Muigizaji mkongwe wa Bongo movie Yvonne Cherry maarufu kama Monalisa ameibuka na kuweka wazi kuwa hana Bifu na msanii mwenzake Kajala Masanja bali watu wanataka tu kuwagombanisha.
Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Jumamosi, Monalisa alisema watu wamekuwa wakizungumza maneno mengi ambayo yanaweza kusababisha wagombane wakati wao wako vizuri, hawana tofauti yoyote kama watu wanavyosema.
Sina bifu na Kajala ila naona watu ndiyo wanataka kutugombanisha, naomba watu waache maneno jamani ili maisha mengine yaendelee maana kila siku ni hilohilo tu“.
Monalisa amesema Baada ya sakata la matokeo ya kidato cha nne yaliyotoka Wiki chache zilizopita amvbapo Watoto wa wasanii hao walikuwa wanasoma shule moja Lakini Baada ya Mtoto wa Kajala Kufeli na Mtoto wa Monalisa kufaulu kuna maneno ya uchochezi yalizungumzwa kupelekea kuonekana kama wana bifu.