Kevin Gates Awakubali Diamond Platnumz na Rayvanny

Msanii wa muziki wa Hip hop kutoka pande za Marekani Kevin Gates ameonekana kuikubali nyimbo mpya ya Rayvanny na Diamond Platnumz Baada ya kuonekana akiwa anaisikiliza.

Kevin Gates ambaye alishawahi kutamba na ngoma kibao ikiwemo ‘Out The Mud’ ameposti kipande cha video kwenye ukurasa wake wa Instagram, akisikiliza ngoma ya Tetema.

Tetema imeendelea kuvunja rekodi kuanzia kuwa nyimbo ya kwanza Tanzania kutazamwa mara milioni moja ndani ya mastaa 17 Mpaka kufikisha watazamaji milioni 3 ndani ya siku tatu.