Harmonize: Namchukulia Wolper Kama Shabiki Wangu Tu

Msanii wa Bongo fleva maarufu kama Harmonize ameibuka na kudai kuwa anamchukulia Wolper kama shabiki wake tu na hakuna kingine.

Mwanzoni mwa wiki hii Jacqueline Wolper, ambaye ni mpenzi wa zamani wa Harmonize na Sarah, ambaye ni mpenzi wa sasa wa Harmonize waliingia katika vita kali ya maneno mtandaoni baada ya Sarah kudai kuwa Wolper bado anamtaka Harmonize. Sarah alivujisha meseji za Wolper mtandaoni na kupelekea Wolper kuchefukwa hivyo kumwambia Sarah kuwa alimuazima Harmonize kwa muda tu anaweza kumchukua muda wowote.

Baada ya hapo Wolper alianza kujirekodi anaimba wimbo mpya wa Harmonize unaotamba hivi sasa ‘Shulala’ na hivyo kupelekea minong’ono ya watu kuwa Harmonize na Sarah wameachana na Wolper kamchukua tena Harmonize kwani alimwambia siku nikimtaka Harmonize namchukua tena.

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na XXL ya Clouds Fm, Harmonize aliweka wazi kuwa anashukuru mchango mkubwa wa Wolper katika nyimbo yake mpya kwani amejirekodi video mbili akionekana akifurahia wimbo huo.

Nadhani mwanzo ilikuwa ni hasira tu, nashukuru kuona mchango wa Wolper kwani namchukulia kama shabiki wangu tu”.

Pia kwenye mahojiano hayo Harmonize aliweka wazi mipango yake ya kuupeleka mziki wake kimataifa zaidi kwani hivi karibuni anategemea kusafiri kwenda Ghana kwaajili ya kurekodi video ya wimbo aliomshirikisha msanii Sarkodie kutoka Ghana, huu ni muendelezo tu wa mafanikio ya Harmonize kwani wimbo wake huu mpya wa ‘shulala’ amemshirikisha msanii Mkubwa kutoka Nigeria, Korede Bello.

Nilikupa Nafasi Ya Kuwa na Harmonize Nikimtaka Ntamchukua, Wolper Amwambia Sarah

Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper amfungukia mpenzi wa Harmonize Sarah kuwa yeye ndo alimuachia Harmonize kwaiyo siku yoyote akimtaka atamchukua tena.

Miezi michache iliyopita Wolper aliweka wazi kuwa walipokuwa kwenye uhusiano na Harmonize, ex wake huyo alianza kuchepuka na mzungu Sarah kutokana na kipato chake kikubwa yaani Sarah alikuwa anamhonga Harmonize ili awe naye na amuache Wolper baada ya kutambua hilo Wolper ndo alikuwa wa kwanza kumuacha Harmonize na baada ya hapo Harmonize akaweka hadharani mahusiano yake na Sarah.

Tangu hapo Wolper na Sarah wamekuwa wakijibishana kwenye mitandao ya kijamii. Siku ya jana Srah alweka hadharani maongezi baina yake na Wolper waliyoyaongea faragha keen he maongezi hayo Wolper aliweka wazi kuwa endapo Sarah ataendelea kumfatilia basi atamchukua Harmonize kutoka kwenye mikono yake.

Tafadhali usinitafute ongea na mwanaume wako we ni chizi nini? Alihoji Wolper kwenye meseji hizo, Unanitafuta tena Sarah? Sema ndio uone nitakacho kufanyia! Siwezi kuwa na Harmonize ila ukiendelea kunifuata fuata nitamchukua. Mimi ndio nilikupa nafasi wewe use naye kwaiyo usije ukafikiria hata kwa sekunde kuwa ntasita kumchukua tena, mimi ndo nilikuachia uwe naye na nikimtaka vile vile namchukua! Aliandika Wolper.

Baada ya mazungumzo hayo kuvuja wapo watu wengi waliodai kuwa aliyesambaza meseji hizo siyo mwengine bali ni Harmonize ili tu apate kiki ya wimbo wake mpya alioutoa juzi.

 

Simjui Brown, Ila Wolper Akinitaka Namkubali -Msami Baby

Mwanamuziki na dancer Msami baby kutoka nyumba ya vipaji THT amefunguka na kudai kuwa Jacqueline Wolper ni msichana mzuri hivyo akimtaka hawezi kukataa.

Msami ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji wa bongo movie Irene Uwoya baada ya tetesi kuenea kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na Wolper.

Katika mahojiano aliyoyafanya na Bongo 5, Msami amedai kuwa hamfahamu mpenzi mpya wa wolper anayejulikana kwa jina la Brown hivo ikitokea Wolpee akamtongoza basi hatasita kuwa naye.

“Mi namjua Wolper simfahamu huyo Brown, mpenzi wa mwisho wa Wolper ninayemfahamu ni Harmonize kwaiyo Wolper ni msichana mzuri akiniambia ananipenda why not bwana?  Alafu sina haja ya kumtumia DM yaani mi namfuata moja kwa moja si ninajua kama anapatikana na yeye kama ananipenda ataniambia basi tutakua pamoja”.

Katika upande mwingine Msami aliweka wazi uhusiano wake na mwanamuziki Nandy;

“Sina uhusiano wa kimapenzi na Nandy, yule ni kama dada yangu au mdogo wangu inawezekana siku moja tukaqa zaidi lakini kwa sasa ni marafiki yaani kwa maana wote tumetokea kwenye familia ya THT kwa hiyo ni kama familia yangu”.

Msami amewahi kukiri kuwa anavutiwa na wanawake wakubwa kiumri kuliko yeye na moja ya mpenzi wake aliyemzidi umri ni mwana dada Irene Uwoya.

“Siamini kama bff anaweza kunifanyia vitendo vibaya”-Wolper

Msanii wa Bongo Movies na mjasiriamali ambae amekuwa na skendo za hapa na pale mitandaoni lakini amekuwa akionesha kuzoea na kutokujali maneno ya watu Jackline Wolper   ameongea na kufunguka kuwa mpenzi wake mpya aliyenae sasa hivi ambae pia ni   mwanamitindo   anaejulikana kwa jina la Brown ambae yeye  Wolper amezoea kumuita ‘bff’ kuwa mwanaume huyo  ndie mwanaume anaemuamini sana na anajua kuwa ni mwanaume wa tofauti kuliko wanaume aliowapitia hapo awali.

Wolper ambae alikuwa katika mahusiano ya kimapenzi  na msanii wa muziki wa Bongo Fleva Harmonize na kuachana hivi karibuni kwa kutupiana maneno katika mitandao  alimsifia mpenzi wake huyo mpya na kusema kuwa kaka huyo ni mcha Mungu sana hivyo anaamini hawezi kufanya mambo mabaya kabisa kama kule alipotoka.

Ingawa wolper ameonekana kukiri kuwa katika mapenzi wanaume sio wa kuwaamini na wengi wana matendo ya kufanana, lakini anaamini bff wake hawezi kufanya mambo kama hayo.

“Siamini kama bff anaweza kunifanyia vitendo vibaya kama nilivyowahi kufanyiwa  hapo awali .Namuamini sana kutokana na kuwa yeye   ana hofu ya Mungu , lakini sisi bado ni binadamu,anaweza kunikosea kawaida au mimi nikamkosea hiyo ni kawaida  kwa sababu sis ni binadamu  hiyo haitanifanya nimchukie, lakini akifika huku pa kunifanya  niumie kama nilikotoka nitaamini kuwa hakuna wa kumuaini tena katika mapenzi ” anasema Wolper.

Licha ya bifu zinazoendelea kati yake yeye na mpenzi wake wa zamani  na kuumizwa na mwanaaume huyo kama anavyodai yeye mwenyewe lakini bado  anaamini kabisa kuwa mwanaume aliyenae sasa ndie mwanaume aliyekuwa anamtaka na kumtafuta siku zote sababu ni mcha Mungu na ana heshima pia.

Ingawa kumekuwa na maneno mengi  katika mitandao watu wakisema  tangu awe na mahusiano  na  mwanaume huyo aliyenae sasa kuwa ni mdogo huku watu wakimuita Wolper ‘sugar mamy’, lakini kwake hajali maana anaamini kuwepo kwa mapenzi ya kweli kati yake na bff , hivyo kwa Wolper umri sio kigezo cha kumtenganisha na bff wake

Sarah,mpenzi wa Harmonize amjibu Wolper

Ikiwa ni  siku moja tu imepita tangu Harmonize na Wolper waingie tena kwenye bifu  zito baada ya msanii huyo wa lebel kubwa nchi ya wasafi kutoa wimbo ambao ulilenga kutoa siri za mahusiano yake na mpenzi wake huyo wa zamani Wolper ,wawili hao walijikuta katika malumbano mazito ambayo mpaka sasa yanaendelea mitandaoni huku kila mmoja akikataa kushindwa na kunyamaza ,katika post yake aliyotoa jana katika ukurasa wake wa instagram wolper aliandika kumshauri harmonize kuacha kuandika nyimbo ambazo zinamuhusisha yeye bali ajitaidi kuandika nyimbo ambazo hata zitakuwa zikimsifia mpenzi wake mpya anaejulikana kwa jina la sarah, pia Wolper aliandika maneno yaliyodhihirisha kuwa harmonize alimfata Sarah kwa sababu ya pesa.

Akitoa majibu ya post ya Wolper ,Sarah  aliandika hivi katika ukurasa wake wa instagram ” kama nilimpa hela nyingi akakuacha na wewe si umpe hela akurudie”, mwanamke huyo  wa Harmonize alikuwa kimyaa kipindi chote cha malumbano ya wawilio hao lakini sasa nae kaamua kufunguka ,hata hivyo Sarah pia alionesha dharau kwa kumwita mpenzi mpya  wa wolper “msukule”, “mbeba pochi” .Sarah ambae aliambiwa na Wolper kuwa hajui lugha leo anaamua kusema kuwa post hiyo ameiandika kiswahili kwa msaada wa mpenzi wake harmonize na kumtagi kabisa,” nimeandika kiswahili kwa msaada wa Harmonize”

Hata hivyo vita hiyo ya kimtandao sasa inaonekana kuwa kubwa kwa sababu imekuwa ni kati ya Harmonize na mpenzi wake Sarah huku Jackline Wolper ,  na inakuchukua taswira mpya kwasababu inakuwa kama kila upande  unaokuwa na wivu  na upande mwingine.

Ikumbukwe kwamba wawili hao wameachana muda mrefu lakini vita hii imeanza upya baada ya Jackline wolper kuamua kufunguka sababu ya kuachana na harmonize ambapo kati ya mengi aliyoyasema alisema kuwa mwanamke mpya  ambae ndio sarah alikuwa chanzo cha yeye kuachana na mwanaume huyo huko pia hela imetajwa kama kivutio cha mapenzi kutoka kwa mwanamke huyo.Je mpenzi mpya wa Wolper ataingilia kati, au watayamaliza wenyewe….

Jacqueline Wolper atokwa na machozi baada ya kuona jinsi vijana walivyong’ang’ania nafasi za kazi

Ukosefu wa ajira nchini ulidhihirika hivi karibuni wakati TRA ilitangaza nafasi za kazi. Maelfu ya vijana walijitokeza kuwania nafasi chache za kazi ambazo zilitangazwa na TRA.

Jacqueline Wolper aliweka picha ya vijana waliojitokeza jana katika usaili wa kazi TRA na kuandika ujumbe mrefu akieleza namna alivyoguswa;

“Nikiangalia picha kama hizi naumiaga sana nanilivyo na machozi ya karibu basi nalia kabisa…?

Yaani naona hata wadogo zangu miongoni mwa hawa wanaopigania nafasi yakupewa kazi

Na ukizingatia nimesomesha wadogo zangu kwa tabu sana tena nilikuwa sina hata biashara huku nikisaidiana na wazazi wangu.

Roho inakuuma pale ambapo mdogo wako anakwambia Dada nimepata kazi ya kujishikiza kwa weeki tatu nitalipwa laki na nusu kule Mbeya kijijini tena hapo ni uliyefikiria akipata degree yake atakuja japo kutuinua ama lah! Basi ajitegemee mwenyewe Dah!

Yaani najiskiaga hasira siku moja mpaka nikamsema mdogo wangu..bila kujua kumbe anaumia anatamani muda na pesa tulizopoteza hata apate wakati wakulipa fadhila na sisi tucheke natujue umuhimu wake kwetu lakini ndo hivyo… Maskini ukimwambia subiri utapata kazi hakuelewi anakuona unampotezea muda..anaishia kukujibu basi Dada we unajulikana niombee kazi ?

Mimi najiuziliza unaposema ipo siku ipo siku sijui hiyo siku ni ipi… haya hapa wote hawa wanaohitajika ni wachache (yaani kwa uwiano ni kama mtu mmoja achaguliwe kati ya watu 140) kwasababu ni watu 56,000 kwa nafasi 400…(kama data ziko sahihi) …ohh my God…

Bora hata huyu mdogo wa Wolper ataomba kaela kavocha nakula na kulala atapata vipi waliosomeshwa na wazazi wakambo au kwa msaada??? au ambao wanapotokea hakuna hata lingine??. Aisee polen sana ndugu zangu na nyinyi mliopata kazi basi heshimuni saana sana kazi zenu. Nawaombea na mabosi pia wawafikirie.”

 

Jacqueline Wolper: Nitukane mimi usitukane damu yangu

Jacqueline Wolper ametoa onyo kali kwa wanaopenda kumkemea. Staa huyo wa filamu za Bongo amesema kuwa yuko tayari kuenda jela kwasababu ya kupigania wazazi wake.

Akiongea na Planet Bongo ya East Africa Radio, Wolper alisema kuwa yeye huwa mpole kwa kawaida lakini mtu akijaribu avuke mpaka na kuguza familia yake hapo ndo kichaa chake huamka.

Mrembo huyo alieleza kuwa huwa haweki familia yake kwa Instagram kwasababu hataki wahusishwe na mambo yake, alitoa onyo kwa kusema kwamba mtu yeyote atakaye tusi familia yake ataona cha mtema kuni kwani yeye haogopi jela.

“Kwa mimi binafsi Jackline Wolper ni mpole, lakini ukija kwenye issue za wazazi mi nitaenda Segerea, ndiyo maana hujawahi kusikia Jackline Wolper kamuweka mama yake au baba yake kwenye instagram, kwenye Tv, yani sitaki wazazi wangu wahusike, nitukane mimi usitukane damu yangu, au usitukane mtu aliyenileta duniani, yani dakika sifuri nitapelekwa tu jela,” alisema Wolper.

 

Wolper amrarua Madee kwa kutumia katuni yake

Jacqueline Wolper amekerwa na hatua ya Madee kutumia katuni ya picha yake bila idhini yake kwenye video ya wimbo wake ‘Sikila’ aliyomshirikisha msanii Tekno kutoko Nigeria.

Mrembo huyo alidhihirisha kuwa hakufurahia alichofanya Madee kwa mtandao wa Instagram ambapo aliweka picha ya katuni yake na kuiambatanisha na ujumbe mrefu:

Picha ya katuni ya Wolper aliyotumia Madee kwenye video yake

“Hebu ona jamani, macho yanatia huruma kama nina upwiro kilo 200. Hii mikaka yetu ya Kibongo kuna muda inaboa, kuna muda inakuwa poa. Sasa Madee, Rais wa Manzese nikuulize swali, ulishindwa nini kunyanyua ka simu kako na kunipigia hata kinafiki na kuniambia unani-video queen katuni, sijui sanamu?

“Unajua wewe, acha dharau, wewe pumbavu, piga simu, omba kwanza, hata kama humlipi mtu, sisi tunasaidiana, wote wasanii, leo kwangu, kesho kwako na kunishika kimahaba, umenishika, una dhambi wewe kaka na suti umenivalia kama unaenda kutoa posa kwa Masawe.

Madee

“Sasa onyo, siku nyingine omba utapewa, acha kuparamia kama vile unaomba raundi kwa kimada wako, kwanza unitafute utoe hata faini ya kuniweka macho kama nimevuta ugoro.

“Ila nyimbo kali, nisiwe mchoyo na nimependa idea ila mwambie alinichonga na kunipa hiyo shepu nitampasua,” Wolper aliandika.

 

Dk Fadhili Emily: Kama singekua nimeokoka ningemuoa Jacqueline Wolper

Mpenzi wa zamani wa Jacqueline Wolper amefunguka na kusema kuwa mrembo huyo anafaa kuwa mke wa mtu. Dk Fadhili Emily amemsifu Wolper kwa kusema kuwa muigizaji huyo anaweza akawa mke mwema kwa atakaye muoa.

Fadhili alisema haya baada ya kuzuka kwa madai kuwa Wolper hawezi kuolewa kwasababu ya yeye kuwa na msururu wa wanaume ambao amekua na mahusiano nao. Fadhili alieleza kuwa angemuoa Wolper lakini yeye sasa ameokoka na pia amepata mpenzi mwingine.

Dk Fadhili Emily na Wolper kwenye picha ya zamani

“Nimeona kwenye mitandao, wanamuandama kuwa hajatulia na kwamba ana msururu mkubwa wa wanaume ambao ametembea nao, kimsingi huyu mrembo hajapata tu mtu sahihi lakini anafaa kuwa mke wa kulea familia kabisa,” alisema Fadhili.

 

Jacqueline Wolper adai ataendelea kubadili wanaume kila kukicha

Muigizaji wa filamu za Bongo Jacqueline Wolper ako na tabia ya kubadili wapenzi kila kukicha. Na sasa amekiri kuwa hatawacha tabia yake hio.

Wolper alipokuwa na mahusiano na Harmonize watu wengi walidhani mapenzi yao yatadumu lakini wawili hao waliachana na kila mmoja kupata mpenzi mpya.

Wolper akiwa na mahusiano na Harmonize

Wolper alijinyakulia kichana mwingine mchanga anayejulikana kwa jina la Brown ilhali Harmonize alipata mpenzi mpya mrembo wa kizungu.

Katika mahojiano na Risasi Mchanganyiko hivi karibuni, Wolper alikiri kuwa ataendelea kubadili wapenzi muda wowote atakapogundua kuwa aliyenaye hana vigezo.

Wolper na mpenzi wake mpya Brown

Mrembo huyo alieleza kuwa hawezi kuogopa maneno ambayo watu wanasema kwani hawaelewi anachokumbana nacho katika mapenzi, alisema kuwa hawezi kung’ang’ania kukaa kwenye uhusiano ambao haendani nao au unampa shida.

“Unajua unapokuwa na mpenzi huwezi kujua kuna tabia utakumbana nazo ambazo haziendani na wewe, lakini pindi unapogundua ni bora kuondoka kuliko kukaa sehemu ambayo huna furaha nayo,” alisema Jacqueline Wolper.

 

 

Wolper: Sina wivu na Harmonize

Jacqueline Wolper hana machungu yoyote na mpenzi wake wa zamani – Harmonize. Mwigizaji huyo wa filamu za Bongo alisema kuwa aliachana na Harmonize miezi sita iliyopita. Alieza pia vitu vinavyo mvutia kwa mpenzi wake mpya – Brown.

“Tumeachana kama miezi sita hivi tulikuwa hatuelewani. Huyu BFF yaani Best Friend Forever tuna kama wiki hivi. Tulikutana vizuri tu alianza kuniona kama miaka minne hivi before. Kinachonivutia kwake ni mpole na mkweli, kwa hiyo ni rafiki yangu mzuri sana,” Wolper alisema kupitia kipindi cha The Weekend Chart Show ya Clouds TV.

Jacqueline Wolper na Brown

Wolper hata hivyo alisisitiza kuwa yeye na Brown ni marafiki tu wala sio wapenzi;

“Mimi siwezi kuingia kwenye vita na siwezi kuwa na uchungu japo stress hazifichiki na furaha haifichiki. Kwa hiyo nyie mnaweza mkajadili. Vitu vya instagram siyo vya kweli vyote japo wanakuwa na vitu vyao vina ukweli kidogo. Huyu kaachana na mtu wake miezi miwili halafu mwezi wa tatu tukakutana. Kwa hiyo, hizo ni story tu wote tumekutana single ila tofautisha wale ni wapenzi na sisi ni BFF na tupo serious. Ni marafiki wa kweli. Mimi siyo mtu wa TV naye siyo mtu wa TV.”

 

Jacqueline Wolper ajibu wanaosema amenyakua mume wa mtu

Inasemekana kuwa mpenzi mpya wa Wolper anayejulikana kama Brown ni mume wa mtu. Wolper amekemewa kwa tendo lake la kupora mume wa mtu.

Hata hivyo muigizaji huyo wa filamu ya Bongo amewajibu wanaomsuta kwa kusema kuwa mtu yeyote anayedai kuwa Brown ni mume wa mtu ajitokeze hadharani kuliko kusema mitandaoni.

Soma pia: Picha 10 za mpenzi mpya wa Jacqueline Wolper

Akiongea na Amani, Wolper alisema madai mitandaoni ni ya upuzi kwani hakuna mtu aliyeibuka na kusema Brown ni mumewe kabla ya yeye kuanza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Brown.

Jacqueline Wolper na Brown

“Kinachonishangaza ni kitendo cha mimi kuwa naye tu ndiyo watu wanaanza kuibuka na kusema eti ana mke, duh! Mbona kipindi siko naye, hakuna mwanamke ambaye alikuwa anasema ni mumewe. Sasa basi kama kuna mwanamke ambaye anadai ni mumewe ajitokeza hadharani. Nilichogundua baadhi ya wanaoibuka ni wale ambao waliwahi kuwa naye kitambo, sasa nasema hivi, huyo anayesema ni mume wake basi ajitokeze,” alisema Wolper.

 

Wolper aonyesha sura ya mpenzi wake mpya aliyechukua nafasi ya Harmonize

Kuna dhana kuwa muigizaji wa Bongo Movies Jacqueline Wolper anapenda vijana ambao yeye amewazidi umri, kuna ukweli kwa dhani hii.

Wolper alitengana na Harmonize miezi chache iliyopita, staa huyo wa Wasafi alijinyakulia mpenzi wa kizungu ambaye ameshamtia mimba.

Wolper pia sasa amejinyakulia mpenzi mwengine, muigizaji huyo ameachia picha zikimuonyesha akiwa na kijana ambaye amechukua nafasi ya Harmonize.

Baadhi ya picha ya Wolper na mpenzi wake ambazo ziko kwenye mtandao wa Instagram, kuna picha moja inaonyesha Wolper na huyo kijana aitwaye Brown wakiwa kitandani.

Ujumbe wa Wolper kwa Diamond yawasisimua watu mtandaoni

Muigizaji wa filamu ya Bongo Jacqueline Wolper ametuma ujumbe kwa Diamond ambaye anasherekea siku ya kuzaliwa kwake leo.

Mrembo huyo alimsifu sana Diamond kwa kuinua sanaa nchini Tanzania kwa kuwasaidia wasanii wengine kunawiri kimuziki.

Jacqueline Wolper na Diamond

Ujumbe wa Wolper kwa Diamond uliwasisimua watu wengi mtandaoni, soma ujumbe huo hapo chini:

“Natamani kila mtu ajue roho yako nzuri na mchango wako ktk nchi yetu na jinsi gani umeweza kuinua wengine tunaowajua na tusiowajua pia!kijana mdogo lkn umeweza kukubalika nje na ndani ya nchi,kiufupi jina lako linaendana na roho yako una moyo wa almasi plus dhahabu unajua kula na vipofu mpk vilema ndo maana Mungu anakufungulia ridhiki zako..Wewe ni zaidi ya Almasi buana,Endelea kutuburudisha na mziki mzuri baba Tee….Happy birthday to you baba Nillan..Sema nn birthday yako bado sana mpk mwezi wa kumi mbali kapicha nako kameshawishi alafu maneno yangu pia yata expire???Nweiiz Nimejisikia tu ndugu zangu,sio mbaya na nyie mkifunguka kwa mazuri yake bwana Ngote #myboss”

 

“Sina ukaribu wa kihivyo na Zari” Jacqueline Wolper afunguka kwanini hakumfariji Zari Ivan Ssemwanga alipofariki

Watu wengi akiwemo Wema Sepetu walimfariji Zari Hassan alipofiwa na mmewe wa kitambo Ivan Ssemwanga. Lakini Jacqueline Wolper alishindwa kumfariji Zari.

Lakini ni kwanini Wolper hakuenda kumfariji Zari? Akizungumza na Wikienda, Wolper alisema kuwa Zari na yeye si marafiki wa karibu.

Ivan na Zari

Mrembo huyo pia alisema Ivan alipokufa alikuwa nchini Burundi alikokwenda kwa ajili ya kuchukua mzigo wa dukani kwake hivyo alikuwa bize na hata kama angekuwepo Tanzania bado hangeenda kumfariji Zari.

“Nilikuwa bize na biashara na hata kama isingekuwa hivyo nisingeenda kwa sababu sina ukaribu wa kihivyo na Zari bali siku zile kwenye video iliyosambaa nilikuwa namtetea kwa sababu sipendi mtu aonewe, yaani watu wanamweka mitandaoni amezeeka wakati ukimuona live ni mzuri na mrembo kabisa, sipendi uonevu katika maisha yangu, mimi ni mtetezi wa wanyonge, sema watu hawanijui wananichukuliaga tofauti,” alisema Wolper.