Msanii wa muziki wa bongo fleva anaefanya vizuri katika muziki , Harmonize amemjibu msanii tid kuhusu tuhuma alimpa za kuwa amekuwa akiiga kuimba nyimbo za wa Nigeria na kuwa amekuwa akipoteza uhalisa wa nyimbo za Tanzania.
Msanii huyoa aliekuwa akiongea na Wasafi tv, anasema kuwa inawezekana kabisa kuwa T.I.D hakuwa anamlenga yeye kwa sababu kama angekuwa amemlenga yeye basi angemtaja jina na kwa sababu kuongea bila kumtaja jina inaweza kuleta bifu pia hata kwa wasanii wengine tofauti na yeye.
Mimi ninaamini kuwa kuna watu alikuwa akiwalenga lakini sio mimi ila kwa sababu hakutaka matatizo na wasanii wengine akaona bora apitie kwangu na kutaja jina la mdogo wake harmonize.