Husna na Tunda Ndani Ya Sakata La Kuibiana Mwanaume

Mlimbwende aliyewahi kushiriki shindano la Miss Tanzania miaka ya nyuma Husna Maulid na video vixen maarufu Bongo Tinda Sebastian wamedaiwa kutibuana kisa bwana wanayemgombania.

Gazeti la ijumaa wikienda linaripoti kuwa Husna ambaye alikuwa na urafiki na Tunda alijikuta amesalitiwa na shoga yake huyo baaada ya kugundua kuwa amemchukulia bwana ake anayeitwa Ally.

Katika mahojiano aliyofanya na Gazeti hili, Tunda alisema watu wamekuwa wakizungumza sana kuhusiana na hilo kwamba ameibiwa bwana na rafiki yake Tunda kitu ambacho hakifahamu kwani anachojua yeye ni kwamba ana mpenzi wake mmoja tu anayejulikana kwa jina la G na ndiye rafiki yake pia.

Jamani naomba watu waelewe kwamba nina mpenzi wangu anaitwa G, huyo mwingine anayetajwa simjui na wala sina urafiki na mtu zaidi ya mpenzi wangu, huyo ndiye rafiki yangu wa karibu“.

 

Husna Ajaribu Bahati Yake Kwa Diamond

Mrembo ambaye aliwahi kufanya vyema Kwenye Mashindano ya Miss Tanzania 2011/2012 Husna Maulid ameibuka na kudai kuwa na yeye ni mmoja kati ya warembo wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Sakata hilo la Husna lilitokea siku chache zilizopita baada ya kuweka picha yake Instagram na kusindikiza na maneno ‘Roho Ya Simba’ na kuonyesha yupo Madale nyumbani kwa Diamond jambo lililosababisha mashabiki kumjia juu.

Mashabiki walimshambulia kwa kitendo cha kumuweka na yeye kwa Diamond ilhali anajua kwamba tayari ana wanawake kadhaa tayari Kwenye Mahusiano naye.

Baada ya povu hilo la mashabiki, Husna alifanya mahojiano na Global Publishers ambapo alimwaga povu kwa watu wanaosema anamtaka Diamond ambaye ni bwana wa Lynn.

Unajua kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, huyo Lynn ni nani, siwezi kumuhofia yeye wala mwanamke mwingine yeyote maana kila mtu na bahati yake, wanaotukana watukane watachoka”.

Hivi Diamond tayari amekwisha mmwaga Lyyn na Yupo Kwenye Mahusiano na Mrembo mwingine anayeitwa KimNana.