“Labda nina mimba ya Wizkid” Gigy Money asema

Msanii na mrembo wa video Gigy Money amekuwa akisingiziwa kuwa anamimba kitu ambacho aliweza kufunguka kuhusu hivi karibuni.

Akizungumza na FNL ya EATV Gigy Money aligusia kuhusu wimbo wake mpya ‘Papa’, alafu baadae akaongeza kwa kana taarifa zinazodai kuwa anamimba huku akisema kuwa ameiambia FNL ya EATV kuwa anatamani sana kutoka kimapenzi na msanii Wizkid ambaye anaweza kumzalia.

“Kipindi cha sasa hivi na Papa ndio nimetoa?, hapana, ujue mpaka yananishtua maneno haya, you know sina mimba lakini labda nina mimba ya Wizkid unajua mimi natamani ikaenda ikashuka tu.”

Akamalizia kwa kusema;

“Yeah namkubali, unajua dream sio wote wanatimiza ndoto zao, mimi nimetimiza ndoto yangu, nilisema Tekno moyoni siumeona huyu hapa akajaa,”

Gigy Money kuwachia wimbo mpya – papa

 

Gigy Money ambaye ni video vixen amefunguka kudai kuwa anamipango ya kuachia wimbo wake wa pili unaoitwa ‘Nampa Papa’. Hii inakuja mwaka mmoja baada ya kuachia wimbo wake wa ‘Supu’ uliompa umaarufu Tanzania.

Mrembo huyu aliambia Bongo 5 kuwa wimbo huu ulitayarishwa na procuder Kimambo Touches. Aliendelea kwa kusema kuwa wimbo huu unasifia urembo wa wanawake na kuwa wengi wataufurahia.

“Nampa Papa ni wimbo fulani kama nyimbo zangu zilizopita, ni kama Supu nilikuwa najivunia maumbile yangu. Kwahiyo kwenye ‘Nampa Papa’ ni wimbo fulani ambao bila shaka kila mtu ataufurahia,”

 

Aliongeza,

“Kwahiyo mabibi na mabwana tukae mkao wakula Gigy kaleta balaa jingine jipya tuoneshe ushirikiano na thamini vya nyumbani. Pia wimbo huu sijaandika mwenyewe nimeandikiwa na mwanangu mmoja anaitwa Marioo,”

Gigy Money aeleza sababu hampendi Shilole

Mrembo kutoka Bongo Gigy money ambaye ni star wa video za mziki amefunguka kudai kuwa yeye si shabiki wa nyimbo za Shilole wala hampendi.

Gigy alisema haya baada akisititiza kuwa yeye binafsi ni fan wa hip hop na kwa hilo jambo, yeye anamsupport Rosa Ree. Aliendelea kwa kusema yeye angepata mtu wa kumuandikia mistari, panda kufanya muziki ambao ungewavutia mashabiki wengi. Mrembo huyu alisema,

shilole
shilole

“Sina hata mpango wala sitaki, sio fun wake (Shilole), labda Rosa Ree, tatizo la watu walio up wanasumbua, so hip hop its better, mimi ningepata mtu wa kuniandikia niwe nachana ningependa, I don’t love this kind of music ambayo nafanya, nafanya ili nipate hela, mimi napenda hip hop,”

Hata hivyo Gigy anaonekana kuwa na ‘beef’ na mastaa wa kike kutoka Tanzania.

Gigy Money amchana Wema Sepetu kwa Kumuita Fake woman

Hakuna anayejua kilichotokea katikati ya Gigy Money na Wema Sepetu lakini kuna fununu kuwa wawili hawa hawapatani hata kidogo. Hapo mbeleni wengi walijua kuwa Gigy Money anatani kuwa kama Wema Sepetu lakini kwa sasa mambo yamebadilika.

Model huyu wa video za Bongo hivi karibuni alifunguka kudai kuwa Wema Sepetu ni mtu fake na anataka kuwajulisha watu ambao bado hawajapata nafasi ya kumuona live. Akizungumza na Bongo 5 Gigy Money alisema,

“Wema ni mtu ambaye she is fake, Yaah! She is fake. Ukimuona WQema hivi live na ukimuona mtandaoni unaweza ukavurugwa, watu wengi ambao hawajawahi kumuona Wema hivi live wanachanganyikiwa, sio kama mimi sasa hivi. Mimi nilikuwa navurugwa magazeti kila siku nikiensda shule napitia Wema kafanya nini? Sasa hivi naishi hayo maisha sasa huwezi kuniambia Wema she is real. Mimi naishi hayo maisha by real sasa ndio maana kwake inakuwa changamoto, atafanya nini. Mimi ni changamoto kubwa sana kwa kila mtu ambaye yupo kwenye industry hii, maana sasa hivi unaweza ukaenda kwenye interview ukamfanyia msichana anayekuja interview akamtaja Gigy from nowhere pia. Mimi sifanyi kwaajili nashindana, nafanya kwa ajili yangu.”

Aliongeza kwa kusema kwamba walipokutana kwenye birthday ya Sallam, Wema Sepetu alinuna baada ya kumuona akikatika na Diamond Platnumz. Aliendelea kwa kusema

“Last time nimekutana naye hawezi kupiga stori na mimi tena, nimekutana naye kwenye birthday ya Sallam, nilicheza sana lakini nilikuwa ba bae Dangote. Alumina kweli na alikuwa ananiangalia vibaya lakini unajua ni mtu ambaye alishakuwa inspiration kwangu kwa hiyo siwezi kuonyesha action yoyote kwangu na kiukweli am the first person nilimwambia umependeza, wakati anaingia, am real. Ni kweli alivaa kizamani na umbo lake lilivyokubwa mashallah, alipendeza lakini nilivyopingia ndani tena sasa nilivyoitwa na Dangote kisa kuna Wema tena, niacheni kidogo siwezi kuvumilia. Sasa nikawa nacheza mimi na Dangote akawa ananiangalia mimi,”