Diamond na Harmonize Wapania Kuondoa Muziki Wa Nigeria Bongo

Staa wa muziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Diamond Platnumz na Harmonize wamekuja na mkakati wa kuua kabisa muziki wa Nigeria ambao umeshika sana kasi nchini Tanzania.

Harmonize amefunguka na kudai wimbo wake mpya wa Kwa ngwaru ni mwanzo mzuri wa kurudisha muziki wa kuchezeka Tanzania ambao kwa kipindi kirefu ulishikiliwa na muziki wa Bongo fleva.

Harmonize amefunguka Kwenye Interview aliyofanya na Radio Five na kudai kuwa nyimbo za kuchezeka Bongo zimepungua kwani ambazo zinazotoka sasa hivi zimepoa kitu ambacho kinafanya nyimbo za wasanii wa Nigeria kupewa nafasi hasa club.

Inafikia wakati tunaona ni lazima tucheze, so tukaona this time around tukija na Kwa Ngwaru kama ngoma nyingi zilitoka kama zimelala ndio maana ukienda club unasikia Wanigeria wakati sisi tunaweza tukafanya muziki mzuri watu wakapenda na wakacheza.

Mwisho wa siku tunapenda tu ngoma zao kwa sababu ya beat lakini lugha hatuijui”.

Harmonize alitoa wimbo huo wa Kwa ngwaru wiki iliyopita na ulitrend kwa wiki nzima Youtube, huu ni wimbo wa pili kwa Harmonize kumshirikisha Diamond ambapo wimbo wa kwanza ilikuwa ni Bado ambao ulifanya vizuri sana.

Harmonize Awaomba Radhi Mashabiki Wake.

Msanii wa muziki kutoka lebel kubwa  ya wasafi  Harmonize ,kwa takribani siku kadhaa nyuma amekuwa akiweka picha  za kuwataka mashabiki wake wakae mkao wa kula kwa kibao chake kipya kilichotakiwa kachiwa hewani siku ya tarehe 01 March mwaka huu,

Lakini kutokana na sababu ambazo Harmonize mwenyewe ameshindwa kuzisema , ameshindwa kutoa wimbo hu uliojulikana kama kwangaru ambao amemshirikisha boss wake Diamond Platinumz.

Akiandika katika ukurasa wake wa instagram ,Harmonize amewaomba msamaha mashabiki wake kwa kuwasubirisha kwa muda mrefu na badoa meshindwa kutimiza ahadi yake ya kuachia wimbo huo.

Hata hivyo sio mashabiki wote wa msanii huyo wameweza kumuelewa msanii huyo huku wengine wakimtolea maneno  makali na kumwambia kuwa alikuwa akitengeneza kiki tu ili kuvuta attention ya watu.Mpaka Harmonize anaomba msamaha hajasema kuwa ni lini tena anatarajia kuutoa tena wimbo huo.

 

Harmonize Afungukia Ishu Ya Kuondoka Katika Lebo Ya Wasafi

Mwanamuziki wa bongo fleva anayefanya vizuri na nyimbo sake mbili hivi sasa ‘shulala’ na ‘nshachoka’ kutoka katika lebo ya Wasafi classic amefunguka kuhusu ishi ya yeye kuihama lebo hiyo.

Harmonize aliamua kulizungumzia jambo hilo baada ya kudai kuwa watu wengi hasa mashabiki zake wamekuwa wakimuuliza mara kwa mara kama ipo siku ana mpango wa kuhama lebo hiyo ambayo ndio chanzo cha mafanikio yake kwani ndiyo iliyomtambulisha kwenye muziki miaka michache iliyopita ijapokuwa safari yake ya muziki ilianzia mbali kwani ni miaka michache tu Harmonize alikataliwa kwenye shindano la kutafuta vipaji la Bongo star search.

Kwenye mahojiano na Times FM kwenye kipindi cha The playlist Harmonize alifunguka:

Kuhusu suala la mimi kuhama WCB naomba niseme hapana kwa kweli kwani unapokuwa unamzungumzia Harmonize unakuwa unaizungumzia Wasafi classic baby na unapoizungumzia WCB unamzungumzia Harmonize pia yaani hiyo kama baba kama mama na pia isitoshe naikubali familia nzima ya WCB kwani kila mmoja wetu ana kipaji hakuna aliyekuja pale kwa Bahati mbaya yaani kikubwa wote tunatofautiana”.

Ni vizuri kwa wasanii kuwa na uangalizi yaani management kwani sahuvi muziki umekuwa biashara kama biashara nyingine kwaiyo msanii yoyote anahitaji timu nyuma yake ili kufanikisha malengo take binafsi.

Harmonize- Namuheshimu Wolper Ameona Utupu Wangu

Mwanamuziki kutoka WCB, Harmonize anayetamba na nyimbo zake mbili zinazofanya vizuri ‘shulala’ na ‘nishachoka’ amefunguka na kusema anamuheshimu sana Wolper kwa sababu ameona utupu wake.

Siku za hivi karibuni kumekuwa na attention kubwa sana iliyoelekezwa kwa Harmonize na mpenzi wake wa zamani wake Jacqueline na mpenzi wake wa sasa Sarah. Sakata hilo lilianza tangu Wolper alipoachana na Harmonize na kuweka wazi kuwa Harmonize yupo na Sarah kwa sababu ya pesa. Siku chache zilizopita baada ya Harmonize kutoa ngoma yake ya Shulala wanawake hao waliingia kwenye ugomvi mkubwa mpaka kusemekana kuwa Harmonize amerudiana na Wolper kitu ambacho Harmonize alichokataa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Lil’ommy  Harmonize alikataa kuwa wimbo wake wa ‘nishachoka’ amemuimbia Wolper:

Unajua msanii mzuri ni yule anayeimba nyimbo zinazogusa maisha ya watu na mapenzi ni kitu kinachogusa watu wengi kwaiyo ule wimbo mi nimeimba ili niwafurahishe mashabiki wangu lakini sio kweli kwamba nimemuimbia Wolper, kuhusu kumtumia model anayefanana na Wolper halikuwa wazo langu mi nimeimba nyimbo director ndo akachagua model wa kuwepo kwenye video kwaiyo mi sijui lolote itakuwa vizuri umuulize director”.

Harmonize aliendelea zaidi kufunguka kuhusu Wolper na mchango wake;

Kikubwa naomba nimshukuru Wolper kwa kuiposti ngoma yangu na kuisapoti kwani ametumia muda wake, bando lake, image yake kaweka kwenye kazi yako  kwa kweli sio kitu rahisi, mi namheshimu sana na namshukuru sana naomba mwenyezi Mungu amjaalie na ukizingatia vitu vyote vilivyokuwa vinatokea kwenye mitandao ya kijamii yeye ndo alikuwa anazungumza kwenye media kwa sababu mimi sio mtu muongeaji sana alafu mi huwa namheshimu sana mwanamke ambaye ameona utupu wangu siwezi nikakaa nikamzungumzia vitu alivyokuwa anafanya”.

Baada ya kuwepo kwa tetesi kuwa Harmonize amemuimbia Wolper ule wimbo, baadaye  akatoa video ya wimbo wake wa Nishachoka na kuonekana wazi kabisa model aliyetumika anafanana na Wolper.

Harmonize Amefunguka Kuhusu Bifu Lake na Idris Sultan

Msanii kutoka label ya WCB, anayefanya vizuri hivi sasa na ngoma yake ya ‘shulala’ Harmonize amefunguka na kudai hana bifu lolote na mchekeshaji Idris Sultan.

Habari za wawili hawa kuwa na bifu zilienea miezi michache iliyopita mara baada ya Idris kuandika mtandaoni kuwa Harmorapa alikuwa anafanya vizuri kuliko Harmonize na hivyo ni bora Harmonize astaafu kufanya mziki maneno hayo yalimkera sana Harmonize ambaye alimuita Idris shoga mtandaoni. Tangu siku ile inadaiwa wawili hawa hawaivi kabisa katika chungu kimoja.

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na Times Fm Harmonize amedai kuwa hana bifu lolote na Idris na anashangazwa maneno hayo yametoka wapi.

Sina bifu na Idris na sijawahi kuonana naye, I am telling you ni stories tu naona watu wanatengeneza kila siku alafu kingine mi ni mtu wa kusamehe sana haya mti akiwa amenikosea kabisa  naamini ni binadamu tu kwani hata might naamini huwa kuna watu nawakoseaga”.

Harmonize ambaye anazidi kufanya vizuri na wimbo wake wa shulala umekuwa ukishika namba moja katika stesheni mbalimbali za redio na hata kwenye mtandao wa video YouTube bado unaongoza.

Kajala, Wolper na Harmonize Waingia Katika Bifu Zito

Mastaa wawili wa Bongo movies Kajala Masanja na Jacqueline Wolper wameingia katika bifu zito baada ya maongezi kwa njia ya video ‘video call’ baina ya Kajala na mpenzi wa zamani wa Wolper mwanamuziki Harmonize kuvuja mtandaoni na kuibua makubwa.

Kajala alikuwa akizungumza kwa njia hiyo ya kisasa na Harmonize ambae alionekana akila tunda aina ya apple kitandani kwake huku na Kajala akiwa kitandani kwake, baadaye Harmonize aliirusha picha hiyo mtandaoni na kusababisha minong’ono ya chini chini kusambaa. Picha ile ilimkera Wolper ambaye ametoka kuachana na Harmonize miezi si mingi na Kajala pia ni rafiki yake hivyo ilipelekea Wolper kuandika maneno yafuatayo kwenye picha ile: “Yaani nimekaa hapa mwenyewe nimewaza mapenzi ya siku hizi yana drama mno, mara leo huyu mara kesho yule”. Akijua wazi Kajala ameumizwa na kitendo hicho. 

Wema Sepetu naye aliingilia kati ishu hiyo na kuandika maneno chini ya picha hiyo “Be carefully my baby huyo nyakunyaku asije akapita maana keshaambiwa mlango uko wazi”. Maneno hayo yalionekana kumuuma Kajala ambaye mara moja alikimbilia mabatini kituo cha polisi kwenda kumshtaki Harmonize kwa kitendo chake cha kuweka picha hiyo mtandaoni na kuleta tafsiri kuwa huenda wawili hao ni wapenzi kitu ambacho sio cha kweli, na yeye amepewa RB No/ KJN/ 73/2017 Jalada la uchunguzi

Kajala amesema;

“Nimemshtaki Harmonize ili ajue mimi sio mtu wa mchezo  kila wakati, maana ile video tulikuwa tukizungumza kawaida kwa nini aisambaze ili iweje kama sio kuchafuana huko”.

Kajala aliongeza kuwa anawashangaa wasanii wenzake Wolper na Wema kuingilia vitu kama hivyo kwa sababu wanaona kama yeye ni wakula mizoga yao. “Mimi nashangaa hivi wamenionaje, wanafikiri mimi ni wakula  mizoga yao nini wanayoiacha, wamenishangaza sana”.

Harmonize aliwasili kituoni hapo na kwa mujibu wa chanzo kinachoaminika kutoka kituoni hapo, Mwanamuziki huyo alijitetea kuwa sio yeye aliyeweka picha hizo mtandaoni bali ni mwanamke wake wa kizungu ndo aliyemtumia mtu mwingine kwa nia ya kutaka kumjua Kajala.

Harmorapa Amponda Mpenzi Mpya Wa Harmonize Adai ni Bibi

Msanii anayechipukia kwa kasi nchini kwenye miondoko ya hip hop Harmorapa amefunguka mengi juu ya Mpenzi wa wanamuziki mwenzie Harmonize, Anayejulikana kama Sarah pamoja na mpenzi wa zamani wa msanii Diamond “Wema Sepetu” akidai kuwa wote ni mabibi yaani watu wenye umri mkubwa.

Akizungumza kuhusu mpenzi huyo wa Harmonize, alifunguka kwamba:

“Mimi namuona yule mpenzi wa Harmonize ni bibi tu, hajaopoa demu pale bali kaopoa mpenzi ambae ni bibi yaani ni kama mimi nikaishi na bibi angu, yaani ndo Harmonize ni kama  anaishi na bibi mzaa mama yake”.

Harmorapa pia alishawahi kufunguka mengi kuhusu  kumpenda Wema aliposema yupo tayari kumliia fedha yoyote kwa ajili ya kuishi naye lakini Wema alikataa kupitia ukurasa wake wa instagram baada ya kuona hivyo harmorapa alimgeuka na kumponda na kusema ana umri mkubwa. Harmorapa alimshauri mwanamuziki huyo machachari aachane na Sarah na atafute mwanamke anayeendana na umri wake.

Madame Ritha Afunguka kuhusu Harmonize

Ritha Paulsen au maarufu kama “Madam Ritha” amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu Mwanamuziki Harmonize ambaye aliwahi kuwa mshiriki katika shindano la kusaka vipaji la Bongo Star Search.

Madame Ritha ambaye alikuwa mwanzilishi wa shindano hilo la Bongo star search na chief judge ambalo lilikuwa limejikita katika kutafuta vipaji vipya vya waimbaji wapya. Harmonize ambaye kwa sasa ni mmoja kati ya wasanii wanaofanya vizuri kwenye bongo fleva chini ya lebo yake ya Wasafi CB. Kabla ya kupata nafasi ya kuwa msanii chini ya lebo hiyo, Harmonize alienda kujaribu nafasi yake katika mashindano hayo ambayo hakufanikiwa kufika mbali kwa kile alichokidai Madam Ritha kuwa hakuimba vizuri.

Madame Ritha amemsifia Harmonize kwa mafanikio yake na kukiri kuwa yeye ni mmoja kati ya watu waliompa changamoto ya kufanya vizuri kwani kwa kipindi kile alikuwa hafanyi vizuri kama sasa Madam Ritha amesema  yafuatayo:

“Alikuja Harmonize kwenye Bongo Star Search na kama tusingemnyoosha wakati ule, May be asingekuwa bora leo na kwenye label kubwa ya muziki hapa nchini. Harmonize alikuwa anaimba “MARAIKA”, hata ingekuwa wewe usingempokea awe msanii wako na ujivunie”.

Harmonize aliwahi kuwafariji watu kuwa wasikate tamaa wakikosea mara moja kwenye maisha kwani yeye angekata tamaa alipokosolewa kwenye BSS basi asingefika pale alipo leo, kwa sasa Hamonize anatamba na nyimbo zake zinazofanya vyema redioni kama “Nimechoka”, “Bado” na vinginevyo vingi.

Wolper na Harmonize ndani ya Bifu Zito

Mwigizaji wa Bongo movies Jackline Wolper na mpenzi wake wa zamani mwanamuziki kutoka WCB, Harmonize wamejikuta katika bifu zito baada ya kuingia katika vita ya kurushiana maneno mtandaoni.  Wolper na Harmonize waliachana miezi michache iliyopta kwa kile alichokidai Wolper kuwa Harmonize alimsaliti na kutembea na msichana mwingine anayejulikana kwa jina la Sarah, katika mahojiano aliyoyafanya Wolper hivi karibuni alielezea machungu aliyoyapata baada ya kugundua kuwa Harmonize anatembea na msichana huyo mwingine kwa ajili ya tamaa ya pesa.

Baada ya kukaa kimya bila kutoa maelezo yoyote siku ya leo Harmonize ameachia wimbo wake mpya unaojulikana kama “Nimechoka” wimbo aliomuimbia mpenzi wake wa zamani Wolper wimbo ambao alituma kwenye ukurasa wake wa instagram na ujumbe usomao:

“Naomba nikupe jukumu la kumtumia #EX wako ambae kila kukicha anakuzumgumzia tena kwa ubaya na kutengenezea mazingira ya chuki katika jamii na umwambie nimechoka”, “Tena mwambie asijekuwa anajidanganya eti unamuwaza…!!! Ni kwasababu umeumbwa na stara hunaga uropo ropo wa kuongea vya ndani pia unaweza kung’oa mkali zaidi yake”.

Wolper naye kwa kupitia ukurasa wake pia alimjia juu Harmonize na kumrushia maneno:

“…Tusilazimishane kuongea nimeshaachana na wewe kiusalama ongelea vilivyopo kwako saivi sio mimi, Nilishatokaga huko kirahisi unaweza ukadeal na style yako ya mziki bila kunihusisha maana unampa hofu pia BFF anahisi labda kuna kitu kumbe hakuna, usiniharibie mahusiano yangu mapya , BFF wangu ni bora kuliko wewe ni adimu na sitaki kumpoteza kwa ajili ya watu kama wewe…Mimi ni Jackie Wolper ambae siwezi kuacha kuongea ukinianza namaliza kwa wale wanaosema bora kunyamaza subirini yawakute alafu mjipe huo ushauri”.

Harmonize na Wolper tangu wameachana kila mtu ameendeelea na maisha yake kwani Wolper ana mpenzi mpya anayejulikana kama Brown na Harmonize yupo na mpenzi wake mpya Sarah lakini tangu wameachana wawili  hao wamekuwa wakirushiana vijembe vya hapa na pale huku kila mtu akimtuhumu mwezie kwa kutokuwa mwaminifu kwenye mapenzi yao.

Harmonize amtetea Zari vikali

Harmonize amemtetea Zari dhidi ya madai kuwa anaponda raha siku chache tu baada ya kumpoteza mama mzazi. Zari, Diamond na Harmonize walionekana Mombasa, Kenya wakijivinjari jambo ambalo halikuwapendeza baadhi ya watu.

Harmonize ata hivyo alimtetea Zari kwa kusema kuwa mtu akipata msiba alafu akapelekwa sehemu nzuri kwa ajili ya kufurahi ni kitu cha kumshukuru mwenyenzi Mungu. Alisisitiza kuwa maisha lazima yaendelee ata mtu akipoteza wapenzi wake.

Harmonize na Zari

“Kwa sababu haikuwa rahisi, unajua kufiwa na mazazi sio kitu kidogo. Tumefika (Mombasa) tumemkuta yupo fresh, yaani kasharidhika na matokeo kwa sababu anajua hakuna binadamu atakuja kuishi milele. Kwanza ukiona mtu anazungumza hiyo ujue haijui dini, kwa sababu dini imeandika kila mtu atakufa, kifo ni kitu cha lazima, ukiwa unaijua dini huwezi kuhofia suala la kifo. Mtu kafariki ni lazima uumie ila ni lazima maisha mengine yaendelee kwa sababu hata ukae ndani miaka sita hawezi kurudi,” Harmonize ameiambia kipindi cha XXL ya Clouds FM.

 

Mr. Nice awashangaza watu kwa kutokea kwenye video mpya ya Harmonize

Msanii Lucas Mkenda maarufu kama Mr. Nice anatrend kwenye mitandao ya kijamii kwa ajili ya kuonekana kwake kwenye video mpya ya Harmonize.

Staa huyo aliyevuma zamani alihamia Kenya kwani hakua anapata kiki Tanzania. Hata hivyo kutokea kwa Mr. Nice kwenye wimbo mpya wa Harmonize – ‘Sifa’ kumedhibitisha kuwa nyota huyo wa zamani bado anafanya kazi na wasanii wa Tanzania.

Wimbo huo wa Harmonize unaangazia maisha ya Mr. Nice alipopata pesa na kuwa mtu maarufu na maisha yake alipofilisika.

Tazama video hio hapo chini:

Wolper: Sina wivu na Harmonize

Jacqueline Wolper hana machungu yoyote na mpenzi wake wa zamani – Harmonize. Mwigizaji huyo wa filamu za Bongo alisema kuwa aliachana na Harmonize miezi sita iliyopita. Alieza pia vitu vinavyo mvutia kwa mpenzi wake mpya – Brown.

“Tumeachana kama miezi sita hivi tulikuwa hatuelewani. Huyu BFF yaani Best Friend Forever tuna kama wiki hivi. Tulikutana vizuri tu alianza kuniona kama miaka minne hivi before. Kinachonivutia kwake ni mpole na mkweli, kwa hiyo ni rafiki yangu mzuri sana,” Wolper alisema kupitia kipindi cha The Weekend Chart Show ya Clouds TV.

Jacqueline Wolper na Brown

Wolper hata hivyo alisisitiza kuwa yeye na Brown ni marafiki tu wala sio wapenzi;

“Mimi siwezi kuingia kwenye vita na siwezi kuwa na uchungu japo stress hazifichiki na furaha haifichiki. Kwa hiyo nyie mnaweza mkajadili. Vitu vya instagram siyo vya kweli vyote japo wanakuwa na vitu vyao vina ukweli kidogo. Huyu kaachana na mtu wake miezi miwili halafu mwezi wa tatu tukakutana. Kwa hiyo, hizo ni story tu wote tumekutana single ila tofautisha wale ni wapenzi na sisi ni BFF na tupo serious. Ni marafiki wa kweli. Mimi siyo mtu wa TV naye siyo mtu wa TV.”

 

Diamond: Ilibidi nipunguze kasi nyimbo zangu zisiwaue kina Harmonize, Rayvanny

Diamond ameeza kwanini alikosa kupata uteuzi wa tuzo la BET mwaka huu. Hit maker huyo wa ‘Marry You’ amewahi kuteuliwa mara mbili (2014 na 2016) kuwania tuzo hilo kwa kitengo cha Best International Act: Africa.

Akiongea katika kipindi cha XXL ya Clouds FM jana, Diamond alieleza kuwa alipunguza kasi yake kimuziki mwisho wa mwaka jana ili akuze kina Rayvanny, Harmonize na wasanii wengine.

Alieza kuwa msanii kupata uteuzi wa BET ni lazima aachilie nyimbo mfululizo na yeye aliwacha kutoa ngoma nyingi kwani kama angefanya hivyo nyimbo zake zingewaua kina Harmonize, Rayvanny na wengine.

“Mwakani lazima niingie, unajua kuna kitu kimoja…lazima uishi kwa plani na malengo…Na ukiangalia mwaka juzi mwishowe mbaka mwaka jana ulikua ni mwaka kuhakikisha nawashika vijana wa Kitanzania nao wasikike katika muziki. Na ili wasikike ilibidi mimi nipunguze kasi yangu kwasababu mimi naachilianga tu mawe, ilibidi nipunguze mawe niwashindirie tu hao mawe kina Harmonize, sijui kina nani Ray… wote…kwasababu nikiingia itakua ni mtafaruko. Ukiangalia mitaa ingine nimeanzisha lebo kuna nyimbo kama tatu, nyimbo zangu zingine ni mishirikisho tu. Ilibidi nipunguze kwasababu mimi najua nikiweka nyimbo na hawajakua na nguvu nyimbo zangu zitawaua. Na zile nomination zinataka mtu aachilie ngoma mfululu,” Diamond alisema.

Tazama mahojiano hayo hapo chini:

https://www.youtube.com/watch?v=K_fRN6xFS8o

Huyu ndiye mrembo mpya anayetoka kimapenzi na Harmonize

Wikendi hii Harmonize kwa mara ya kwanza aliweka picha ya mpenzi wake mpya baada ya wengi kumchana kwa kumwaga Wolper.

Kama ilivyokuwa ikitangaza kwenye mitandaoni, Harmonize anatoka na mrembo wa kizungu na kama hiyo haijatosha wawili hao wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

mambo haya mawili yamewaacha mashabiki kama wameduwaa kwa sababu mimba hiyo inaonekana kuwa ina miezi 6.

Hata hivyo, Wolper naye ameonekana aliendelea na maisha yake bila kujali kile mpenzi wake anafanya. Tazama picha hizo hapa;

Harmonize ampachika mimba mpenzi wake wa kizungu (Picha)

Harmonize sasa anatarajia kuwa mzazi wakati wowote, staa huyo wa Wasafi amempachika mimba mpenzi wake wa kizuri miezi michache baada ya mapenzi yake na Jacqueline Wolper kuvunjika.

Akiongea kwenye kipindi cha Shilawadu cha Clouds TV, Wolper alisema kuwa uhusiano wake wa kimapenzi na Harmonize uliisha miezi mitatu iliyopita.

“Nyie mnajua sisi tumeachana juzi? Tumeacha miezi mitatu iliyopita kabla hata ya wimbo wake Niambie haujatoka. Sisi wenyewe tuliamua kukaa kimya kwa sababu kuachana sio kugombana kuna kesho mnaweza kushirikiana katika mambo mengine ya kibiashara,” Wolper alisema.

Wolper na Harmonize

Harmonize aliharakisha kuingia katika uhusiano nyingine baada ya kukosana na Wolper, kwa sasa mpenzi wake ni mzungu.

Hit maker huyo wa ‘Happy Birthday’ alitangaza kwa Instagram kuwa anatarajia mtoto wake wa kwanza na mpenzi wake wa kizungu.

Mrembo wa kizungu wa Harmonize

“Mnh! nawaza huu mchanganyiko wa damu ya kimakonde na ya kizungu sijui itatuletea mwana gani… asa nikiona kakomwe hapo, kananistua?…Chonde mtoto chukua vyote kwangu ila kwenye rangi jitahidi uibe ya mama yako…..!!! nikavimbe Mtwara ?,” Harmonize aliandika kwa Instagram na kuweka picha ya mtoto wake akiwa tumboni mwa mpenzi wake.

Maoni ya Dogo Janja kuhusu uhusiano wa Jacqueline Wolper na Harmonize

Dogo Janja ametoa maoni yake kuhusu uhusiano wa Jacqueline Wolper na Harmonize kufuati matukio ya hivi karubuni.

Kuliibuka uvumi kuwa wawili hao (Harmonize na Wolper) waliachana lakini baadae Harmonize alikuja kuthibitisha ukweli wa mambo.

Dogo Janja alikuwa na mengi ya kusema kuhusu uhusiano wa Wolper na Harmonize; akiongea katika kipindi cha XXL cha Clouds Fm, msanii huyo wa Tip Top Connection inayomilikiwa na Babu Tale, alisema kuwa maisha ya watu mashuuri ni filamu.

Jacqueline Wolper na Harmonize

Dogo alisema kuwa mapenzi ya Harmonize na Wolper ulikuwa kama drama ulipokua unaanza lakini mwishowe ukawa ‘serious’.

“Ukishakuwa na mpenzi staa hiyo ni flamu tayari, maisha yenu ni filamu watu wanafuatilia. Kingine mapenzi yao yalivyokuwa yananza watu walikuwa wanachukulia kama Drama lakini mwisho wa siku unakuja kuona kama wapo serious, kwa hiyo ni vitu kama hivyo.

“Mimi kama mimi siko interested nao sana, ni verse tu zile, siko interest nao kwa vile na mimi nina mapenzi yangu , kila mtu ana mitikasi yake” amesema Dogo Janja.

Dogo Janja