa anapata.

Kulingana na yeye anapata kiwango cha Dola 3,500 ambazo zimeweza kuchangia kwa maisha yake ya kifahari. Harmonize alisemakuwa pesa hizi ndiyo zimemuwezesha kutembelea magari ya kifahari ambazo mashabiki hushindwa katoa wapi.

Msanii huyu alisema,

“Namshukuru Mwenyezi Mungu Kupitia muziki umenikutanisha na watu wengi,Umenipa Dili napata riziki kwenye njia tofauti tofauti,sio tu kwenye show,licha ya kufanya show nauza nyimbo zangu kwenye Platform,Mimi akaunti yangu ya Youtube kila mwezi nalipwa Dola 3,500.”

Hata hivyo sio siri kuwa muimbaji huyu amejikaza kimziki na ndio maana maisha yake yamebadilika.

Hatimaye Shilole apata mwanaume wa kumuoa

Kuna fununu kwamba Shilole amepata mchumba kulingana na magazeti wanavyosema mitandaoni. Mrembo huyu ambaye ameweza kuwa na wanaume kadhaa bongo hatimaye amepata mtu ambaye anamtuliza kiroho na kiakili.

Kulingana na Global Publishers Shilole amempata mwanaume mchumba ni dereva wa bodaboda Kinondoni. Waliendelea kusema kuwa chanzo cha habiri hizi kilikiri kuwa Shilole na mchumba wake wanatarajia kufunga ndoa ya siri kabla ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kuanza.

“Shilole anatarajia kufunga ndoa na dereva bodaboda hivi karibuni kabla Waislamu kuingia kwenye Mfungo wa Ramadhan na itakuwa ya siri, nyie fuatilieni mtaujua tu ukweli,” kilisema chanzo.

Hata hivyo Shilole ambaye aliweza kuongea na wanahabari alisema kuwa ni kweli kuwa amepata mchumba lakini akikataa kumuweka wazi kwa sasa. Aliendelea kwa kusema kuwa Mchumba wake siyo siyo dereva wa bodaboda kama watu wanavyosema.

“Ni kweli nina mchumba, ila siyo dereva bodaboda, ni fundi magari, tuko kwenye utaratibu wa ndoa na nitawajulisha maana ndoa yangu haitakuwa ya siri, itakuwa ya wazi na itafungwa kwenye ndege,” alisema Shilole.

Baada ya ‘Muziki’ Darassa apanga kuachia nyimbo mpya

Darassa ambaye anatambulika Afrika Mashariki amewahaidi mashabiki wake nyimbo mpya ambayo aitawachilia hivi karibuni. Nyimbo hii inakuja miezi mitano baada ya kuachia Muziki ambayo imefanya vizuri baada ya kuangaliwa mara 7,056,225 YouTube.

Nyimbo hii ambayo inaitwa Hasara Roho ndio itakuwa project yake ya kwanza mwaka huu na mashabiki wake wameonyesha furaha kwani wameigonja project nyingine kutoka kwa Darassa.

Darassa

Kupitia Instagram yake Darassa aliandika kusema,

“Good morning from Bongo Tanzania East Africa to the Top of the world!. Nataka kusema asanteni sana kwa love na support ambayo mmetupatia kwenye project yetu ya ‘Muziki’ na kuipelekea kuwa National Anthem. Hakuna neno linaweza kumaanisha thamani yenu kwetu! God bless you all usikose kusikiliza project yetu mpya leo ??? #CMG#HasarARoho,”

Hanscana ambaye ni mmoja wa manager wake aliambia Bongo5,

“Sisi tumejiandaa vizuri kwa sababu tunajua mashabiki wanataka nini. Maandalizi ni makubwa sana, yaani ni kama tunaandaa Marais 5 wa nchi. Kwahiyo tumejipanga vizuri kuhakikisha jamaa anarudi vizuri katika game,”

Kesi ya Wema Sepetu ya hairishwa baada ya upelelezi kukamilika

Jumanne hii Wema Sepetu na wakili wake waliweza kufika kotini kuskiza kesi ya malkia huyu wa filamu miezi miwili baada ya kusemekana anatumia dawa za kulevya.

Wema Sepetu aliweza kufika mahakama ya hakimu mkazi kisutu, Dar es salaam, ambapo hakimu mkuu aliwajulisha kuwa upelelezi wa kesi hiyo ulikuwa umekamilika na mrembo huyo sasa amebaki kusomewa mashtaka baada ya kupatikana na msokoto wa bangi nyumbani kwake.

Hata hivyo Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, alisema kesi hiyo itaskizwa June 1, ambapo Wema Sepetu ataweza kujibu mashtaka yake kwa mara ya kwanza.

Wakili wa mrembo huyu hata hivyo akona imani kuwa watashinda kesi hii.

Emmanuel Mbasha asema kuwa Flora hakumkimbia kutokana na ukosefu wa pesa

Muimbaji wa nyimbo za injili Tanzania, Emmanuel Mbasha amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya mama ya watoto wake Flora kufunga ndoa na mwanaume mwingine.

 

Emmanuel Mbasha ambaye ni mmoja wa waimbamji maarufu Afrika mashariki ameweka wazi kuwa hana tatizo lolote na mwanaume aliyemuoa Flora. Hata hivyo alitaka watu kujua kuwa Flora hakumtoroka kwa sababu hakuwa na pesa lakini ni kwa sababu ya maisha mbayo yeye mwenyewe alitaka.

“Jamaa ambaye amemuoa Flora sina shida naye, anaweza kuwa mtu ambaye ananihofia kuwa nikikutana naye naweza kumdunda.Ila huyo jamaa mimi simchukii na wala simjui. Hajawahi kuniingilia kwenye issue yangu yoyote ya mapenzi ila mimi namchukia jamaa ambaye aliniingilia kwenye ndoa yangu ndiye mbaya wangu, na Watanzania wote wanamjua,”alisema Mbasha.

Hata hivyo anawatakia kila la heri kwenye Ndoa yao.

Madee atisha baada ya kuonyesha gari ‘yake’ mpya

Msanii wa Bongo Madee ni mmoja wa watu ambao wanapenda kuonyesha vitu vyao vya thamana mitandaoni. Kama sio saa ni viatu ama kitu kingine.

Lakini hivi karibuni aliwaacha mashabiki wake kama wameduwaa baada ya kuonyesha gari ambalo lina jina lake kwenye number plate.

Hata hivyo Madee hakudhibitisha kuwa gari hilo ni lake lakini aliandika kusema, “Gangster paradise!!! #WinoMweusi,” huku akiwapa mashabiki wake nafasi ya kubashiri ikiwa amenunua gari.

Kama kawaida wengi walimpongeza na wengine wakimsomea kwa kuwaringia na gari ambalo wanajua sio lake. Madee hata hivyo hakuwajibu kwani yeye anaishi maisha ya super star.

Tazama gari hilo hapa.

“Mimi sina mpenzi” Ray C asema

Ingawa Ray C ni mrembo na mwanamke mwenye umbo la malkia bado hajaweza kuanza familia yake kwani hivi sasa hana mpenzi wala hana haraka ya kutafuta mtu wa kumpenda.

Muimbaji huyu amesema kuwa sasa hivi mawazo yake yote yako kwenye muziki na siyo mapenzi. Ray C ambaye alikuwa amepotelea kwenye madawa ya kulevya amejipa muda kufanya kazi yake ambayo aliiwacha baada ya haijakamilika baada ya kuzidiwa na raha ya madawa ya kulevya.

Ray C
Ray C

Hata hivyo akizungumza katika interview Ray C aliweza kusema kuwa hivi sasa anaonelea kuachilia nyimbo ambazo mashabiki wake watafurahia kabla ya kufikiria ikiwa atatafuta mpenzi wa kutulia na yeye. Alisema,

“Mimi sina mpenzi. Kwa sasa nafikiria kuhusu muziki wangu sitaki kujichanganya na mambo mengine. Mashabiki wangu wamenipambania kwa muda mrefu siyo kwaajili ya mpenzi wangu, wao wanataka kazi, muziki mzuri.”

Ruby afunguka baada ya kusemekana anatoka kimapenzi na Alikiba

Iwapo hauna habari basi hivi karibuni muimbaji wa Bongo Ruby alisemekana kuwa ndiye mpenzi mpya wa Alikiba. Taarifa hizi zilisabaa kwenye mitandao baada ya wawili hao kuonekana wakiwa pamoja mara kadhaa.

Hata hivyo Ruby ameweza kufunguka kuhusu taarifa hizi na kukana waandishi wanachoandika mitandaoni. Kulingana na Ruby hakuna kinachoendelea kati yake na Kiba huku akiendelea kwa kusema kuwa hata hana namba ya muimbaji huyo.

Ruby
Ruby

Hii sio mara ya kwanza Ruby kusingiziwa kuwa anatoka kimapenzi na msanii wa bongo. Hapo mbeleni ilisemekana kuwa alikuwa na uhusiano na Diamond Platnumz hata hivyo sio wengi walioamini.

Akizungumza na Bongo 5 Ruby alisema,

“Na mimi taarifa hizo nimekuwa nikiziona kama wewe ulivyoziona, sioni jipya kwasababu walishawahi kusema kuwa nipo karibu sana na Diamond, sasa wamegeukia kwa Kiba ambaye hata mawasiliano yake sijawahi kuwa nayo.”

Diamond Platnumz awaandikia barua wasanii wanaokosoa nyimbo zake

Diamond Platnumz hivi karibuni aliwaandikia wasanii wenzake barua huku akiwasihi wanapoandika nyimbo zao lazima wawe na malengo ya kuwafikia watu wengi na sio watanzania peke yao.

Kupitia mtandao wake wa Instagram Diamond aliandika huku akitoa mfano wa muziki wake. Kulingana na alichaondika Diamond Platnumz alisema kuwa muziki wake umemfungulia njia za kupiga show nchini ambazo yeye hakuwa anajua anaweza kufika.

Mkali huyu wa bongo aliandika kusema

Leo ningependa nitoe ujumbe huu kwa wasanii wenzangu pendwa… Siku hizi mjini kila mtu anajifanya yeye soko la Muziki analijua sana na bingwa wa kuelekeza na kukosoa nyimbo za watu….Pasipo kujua kuwa kila nyimbo ina soko lake na kila mwanamuziki anapotoa nyimbo anakuwa na malengo ama plan ambayo ameidhamiria…leo ntakupostia baadhi ya nyimbo ambazo wakati nazitoa zilidharauliwa, zilipingwa sana na wanaojifanya wajuaji wa Muziki… pasipo kujua kuwa dhamira ama nini yalikuwa malengo yangu….kwakuwa nilikuwa na imani na kufahamu nikifanyacho basi nikawa nawaekea tu neno #MALENGO na leo hii nyimbo hizo ndio sababu kubwa ya mimi kuwa na Show za nchi ambazo kiukweli sijawai tegemea fika na kufanya show za Uwanjani….. sababu yangu kubwa leo ni kuwasihi wasanii wenzangu kuwa mnapokuwa na kitu ambacho mnamalengo ama target nacho msiogope kukisimamia…lakini pia kuwajuza kuwa kila kanda ina maadhi ya muziki wake ambao unaupenda, hivyo ukitaka kufanikiwa kushika kanda zote usiogope kufanya Muziki tofautitofauti ili kuongeza Mashabiki ila ukiogopa kufanya muziki wa mahadhi flani kisa wabongo wataongea na kuamua tu kutoa kina “UKIMUONA” Basi hatutafanikiwa kuteka Masoko na chi zingine… #SimbaInZambia

Shilole adai kuwa anatamani kuolewa ila hajapata wa kumuoa

Shilole ambaye ni mmoja wa wasanii maarufu Afrika Mashariki bado hajapata mtu ambaye anaweza kufunga ndoa naye. Iwapo ameonekana na wanaume kadhaa, hakuna ambaye alifika kiwango cha kuwa mume wake.

Hata hivyo, msanii huyu anatamani sana kuoleka kitu ambacho watu wengi hawajui. Akizungumza na Showbiz Xtra hivi karibuni, Shilole alisema kuwa ni wengi ambao wanamtakia mambo mazuri ya ndoa lakini bado anamsubiri yule ambaye mwenyezi mungu atamletea.

Kwa sasa anaamini kuwa siku yake itafika na ataolewa na kuvalia shela (vazi la mwamke siku ya ndoa yake) kama bibi harusi wengine wanavyofanya.

shilole
shilole

Mrembo huyu alisema,

“Natamani sana na mimi nivae shela ila naamini wakati bado, najua nitavaa tu na watu wataongea sana maana wengine wanajua siwezi kuolewa ila Mungu atanifanyia wepesi na ndoa yangu itakuwa si ya nchi hii,”?|

Baada ya mashabiki kumfananisha na Jay Z, Joh Makini asema haya

Wengi wanaopenda nyimbo za Bongo wananamtambua Joh Makini kama mmoja wa wasanii ambao wanapiga nyimbo ambazo zinapendwa na wengi Afrika Mashariki.

Joh Makini kwa kweli anatalanta ambayo imempa uwezo wa kufanya kazi na wasanii wakubwa kutoka Afrika na iwapo ataendelea hivyo miaka ijayo basi anaweza pia fanya kazi na wasanii kutoka nje ya Afrika.

Jay Z

Kwa sasa wengi wanamfananisha na rappa wa Marekani Jay Z, kitu ambacho kimemfanya kufurahi sana. Japo anajua kuwa bado anavitu vingi vya kufanya kabla kumfikia mkali huyu, Joh Makini amesema kuwa mashabiki wake kumuweka kiwango cha Jay Z ni kitu kubwa sana.

Akizungumza muimbaji huyo alisema,

“Jay Z ni ‘role model’ wangu…mimi naimba maisha ya sinoni daraja mbili na Tanzania na Jay Z anaimba maisha ya Brooklyn na Marekani, nafikiri nipo katika ‘level’ ambayo hawaoni mtu mwingine wa kunifananisha naye… Kwahiyo mimi naona poa kwa sababu kama unanifananisha na Jay z ‘yeah i like it’ kuliko ungenifananisha na mtu mwingine”