Mabeste Awatolea Povu Wanaodhalilisha Wanawake

Msanii wa muziki wa kizazi kipya wa siku nyingi MABESTE amefunguka na kutoa dukuduku lake la moyoni kuhusu baadhi ya wanaume wanaokaa kutwa kuwadhalilisha wanawake wanaokuwa nao katika mahusiani hata kama wanakuwa tayari wameshaachana nao.

Mabeste anasema kuwa wanaume wamekuwa na tabia ta kuwadhalilisha sana wanawake wao huku akisema kuwa ameumizwa  sana na swala la wema na PCK.

Mabeste anasema kuwa kwa muda sasa mambo kama haya yamekuwa yakitokea na wamekuwa wakitasikia lakini ifike sehemu inabidi wanaume wajifunze kuwaheshimu na kuwapenda wanawake zao kama vile ilivyokuwa kwa mamamzao na hata dada zao wanapokuwa nyumbani.

Mabeste anasema kuwa wanawake ni zaidi ya ndugu kwa sababu mpaka mnaamua kuwa mwili mmoja kuna vitu vingi mnakuwa tayari mmeshajitoa kuvifanya hivyo ni vizuri kuwaheshimu, hata hivyo mabeste anasema kuwa ikitokea mnaamua kuachana basi ni bora kuachana kwa amani na kila mmoja afanye mambo yake.

Mabeste ni moja ya wasanii waliokaa katika ndoa kwa muda mrefu na kupoitia magumu mengi na mama watoto wake lakinikila siku amekuwa akimuweka mke wake katika  kipaumbele cha maisha yake.

 

 

Mabeste Awatolea Povu Wanaume Wanaodhalilisha Wanawake

Msanii wa muziki wa Bongo fleva aliyewahi kutawala kwenye gemu Venance William maarufu Kama Mabeste amewaji juu wanaume ambao wanadhalilisha wanawake.

Mabeste amezungumza hayo Baada ya kuwepo matukio mengi ya wanaume kudhalilisha wanawake waliozaa nao au waliokuwa nao likiwemo lile la muigizaji Wema Sepetu na mpenzi wake PCK.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Mabeste alisema kuwa, vijana inabidi wajitambue na kuwaheshimu wake zao kama ambavyo wanawapenda na kuwaheshimu mama zao kwa sababu wanastahili heshima na thamani.

Unapomdhalilisha mke wako au mwanamke wako ni sawa na umejidhalilisha mwenyewe kwa sababu mwisho wa siku nyie ni mwili mmoja, kama mnafikia uamuzi wa kuachana achaneni kwa amani sio mpaka kila mtu ajue majirani au mitandaoni”.

Msanii mkubwa Kama Diamond Platnumz ameshawahi kunyoshewa kidole kwa kudhalilisha wanawake aliozaa nao Baada ya kuweka video na picha za faragha Waliowahi kuwa wapenzi wake Hamisa Mobetto na Zari.

Mabeste Afungukia Bifu Lake na Juma Jux

Msanii wa muziki wa Bongo fleva ambaye anafanya muziki wa kurap Venance Mabeste maarufu kama Mabeste aliyewahi kuhit na ngoma zake kama ‘Sirudi nyuma’ na ‘Baadaye sana’ amefungukia bifu lake na msanii mwenzake Juma Khalid ‘Jux’.

Mabeste ambaye aliwahi kuhit sana miaka kama nane iliyopita ameachia ngoma mpya, ngoma inaitwa Chakusema ambayo imefanywa na Prodyuza Rush The Don huku kichupa kikifanywa na Paxpyne.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Mabeste amefunguka kuhusu mengi lakini moja kati ya vitu vilivyokiki siku za nyuma kidogo ni bifu lake na Jux na anafunguka zaidi:

Kuna hali ya kutoelewana tu ilitokea huko nyuma na sipendi kuizungumzia sana. Lakini Jux ni mshikaji, tumetoka mbali sana kabla hata hajaenda China kwa ajili ya masomo”.

Lakini pia Mabeste amefunguka kuhusu uhusiano wake na ushkaji wake na Jux kwa sasa unaendaje:

Siyo mbaya. Ninamshukuru, ingawa hatukutani kama ambavyo ilikuwa zamani. Kwa sasa tumekwishakuwa watu wazima, kila mmoja ana majukumu yake, kwa hiyo muda mrefu huwa unapita bila kukutana wala kuwasiliana“.

Wasanii Wanahitaji Elimu Ya Uwekezaji- Mabeste

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kurap Mabeste amefunguka na kudai kuwa wasanii wengi wanahitaji kupewa elimu ya uwekezaji.

Mabeste amefunguka na kudai kuwa anatamani wasanii wa Bongo wapate elimu ya jinsi ya kuwekeza katika kazi za sanaa na jinsi gani wanatakiwa wafanye kazi hiyo kwa ufanisi zaidi.

Wasanii wengi wa Bongo wana vipaji sana na hata hiki kizazi kipya kinachokuja kina talent sana lakini nilikuwa natamani wapate elimu ili wajue muziki kama biashara nyingine inahitaji msingi ambao msingi wake ni uwekezaji mkubwa ili hata yule investor aoene kile alichoweka kinarudi ili aweze kukuwezesha Kisonga mbele zaidi”.

Lakini pia Mabeste ameongeza kuwa wasanii wengi wanafikiri ni biashara tu na ukiingia unaifanya kirahisi, lakini business ya muziki inahitaji investment na wakati huo huo inabidi faida irejee kutoka Kwenye kazi hiyo.

Mabeste- Nimeamua Kufanya na Biashara Nyingine Maana Muziki Umekuwa Mgumu

Msanii wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kurap Mabeste amefunguka Kuhusu uamuzi wake wa kutafuta kazi nyingine ya kufanya mbali na muziki ili kuweza kutanua wigo wake wa kupata kipato.

Siku za nyuma Mabeste alishawahi Kupitia wakati mgumu hasa lilipokuja suala la kukosa kipato kwani mke wake alipotwa na ugonjwa hali iliyopelekea wasanii kufanya Tamasha la kumchangia chochote kitu.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Risasi Vibes, Mabeste amesema amepitia mengi kwenye muziki lakini hawezi kuacha japokuwa ameamua kutafuta kazi nyingine ya kufanya ili kutanua wigo wa kujiingizia kipato.

Unajua kwa sasa wanamuziki wamekuwa wengi sana na changamoto zimeongezeka tofauti na ilivyokuwa mwanzo kipindi ambacho wanamuziki walikuwa wachache.

Sasa kwa wengine ambao tunaweza kuendelea na mambo mengine imebidi kujiweka kando kidogo huku tunafanya muziki lakini pia tunaendelea na maisha mengine, kwa sababu muziki ni kama zilivyo biashara nyingine.

Lakini limekuwa jambo la kawaida wasanii wa muziki kuanzisha biashara mbali mbali za pembeni za kuwaingizia kipato kwa kujua wazi kuwa hawawezi kufanya muziki milele hivyo inabidi upate kazi ya pembeni ya kufanya mbali na sanaa.

 

Mabeste Afunguka Mazito Kuhusu Mke Wake

Mwanamuziki wa Bongo fleva, Mabeste amefunguka mazito na kumwagia sifa lukuki mkewe anayejulikana kama Lisa Fickenscher ikiwa ni siku ya kumbu kumbu yake ya kuzaliwa.

Mabeste na mkewe wamekuwa pamoja kwa kipindi kirefu sana na ni moja kati ya zile couple ambazo wamepitia mambo Mengi magumu maishani. Tangu Mabeste alipogombana na uongozi wake wa zamani mpaka alipougua ugonjwa wa ajabu lakini wameyavuka hayo yote na mpaka leo bado wako wote.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mabeste amefunguka na kusema kuwa moja kati ya vitu ambavyo hajutii kwenye maisha yake ni kumuoa;

Happy birthday my love sina kitu cha kusema zidi ya kusema nakupenda sana mama watoto wangu wewe ni mvumilivu sana una Upendo wa ajabu na una huruma pia, kikubwa zaidi una akili sanaa ooh thank you God kwa zawadi hii, kuna msemo unasema bora ukosee kujenga nyumba kuliko ukosee kuoa, yaani nakupenda sanaa sanaa kitu kingine kizuri ulicho barikiwa kikubwa sana, unapenda kazi yangu ya music unajua muziki mzuri ukisikia tu japo kuimba ndio hujui. Leo ni siku kubwa sana kwako na kwangu pia kwa sababu leo ndio naachia wimbo wangu”.

Lakini Mabeste hakuishia hapo aliendelea kumfungukia mkewe na kusema “Leo mama wa watoto wangu umezaliwa upya katika Bwana Yesu na pia hata kipaji changu kimezaliwa katika bwana wetu Yesu…kwenye Upendo sana Mungu yupo Muda wote”.