Z-Anto amtaja mnigeria atakaye shirikiana na yeye hivi karibuni

Z-Anto ambaye ni mmoja wa wasanii ambao walianza muziki zamani ameonyesha uwezo wa kurudisha nyimbo kama za hapo mbeleni baada ya kuachilia nyimbo kadhaa.

Hata hivyo bado hajapata nafasi ya kushirikiana na wasanii wengi lakini kuna uvumi kuwa staa huyu wa Bongo Fleva, huenda akafanya kolabo na pacha wa Kundi la P-Square, Peter Okoye.

Akizungumza na Over Ze Weekend, Z-Anto alianza kuupongeza uongozi wake wa South For Life (SFL) kwa kumsaidia kuachia nyimbo mzuri zinazovuma kwa sasa. Aliendelea kuwashukuru kwa kkumuunganisha na wasanii wakubwa akiwemo Peter Okoye. Z-Anto alisema,

“Ni furaha ya juu niliyonayo. Yote kwa sasa nawaachia South For Life kwani nipo chini yao, endapo mipango itakaa poa basi mtanisikia nikipaa kimataifa,”

Mashabiki wake Wa Afrika mashariki kwa hivi sasa wanaingojea kuiona project yake.