Harmonize Akana Mahusiano Yake na Sarah Mzungu

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutokea kwenye Label kubwa Bongo WCB, Harmonize amejikuta akijikanyaga Baada ya kuulizwa kuhusu Mpenzi Wake na kuishia kukana mahusiano yake na Sarah Mzungu.

Harmonize yupo nchini Nigeria na siku ya jana,  Jumatatu Februari 25, 2019 alitembelea kwenye kituo cha radio cha The Beat 99.9 FM cha jijini Lagos kwa ajili ya Media Tour.

Kwenye mahojiano hayo, Harmonize aliulizwa maswali kadhaa na swali la kwanza lilikuwa ni “Tunamuona mwenzio Diamond yupo na Tanasha vipi wewe upo single?”.

DAHH MIMI? NIPO SINGLE NA NATAFUTA PIA…HAPANA NATANIA SIPENDI KUZUNGUMZIA SANA MAHUSIANO YANGU, UNAJUA MIMI MASHABIKI WANGU NI WANAWAKE NINAVYOJIBU WENGINE WATAJISIKIA VIBAYA”.

Kiukweli ni kwamba Harmonize yupo kwenye mahusiano ya muda mrefu na Mpenzi wake Sarah ambaye pia yupo kwenye moja ya nyimbo zake ambayo ipo kwenye EP yake.

Wolper Afunguka Kuwaingilia Harmonize na Sarah Tena

Mbunifu wa Mavazi na Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper ameibuka na kujibu Tuhuma Za kuingilia tena mahusiano ya aliyekuwa Mpenzi Wake Harmonize na Mpenzi Wake Mpya Sarah.

Sakata hilo lilijitokeza siku chache zilizopita baada ya Wolper alionekana kuuimba katika akaunti yake ya instagram wa mapensi mabaya akimaanisha ‘mapenzi mabaya’ na yeye kubadilisha na kuimba kinyume.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Wolper alisema kuwa amejisikia tu kuimba kinyume kuwa mapensi mazuri.

Lakini watu wanazungumza vingine kwamba namchokoza lakini isivyo hivyo. Nimejisikia tu kuimba haijalishi yeye ndiye ameanza kuimba lakini mimi nikaona niimbe kinyume na yeye alivyoimba ni vile nimejisikia tu kufanya hivyo”.

Baada ya video ile kusambaa watu wengi walichukulia kuwa Wolper amefanya vile ili kumsanifu Sarah hasa kwa sababu wawili hao hawaivi kabisa.

 

Harmonize Afungukia Ujauzito Wa Sarah

Msabii wa muziki wa Bongo fleva Kutoka katika Label ya WCB, Harmonize amefunguka na kutoa majibu kuhusu utata wa ujauzito wa Mpenzi Wake Sarah.

Wiki chache zilizopita Sarah alitupia picha zilizomuonesha ni wa kujifungua muda wowote. Kabla ya kutupia picha hiyo kulikuwa na madai na minong’ono mingi kuwa mchumba huyo wa Harmonize alikuwa haonekani mara kwa mara kwenye mitandao ya kijamii kama ilivyokuwa huko nyuma kwa sababu eti alikuwa analea mimba hiyo hivyo hakutaka kujitokeza hadharani.

Lakini alipohudhuria Birthday party ya Msanii Wolper Wiki iliyopita na kuonekana akiwa hana ujauzito maneno Mengi yalizuka na kushangaza wengi walioamini mzungu huyo ni mjamzito.

Baada ya kuzidi kwa minong’ono Gazeti la Ijumaa, lilimfuata Mpenzi Wake Harmonize ili kupata ukweli wa mambo ambapo alifunguka:

Sidhani kama kila kitu ni vizuri kukiweka kwenye hadhara. Ni jambo kubwa hilo, lakini ni la kifamilia zaidi.

Kama anavyoonekana, hajajifungua na hana mimba kweli. Mara kadhaa Sarah amekuwa akidaiwa kuwa mjamzito, lakini hazina ukweli”.

Jacqueline Wolper Ashabikia Mapenzi Ya Harmonize na Sarah

Muigizaji wa Bongo movie na mbunifu wa mavazi Jacqueline Wolper ameshangaza wengi Baada ya kuonekana akiwa anashabikia Penzi la hasimu Wake Sarah na Harmonize.

Wiki iliyopita kuna tetesi zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Harmonize na Wolper wamerudiana Baada ya kuonekana wakiwa karibu katika tamasha zima la Wasafi Festival.

Lakini Harmonize na mpenzi Wake Sarah walionekana kuzima tetesi hizo Baada ya kuposti video iliyowaonyesha wawili hao wakiwa wanacheza pamoja na kukumbatiana kwenye nyumba yao.

Siku ya jana ilikuwa ni siku ye kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Wolper ambaye alifanya party yake kubwa na kualika wasanii wakubwa lakini cha kushangaza aliwaalika Harmonize na Sarah pia.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Wolper aliposti video ya Harmonize na Wolper na kuisindikiza na maneno haya:

https://www.instagram.com/p/BrDmRCCnUsh/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=ijbkt2241p33

Katika kuonyesha kuwa Harmonize na yeye Hana tatizo na Wolper alimposti katika ukurasa wake wa Instagram na kumtakia Birthday njema.

Harmonize na Sarah Wazima Tetesi Za Kuachana Kwa Staili Hii

Mwanamuziki wa muziki wa Bongo fleva Harmonize na Mpenzi Wake Sarah wamezima tetesi zilizokuwa zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa wameachana.

Harmonize na Sarah wameachia kipande cha Video kinachowaonyesha wakiwa wanacheza wimbo mpya wa Harmonize aliomshirikisha Rayvanny ‘Para nawe’ na kukumbatiana kimahaba na kuonyesha kuwa wapo pamoja.

https://www.instagram.com/p/BrC0I0oHdIu/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1w96soh00gm09

Kipande hicho cha video kimewekwa mtandaoni na Harmonize mwenyewe pamoja na mpenzi wake huyo ikiwa ni siku chache baada ya kuripotiwa kuwa wamemwagana kisha kurudi kwa mpenzi wake wa zamani, Jackline Wolper.

Tetesi za kuvunjika zilianza Baada ya Harmonize kuanza kuonekana pamoja na Harmonize katika tamasha la Wasafi Festival na hata kukumbatiana stejini huku Mpenzi Wake Sarah akiwa nje ya nchi na kupelekea tetesi za kuachana.

Harmonize na Wolper Mapenzi Moto Moto

Msanii wa Bongo fleva nchini kutoka WCB Harmonize na msanii wa Bongo movie Jacqueline Wolper wamezidi kutengeneza headline kwa tetesi za kurudisha Penzi Lao Kama zamani.

Wawili hao wameendelea kuzua gumzo baada ya Harmonize kutangaza kurudi kwa Wolper wake ambaye alimwagana naye miezi kadhaa iliyopita. Ishu nzima ilijiri usiku wa kuamkia juzi Jumamosi katika shoo ya Wasafi Festival iliyofanyika mjini Iringa na kusababisha mji huo kutikisika.

Gazeti la Ijumaa Wikienda linaripoti kuwa Wikiend iliyopita katika Uwanja wa Samora, Harmonize alimpandisha stejini Wolper kama ‘sapraizi’ na kumwangukia akimuomba warudiane, jambo ambalo Wolper alilikubali mbele ya maelfu ya mashabiki wao.

Naomba niseme wazi hapa hadharani kuwa nimerudi kwa Wolper wangu”.

Kufuatia kile kilichojiri mjini Mtwara ambapo Wolper alieleza nia yake ya kumrudisha Harmonize kwenye himaya yake ambapo wengi waliamini kuwa wawili hao wamerudiana maana wahenga walisema kiporo hakihitaji kupashwa na moto mwingi.

Pamoja na kuwepo kwa tetesi za wawili kurudiana Mpenzi wa siku nyingi wa Harmonize, Sarah ambaye kwa sasa yupo nyumbani kwao nchini Italy lakini amesema wazi kuwa yeye na mpenzi wake Harmonize bado wako wote na anategemea kurudi Tanzania muda wowote.

“Sarah Hajakasirika Nilivyokumbatiwa na Wolper”- Harmonize

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutokea katika label ya WCB Harmonize ameibuka na kudai kwamba Mpenzi Wake Sarah hajamind kitendo cha yeye kukumbatiana na Ex Wake Wolper.

Wikiend iliyopita mkoani Mtwara kwenye tamasha la Wasafi Festival Harmonize alirekodiwa akikumbatiana na Ex Wake Wolper wakati wa kusalimiana mara moja tetesi zilianza kusambaa kwamba wawili hao wamerudiana.

Tetesi hizo zilizimwa na Mpenzi wa Harmonize, Sarah ambaye Kupitia ukurasa wake wa Instagram alisema yeye na Harmonize hawajaachana na hawategemei kuachana na muda si mrefu angejiunga naye Mtwara kwa ajili ya shoo hiyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Harmonize alisisitiza yeye na Wolper ni washkaji tu na wapo kikazi ila Mpenzi Wake ni Sarah na hajamind alivyoona video za wawili hao kukumbatiana:

Wolper ni mtu wangu wa karibu na nilifurahi  kumuona akishiriki tena na Wasafi na kuhusu Sarah najua hawezi kumaindi kwani anaelewa kuwa tupo Mtwara kikazi zaidi”.

Harmonize Akana Tetesi Za Kumchumbia Sarah

Staa wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika label matata WCB Harmonize ambaye kwa sasa anafanya vyema kabisa na ngoma yake ya ‘Kwangwaru’ amefunguka na kukataa tetesi zinazodai kuwa amemvisha Pete mpenzi wake Sarah.

Tetesi za Harmonize kumvusha pete ya uchumba mpenzi wake Sarah zilianza kusambaa wiki chache zilizopita baada ya kuposti picha Kwenye mitandao ya kijamii zikiwaonyesha Harmonize akimvisha pete ya thamani Sarah.

Tukio hilo la kuvalishana pete lilionekana kwenye mitandao ya kijamii siku chache baada ya wawili hao kugombana na kurushiana maneno kwenye Instagram baada ya Tetesi za Harmonize kuchepuka.

Kwenye mahojiano aliyofanya alipokuwa nchini Kenya kwa ajili ya shoo yake Harmonize aliwaambia Pulse Live kuwa hajamvalisha pete ya uchumba Sarah kama Tetesi ila wapo mbioni kufanya hivyo:

Sijamvisha Pete mchumba wangu,… na Ndoa bado unajua siku zote ndoa ni mipango na ikifika wakati wa engagement nitawatangazia”.

Mwezi uliopita Harmonize alikumbwa na tetesi za kuchepuka na wasichana kadhaa ikiwemo msanii wa nyimbo za Injili kutoka Kenya na mtangazaji kutoka Nigeria lakini pia Ex wake Jacqueline Wolper.

Harmonize Amtaka Mpenzi Wake Azoee Kusikia Ana Michepuko

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva kutoka WCB anayeendelea kufanya vyema sana  Harmonize amemfungukia mazito mpenzi wake Sarah na kumsisitizia kuwa hana michepuko.

Harmonize ambaye amekuwa Kwenye headlines sana kwa tuhuma za kuchepuka amefunguka na kukataa tuhuma hizo lakini pia amesema Tetesi hizo ni lazima kwa mtu maarufu kama yeye na hata mpenzi wake Sarah lazima azizoee tu:

Harmonize alifunguka hayo nchini Kenya alipokuwa kwenye shoo yake ambapo kwenye mahojiano na Pulselive na kumtaka mzungu wake kuwa mvumilivu:

Sio Kitu Kibaya maanake wivu pia ni Mapenzi, lakini kitu ambacho Sarah inafaa ajue kuwa ukikubali kuwa na Msanii lazima kuna vitu lazima tu ukubaliane navyo tu. Na Life style ya msanii inakaa vipi kuna wengine ni mashabiki na siwezi goma kupiga picha nao maanake bila wao mimi sipo. Kwa hivyo natumai tu anafaa kuelekezwa alafu atajua jinsi ya kuhandle situation kama hizo”.

Sarah na Harmonize waliingia Kwenye mgogoro mkali mapema mwezi huu baada ya Tetesi za Harmonize kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na wanawake kadhaa.

Harmonize Amvisha Pete Ya Uchumba Mpenzi Wake Sarah

Staa wa muziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘Kwangwaru’ Harmonize amemvalisha Pete ya uchumba mpenzi wake mwenye asili ya Italia Sarah Michelotti.

Harmonize na Sarah walikuwa kwenye mgogoro wiki chache zilizopita baada Sarah kumtuhumu mpenzi wake huyo kwa kuchepuka baada ya kuona picha zake na mtangazaji kutoka Nigeria Nancy Isime na kudai ni wapenzi.

Lakini Sarah na Harmonize walionekana kumaliza tofauti zao siku chache zilizopita baada ya kuonekana pamoja Kwenye shoo  ya Kusi Night wakiwa wanakumbatiana stejini.

Hatimaye wawili hao wameweka wazi kuwa wamechumbiana baada ya Kuposti video iliyomuonyesha Harmonize akimvalisha Sarah Pete na Sarah Kuposti Kwenye ukurasa wake wa Instagram na Kuandika “Thank You Baby ♥️“.

 

Harmonize Afunguka Baada Ya Kumwagana na Sarah

Staa wa muziki kutoka WCB Harmonize amefunguka kwa mara ya kwanza tangu sakata litokee wikiendi iliyopita na kusababisha yeye na mpenzi wake Sarah kutofautiana.

Harmonize na Sarah walikamata headlines mwishoni mwa wiki hii baada ya wawili hao kurushiana maneno Kwenye mitandao ya kijamii na hata matusi yaliyopelekea kumwagana baadae.

Harmonize anafunguka kuhusu sakata hilo na kuweka wazi kilichokuwa kinatokea pale ni wivu wa kimapenzi ambao Sarah anao juu yake hasa pale alipomuona akiwa na wadau wa muziki wa kike.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Wasafi Tv, Harmonize anafunguka kuhusu sakata hilo lililotokea kati yake na Mpenzi wake Sarah:

Unapoamua kuwa na mtu unatakiwa ujue huyo mtu ni wa aina gani, anafanya kazi gani, ukishajua hivyo unakuwa ni rahisi zaidi ku-deal naye.

Nakutana na watangazaji, wasanii inatakiwa ni badilishane nao mawazo, sasa ukiwa unaendekeza kila saa masuala ya kimahusiano inakuwa unanirudisha nyuma kwa namna moja au nyingine”.

Harmonize ameweka wazi kuwa sakata  hilo lilianza baada ya Sarah kujaribu kumpigia kwa muda mrefu na yeye kutokana na kuwa bize na kazi alishindwa kupokea simu na hivyo kusababisha kukosa maelewano.

Penzi la Harmonize na Sarah Linapumulia Mashine

Penzi la staa wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize na mpenzi wake mzungu Sarah limedaiwa kuwa linapumulia mashine baada ya kugombana wikiendi iliyoisha.

Kupitia mitandao ya kijamii Harmonize na Sarah walidhihirisha kuwa katika mafarakano baada ya Sarah kumwaga povu Kwenye ukurasa wa Instagram wa Harmonize.

Huku sababu juu ya kugombana Ikiwa ni wivu wa kimapenzi, Sarah alionekana kuona wivu baada ya Harmonize kuposti picha akiwa na mwanadada ambaye ni mtangazaji nchini Nigeria anayejulikana kama Nancy Isime, ambako Harmonize ameenda kikazi.

Basi Sarah akiwa nyumbani wivu ukamshika alipoona picha hiyo alianza kumshushia matusi ya nguoni Harmonize huku akimjulisha yule mdada  kuwa yeye ndiye mwanamke halali wa Harmonize.

Baada ya povu hilo kuendelea basi Sarah akahamia kwa mwanadada aliyekuwa na Harmonize akampa na yeye vya kwake kuonyesha kukabwa na wivu uliopitiliza.

Baada ya sakata hilo Harmonize alitangaza yeye na Sarah wameachana baada ya kuposti kwenye ukurasa wake wa Snapchat kuwa yupo single:

 

 

Harmonize Amlipua Wolper na Kumuanikia Listi Nzima Ya Wapenzi Wake

Msanii wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize ameingia Tena Kwenye bita ya maneno na Ex girlfriend wake staa wa Bongo movie Jacqueline Wolper.

Siku ya jana kuna video ilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii iliyomuonyesha Wolper akimrushia Dongo Sarah ambaye ni mpenzi wa Harmonize kwa kumuita Mlezi wa wana baada ya taarifa kusambaa kuwa kamtosa Harmonize na kumchukua Mwarabu Fighter.

Baada ya kuona video hiyo, Harmonize alitokwa na povu zito kwani kwa Kupitia ukurasa wake wa Instagram alimtetea mpenzi wake Sarah na kusema yeye sio Mlezi wa wana ila Wolper ni Mlezi wa Wana na kuambatanisha na listi kamili ya wanaume wote aliokuwa nao Kwenye Mahusiano.

Hii sio mara ya kwanza kwa Harmonize na Wolper kuwa na sintofahamu na hata Wolper na mpenzi wa Harmonize Sarah.

Wolper Amtupia Dongo Zito Sarah Wa Harmonize na Kudai ni Mlezi Wa Vijana

Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper amemtupia Dongo zito Sarah baada ya habari zake za kumtosa Harmonize na kumchukua Bodyguard wa Diamond, Mwarabu Fighter.

Siku mbili zilizopita stori iliyotrend kupita zote ni ya mpenzi wa Harmonize Sarah kumtosa mpenzi wake na kumchukua Mwarabu Fighter.

Inasemekana Sarah amefufa ameoza kwa Mwarabu kiasi ya kwamba anamuhudumia ipasavyo yaani kampangishia hadi nyumba yaani zile huduma zozote alizokuwa anapata Harmonize zimehamia kwa Mwarabu.

Kama utakumbuka Kuwa Sarah na Wolper ni maadui wakubwa na kisa kikiwa ni penzi la Harmonize na juzi tu wametoka kumgombania Harmonize.

Baada ya tetesi hizo za usaliti kusambaa mitandaoni Sam Misago Tv walimsaka Wolper na kumuuliza nini maoni yake juu ya ishu hii kumuhusu Sarah na Wolper ameishia kumtupia dongo zito Sarah:

Duh iyo ishu mbona ni exclusive kabisa sijaisikia lakini freshi tu mbona yule demu ni Mlezi wa wana labda kachoka kumlea mwana kaamua kumchukua mwana mwingine freshi tu”.

Bifu laWolper na Sarah lilianza baada ya Sarah kuanza kuchepuka na Harmonize wakati Wolper yupo Kwenye Mahusiano na Harmonize.

 

Sarah Wa Harmonize Adaiwa Kufa na Kuoza Kwa Penzi la Bodyguard Wa Diamond

Mpenzi wa msanii wa Bongo fleva kutoka Label ya WCB Harmonize, Sarah maarufu kama Sarah Mzungu amejikuta ndani ya skendo nzito baada ya kudaiwa kuhamisha penzi lake kutoka kwa Harmonize kwenda kwa Bodyguard wa Diamond.

Habari kutoka Kwenye mitandao ya kijamii zinadai kuwa hivi sasa Sarah amehamisha penzi kwa Bodyguard wa Diamond anayeitwa Mwarabu fighter na kudaiwa kumsahau mpenzi wake Sarah.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mange Kimambi amepasua jipu hilo na kudai harmonize anamlilia Sarah asimtose kwani keshahamisha majeshi kabisa kwa Mwarabu fighter:

Basi mnaambiwa Sarah wa Harmonize yuko deep in love na Mwarabu yaani sahivi Harmonize ndio analia mzungu asimkimbie ila bibie mnaambiwa anampenda Mwarabu Fighter. Siku hizi mnaambiwa Mwarabu gym anafanya, Collesium bibie analipia, ana maisha mazuri mzungu anampa hela balaa Mnaambiwa mapenzi moto moto”.

Baada ya tetesi hizo kuingia kwenye mitandao ya kijamii mara moja Sarah alianza kuposti kukana tetesi hizo Lakini mara moja Mange alidai kuwa anayeposti vile sio Sarah bali ni harmonize ambaye ana password ya akaunti ya Sarah.

Harmonize aliposti picha ya Mwarabu Fighter na kuandika maneno haya kuashiria Stori hiyo haina ukweli:

 

 

Harmonize- Nipo Tayari Kumuoa Sarah

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize amefunguka na kuweka wazi mipango yake ya kumuoa mpenzi wake Sarah.

Kwa muda mrefu kumekuwa na maneno mengi kuhusu Mahusiano ya Harmonize na Sarah huku wengi wakidai Harmonize hana mapenzi ya kweli kwa Sarah bali yuko naye kwa ajili ya pesa.

Huku dhana hiyo ikiwa imepandikizwa na Ex wa Harmonize, Jacqueline Wolper ambaye alisema Harmonize alianzisha Mahusiano na Sarah wakati wako pamoja kwa sababu alikuwa anamuwezesha kifedha.

Lakini Harmonize ameibuka na kuweka wazi kuwa anampenda Sarah na hivi sasa yuko tayari kumuoa mwanamke wake huku akipuuzia maneno yote ambayo yanasemwa na watu.

Kwenye mahojiano na The Playlist ya Times Fm, Harmonize aliweka wazi mipango yake ya ndoa baada ya kuulizwa na Lil Ommy kama ana mpango wa kumuoa Sarah:

Ndiyo nataka nimuoe Inshallah”.

Harmonize anafanya vizuri na nyimbo zake mbili ambazo ni Kwa ngwaru aliyomshirikisha Diamond Platnumz na wimbo wake mpya Dm Chick ambao amemshirikisha Sarkodie.