Lungi Amcharua Gigy Money Kisa Zari

Muigizaji mkongwe wa Bongo movie Lungi Maulanga amemwagia povu zito msanii wa Bongo fleva Lungi Maulanga kisa Mzazi mwenza wa Diamond Platnumz, Zari The Bosslady.

Lungi ameibuka na kudai hakufurahishwa na maneno yaliyotolewa na Gigy Money na kuelekezwa kwa Zari siku chache zilizopita baada ya wawili hao kuingia kwenye majibizano ya Mtandaoni.

Kwenye Interview yake na gazeti la Ijumaa, Lungi alisema amekuwa akikerwa mno na Gigy ambaye amekuwa akitoa kauli ya kuwa yeye ni mzuri na mrembo kuliko Zari, jambo ambalo siyo kweli kwani msanii huyo hawezi kumfikia hata robo mwanamama huyo ambaye ni raia wa Uganda mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini.

Huyo Gigy alipata jina kwa kukaa utupu, lakini Zari ni mwanamke mpambanaji na ana pesa zake siyo anadanga, sasa namshangaa huyo mtoto kujilinganisha naye.

Ni bora hata mimi nikajilinganisha naye kwa sababu hapa nina watoto wanne, lakini bado ninaonekana mrembo.

Sina hata tumbo, lakini yeye mtoto mmoja tu utadhani anao zaidi ya watano, namsihi anyamaze na aache kutafuta kiki kupitia jina la Zari maana siyo levo zake”.

Gigy Money alimwagia povu zito Zari mara baada ya kutoa kaulia ambayo mwenyewe aliamini ilikuwa imelenga kumdhalilisha.

Baada Ya Kutuma Maombi kwa Mh. Rais ,Lungi Amshambulia Ray C

Wiki chache zilizopita msanii wa kike Rehema Chalamila maarufu kama Ray C alimuandikia Mh.Rais Magufuli barua na kumuomba  kuweka sheria ya kuzuia ufuksa katika nyumba za kulala wageni kwa kutunga sheria itakayo waamuru   watu wanaoingia katika nyumba za wageni wawe ni wale waliofunga ndoa  na wanapofika maeneo haya watoe na vyeti vya ndoa kuthibitisha kuwa wana ndoa iliyo halali. Msanii mwenzie Lungi Maulanga amemjibu na kumshambulia kuwa maneno hayo ameyasema kwa sababu hana ndoa na hayajawahi kumkuta yanayowakuta.

Msanii huyo wa kike anasema kuwa Ray C hakupaswa kuyaongea hayo ilhali hana ndoa alipaswa kuyaongea haya siku akiwa ameshaingia katika ndoa na ameyaona yanayopatikana katika ndoa ndio aweze kusema hayo yote.

ninavyomjua ray c ni kwamba hajaolewa sasa hayo anayomwambia mheshimiwa anatakiwa kuyafanyia kazi kwanza yeye kwa sababu ninachoamini kuwa hata yeye bado anaingia katika nyumba za wageni na wala hajaolewa.anatakiwa atupe mfano kwnza kutoka kwake  sababu najua sheria hatungi yeye. Alifunguka Lungi

Hata hivyo majibu ya Lungi kwa Ray C haijafamika kama amemjibu kwa ugomvi au ni kitu gani kilimkera kutoka kwa maoni ya msanii mwenzie huyo ilhali haijawahi kuripotiwa kwamba wawili hao walishawahi kuwa na mgogoro wowote kabla.