Huyu ndiye mrembo anayetoka na Gnex_thebaddest Wa Clouds FM?

Kuna fununu kuwa mtangazaji wa CloudsFM Gnex_thebaddest anatoka kimapenzi na mrembo mmoja ambaye ni mwanahabari kutoka Kenya, Kamene Goro.

Hii ni baada ya Gnex_thebaddest kuachia picha kadhaa kupitia mtandao wake Wa Instagram huku akimsifia mchumba wake kwa maneno matatu.

Kamene Goro pia amekuwa akiweka picha za Gnex_thebaddest akiziambatanisha na ujumbe unaodhibitisha kuwa wawili hawa wanauwezekano wa kuwa wapenzi.

Mrembo huyu wa Kenya anafanya kazi na kituo kinachoitwa Ebru Tv na ni mtangazaji wa habari za adhuhuri na anatambulika sana kutokana na umbo lake linalowatia wengi wasiwasi. Tazama picha zake hapa: