Hawa Asimulia Alivyonusurika Kifo

Afya ya Hawa kwa sasa imeimarika na kurudi katika hali yake ya kawaida baada ya kuchungulia kaburi, jambo ambalo hata yeye mwenyewe hakulitegemea kwani alishakata tamaa ya kuishi. Mwishoni mwa mwaka jana, Hawa alipelekwa kwenye matibabu nchini India kutokana na tatizo lake la tumbo kujaa maji.

Jitihada hizo za matibabu ya Hawa zilifanywa na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ aliyeshirikiana naye kwenye Wimbo wa Nitarejea. Baada ya kurejea Bongo, Hawa aliwekwa mafichoni kwenye hoteli moja jijini Dar kutokana na maelekezo kutoka kwa madaktari ambao walitaka iwe hivyo kwa miezi mitatu.

Baada ya miezi hiyo mitatu, Hawa alirejea nyumbani kwao, Buguruni-Rozana jijini Dar kuendelea na maisha yake kama kawaida. Risasi Mchanganyiko lilimuibukia nyumbani hapo ili kufanya naye mahojiano kuhusu hali yake kwa sasa na mambo aliyoyapitia.

“Kwa kweli ninamshukuru sana Mungu maana bila yeye, huenda nisingekuwepo, leo hii naweka tabasamu usoni, lakini niliteseka mimi jamani. Hadi ninasafiri kwenda India nilikuwa na maumivu makali hadi nilihisi kama nataka kuchanganyikiwa, yaani hadi kumsimulia mtu nahisi kama nitampunja kwa sababu hayaelezeki, yalikuwa makali sana. 

Hawa kutoka ‘Nitarejea’ alioshirikishwa na Diamond adaiwa kupotelea kwenye vileo!

Nitarejea ni wimbo ambao bado unafanya vizuri Hata baada ya kuachiwa mwaka Wa 2013. Diamond Platnumz alimshirikisha muimbaji anayejulikana kama Hawa na kutokana na sauti yake nzuri, mrembo huyu alitarajiwa kwenda mbali lakini hivyo sivyo mambo yalienda.

Hawa anasemekana kuwa alipata mtoto wake Wa kwanza anayedaiwa kuwa mtoto wa Diamond Platnumz na baadaye akafunga ndoa na mwanaume mwingine ambaye amemsababisha kuingilia vileo kutokana na ‘stress.’

Sasa hivi mrembo huyo amekiri kuwa maisha yake ilipotelea kwenye unywaji wa pombe kali aina ya gongo, kiasi cha kumfanya apoteze mwelekeo maishani mwake.

Akizungumza na Global TV Hawa alisema kuwa alijipata kwenye maisha haya baada ya mumewe kuondoka na kumuacha bila mawasiliano yoyote kwa muda wa miaka miwili baada ya kukaa kwenye ndoa yao kwa muda mfupi.

Kutoka na kufikiria sana, Hawa alitafuta namna ya kutoa ‘stress’ na akaingia kwenye vileo ambavyo vimemdhoofisha kimwili. Amedai kuwa amekonda huku akiomba msaada kutoka kwa mashabiki na wadau kumsaidia kuepuka maisha haya ambayo yanampeleka vibaya.