Mume Wa Mama Diamond Afunguka Mazito

Mume wa mama Mzazi wa Msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Mama Dangote amefunguka mazito kuhusu mke Wake na kuamua kuyaanika hadharani kabisa.

Mume wa Mama Diamond anayejulikana Kama Maisara Shamte ameibuka na kumfungukia mazito mke Wake Mama Diamond.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Shamte amefunguka na kueleza Jinsi gani anavyompenda bibi huyo wa wajukuu watano na kusema amemchaganya Mpaka anataka kulipa tena mahari:

Yaani kuna wakati nakuangalia Mama Dangote halafu nasema mbona mahari nimelipa kidogo halafu nimeishia kupata kitu kikubwa sana basi naishia tu kusema Asante Mungu, Yaani Ikifika asubuhi natamani kukuamsha uende shule kwa Jinsi ulivyofanana na vitoto vya shule “.

 

Mama Diamond Amwaga Povu Kulinganishwa na Mobetto

Mama mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi. Sandrah maarufu kama Mama Diamond amemwaga Povu zito baada ya mashabiki wa mtandaoni kumlinganisha na aliyekuwa mkwe Wake Hamisa Mobetto.

Sakata hilo lilitokea siku chache zilizopita baada ya Mama Dangote kuweka picha mtandaoni zilizomuonyesha akiwa amebebwa na Mume Wake Shamte ndipo mashabiki walimtuhumu kwa kumuiga Mobetto.

Siku za nyuma kidogo Mobetto aliweka picha zake na Mpenzi Wake Josh Adeyeye zilizomuonyesha wakiwa wamebebana kimahaba ndipo walipounganisha na zile za Mama Dangote na kumtuhumu kwa kuiga.

Katika mahojiano yake aliyofanya Global Publishers, Mama Diamond alimwaga Povu zito Baada ya kuulizwa kuhusu tuhuma hizo:

Unajua siwezi kujibu swali hilo la ajabu, kwani wewe ukibebwa unajisikiaje? Na hayo mambo ya Mobeto jijibu mwenyewe na uandike unachojisikia“.

 

Mama Diamond Avunja Ukimya Kuhusu Mpenzi Mpya Wa Diamond

Mama wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz   Bi. Sandrah amefunguka na kumuongelea Mpenzi mpya wa Diamond anayejulikana kama Tanasha Donna Oketh mwenye ajili ya Kenya.

Wiki iliyopita Diamond alishangaza watu wengi Baada ya kutangaza ndoa na Mpenzi Wake Mpya Tanasha itakayofungwa 14 February 2019 ilihali alikuwa anadaiwa kuwa kwenye mahusiano na Kimnana.

Gazeti la Risasi Mchanganyiko linaripoti kuwa kumekuwa na taarifa za chini chini kuwa Mama Diamond hamtaki kabisa Tanasha kwa sababu alikuwa anamkubali Kim Nana ambaye alikuwa tayari kubadilisha dini na alikuwa kashaanza kufundishwa Quran tayari kwa ajili ya ndoa na Diamond.

Kwenye mahojiano na Gazeti la Risasi, Mama Diamond alianza kwa kukanusha habari kuwa alimkataa mrembo huyo na kwamba alikuwa anamtaka Kim Nana. Mama Diamond alisema anamkubali Tanasha kwa moyo mmoja wala hana kipingamizi naye na ikitokea mwanaye kweli anataka kumuoa, basi yupo radhi wala hana shida.

Sasa nimkatae amenikosea nini mtoto wa watu? Nani amesema nimemkataa mkwe wangu? Kama  mwanangu amemuona anamfaa basi nipo radhi amuoe maana umri Wake unaenda na umri wa kumuoa ndio huu”.

 

 

Mume wa Mama Diamond Afunguka Kuishi Madale Kwa Diamond

Mume wa Mama mzazi wa Diamond Bi. Sandra aitwaye Shamte Maisala ambaye kwa sasa ndiye baba wa kambo wa msanii Diamond Platnumz, amefungukia tuhuma za kuishi Madale.

Katika mahojiano yake na Global Publishers, Shamte amesema kuwa, anashangazwa na maneno hayo kwani ana kwake lakini anaishi Madale kwa kuwa kote ni nyumbani kwake. Amesema, kikubwa anachokitaka kutoka kwa mkewe ni heshima ya mume na anaipata hivyo suala la kuishi kwake siyo ishu.

Unajua watu wamekuwa wakihoji sana sababu ya mimi kumuoa mama Diamond na kuishi kwake lakini wanasahau kuwa zote ni nyumba, siku tukiamua kukaa Bunju (kwake) tutakaa na siku tukiamua kukaa Madale tutakaa kama tunavyokaa sasa, ishu si makazi bali ni heshima ya mume kwani napikiwa, nafuliwa na huduma zote napata”.

Baada ya Diamond kununua Jumba la kifahari maeneo ya Mbezi beach mapema mwaka huu aliamua kuhama Madale na kumuachia Nyumba mama yake na baba yake wa kufikia.

Mama Diamond Afungukia Uhusiano Wa Ommy Dimpoz na Zari

Mama mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi. Sandra Kassim maarufu kama Mama Diamond amefunguka na kuongelea uhusiano na kinachoendelea kati ya Zari na Ommy Dimpoz.

Siku chache zilizopita msanii wa Bongo fleva Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ na mzazi mwenzake na Diamond Zari the Bosslady walitengeneza headlines baada ya picha zao wakiwa pamoja nchini South Africa kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano na gazeti la Risasi Jumamosi, Mama Diamond amesema kuwa ukaribu wa Zari na Dimpoz ni wa kawaida kama watu wengine na kuwataka watu waache maneno maneno yasiyo na msingi.

Kwani kuna ubaya gani? Hivyo ni vitu vya kawaida kwa mtu kukumbatiana na mtu aliyekutana naye Mimi sijaona hiyo picha ambayo kamshika pajani lakini bado nasema hayo ni mambo ya kawaida tu. Ina maana Zari asiongee na watu? Watu wanasema Nasibu na Ommy wana ugomvi, mimi sijaona wakipigana, najua wanaongea na wala mimi sina ugomvi na mtu”.

Siku za nyuma Diamond aliwahi kuingia kwenye ugomvi mzito na Ommy Dimpoz uliopelekea kutukanana matusi ya nguoni hadi Ommy kumkashifu Mama Dimoand lakini tangu alipougua kuna tetesi kuwa bifu hilo limeisha na wasanii hao wamesahameana.

 

Mama Diamond Adai Kusubiri Kwa Hamu Harusi Ya Mwanaye

Mama mzazi wa msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz. Bi. Sandra Kassimu au maarufu kama Mama Diamond ameibuka na kudai kuwa anasubiri kwa hamu harusi ya mwanaye huyo licha ya kwamba hana taarifa itafungwa lini.

Mama Diamond amefunguka na kuweka wazi kuwa licha ya kwamba anasubiri kwa hamu harusi hiyo lakini hajui tarehe ya mwananye kuoa na wala hajui ataoa mwanamke gani.

Kwenye mahojiano aliyofanya na gazeti la Risasi Vibes, mama Diamond alisema licha ya kwamba Diamond ni mwanaye, lakini hawezi kumchagulia mwanamke wa kuoa kwani hata yeye hakuchaguliwa mwanaume wa kuwa naye hivyo kikubwa anachosubiri ni kusherehekea tu siku hiyo.

Unajua siwezi kumchagulia Diamond  mwanamke wa kuoa bali yeye mwenyewe ndiye atakayechagua maana hata kama watu wanavyosema amuoe Zari (mzazi mwenza wa Diamond) wakati wanakutana na kuanzisha uhusiano wao mpaka wakapata watoto mimi sikuwepo hivyo mambo ya kuoa ni uamuzi wa mtu mwenyewe”.

Diamond ameshazaa watoto watatu na wanawake wawili tofauti lakini mpaka hivi sasa hajamuweka wazi mpenzi wake na kudai yupo single licha ya kuonekana na wanawake kadhaa na hata wanawake hao kumgombania hadharani.

Mama Diamond na Zari Wadaiwa Kuwa Ndani Ya Bifu Zito

Mama mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi. Sandrah au maarufu kama Mama Diamond amedaiwa kuwa kwenye bifu zito na mazi mwenzake na mwanaye mwanamama Zari The Bosslady.

Global Publishers wanaripoti kuwa kuna bifu zito linaendelea kati ya Zari na Mama Diamond huku mtu wa karibu na familia hiyo kuanika kuwa wawili hao waliingia kwenye mgogoro baada ya mama Mondi kubeba ujauzito.

Inaripotiwa kuwa Mama Mondi alipata ujauzito na kumueleza mkwewe huyo kuwa anahitaji daktari mzuri kutoka Afrika Kusini ili ahakikishe kuwa ujauzito huo hautoki kwani anahitaji kupata mtoto na mumewe Maisala Shante ‘Anko’ ili aifurahie ndoa yake.

Unajua kwa nini mama Mondi na Zari waliingia kwenye bifu akamchukia? Ni kwa sababu alimpa siri ambayo alikuwa hajamwambia mtu yeyote ya ujauzito wake yeye akamwambia meneja mmoja wa Diamond ambaye naye alimtania mama bila kujua kuwa ilikuwa ni siri”.

Aidha, mtoa habari huyo alisema kuwa baada ya Zari kumueleza meneja huyo bila kujua kuwa hakutaka mtu ajue na meneja huyo akamtania mama Mondi kuwa ni mama kijacho kitendo ambacho kilimkera ndipo bi’mkubwa huyo alipomchamba Zari.

Unaambiwa mama Mondi alimchamba Zari vibaya na bahati mbaya ujauzito wenyewe ukatoka kwani ulitoka hata kabla hajapata msaada aliokuwa anautaka”.

Baada ya tetesi hioz za bifu na Zari gazeti la Amani lilimsaka Mama Diamond ambaye alikana kabisa bifu hilo na mkwe wake na kufunguka;

Sina bifu na Zari mbona huwa nawasiliana naye kwa njia ya WhatsApp na mara ya mwisho amenitumia picha za watoto na kuhusu kumposti kwenye Instagram mbona tulishaacha kupostiana siku nyingi ndio maana sijamposti lakini hatuna bifu lolote“.

Mama Diamond alipoulizwa kuhusu taarifa za ujauzito alidai kwamba ameshezaa tayari na kwa sasa mtoto wake ameshakuwa mkubwa tuu.

 

Mume wa Mama Diamond Kwenye Skendo Nzito na Mke Wa Mtu

Maisala Shante ambaye ni Mume halali wa Mama mzazi wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi Sandrah amejikuta katika skendo nzito na Mke wa mtu.

Global Publishers wanaripoti kuwa Wamenasa SMS za Shamte ambazo alikuwa anachati na mwanamke ambaye anaaminika kuwa mke wa mtu na kuibua maswali juu ya ukaribu wao ilhali wote wapo kwenye ndoa.

Mwanamke ambaye anadaiwa kuwa mke wa mtu alikuwa anachat kimahaba Lakini pia inadaiwa Kwenye meseji hizo walikuwa wanatumiana picha kudhihirisha mambo yamekolea.

Gazeti la Risasi lilimsaka Mwanamke huyo ambaye alikataa kabisa tetesi za Mahusiano na Shamte na kufunguka haya:

Nimekuambia simu yangu ilipotea, unachoniambia mimi sikikumbuki kabisa kama niliwahi kuchati na huyo mwanaume chochote, lakini pia kama nitakuwa nimechati naye kuna ubaya gani, si mwanaume kama wanaume wengine“.

Baada ya mwanamke huyo kubanwa na kufunguka hayo, Risasi Jumamosi lilimtafuta Shamte ambaye alidai kuwa hana tabia za kuchati na wanawake.

Nakuheshimu kama mwandishi kukujibu swali hili, mimi sijawahi kuchati na wanawake ovyo, kama una namba ya huyo mwanamke nitumie ndio nitakujibu“.

Shamte ni mume halali wa Mama Diamond, walifunga ndoa mwaka jana na baada ya ndoa hiyo kukazuka ‘vijineno’ ikiwemo madai kuwa mwanaume huyo ni marioo na ndoa yao haitadumu. Hata hivyo, wawili hao wameendelea kuwa pamoja na kuwafanya watu waamini kwamba, kweli mapenzi hayachagui umri, kikubwa ni kuwepo kwa mapenzi ya kweli.

Esma Platnumz-Siwezi Tena Kumshauri Mama Yangu

Dada wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Khan maarufu kama Esma Platnumz amefunguka na kuweka wazi kuwa hawezi Tena kuwa mshauri wa mama yake Bi Sandra maarufu kama Mama Diamond.

Familia ya Diamond inafahamika sana Kwenye mitandao ya kijamii kwa kupendelea kuanika mambo yao Kwenye mitandao ya kijamii lakini sasa Esma amepasua kuwa yeye ndiye alikuwa mshauri mkubwa wa Mama yake.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Esma ameweka wazi kuwa kwa sasa amestaafu rasmi kumpa ushauri mama yake kwani nafasi hiyo imezibwa na Baba yake wa kambo.

Nilikuwa ninampa ushauri kama mwanaye maana mimi ndiye mtoto wake mkubwa, lakini kwa sasa mama ana mume wake ambaye ni Anko Shamte kwa hiyo ndiye mshauri wake, sisi tunakaa pembeni”.

 

Esma Akana Tuhuma Za Kula Njama Za Kumchafua Mobetto

Dada wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Platnumz ameibuka na kuandika waraka mrefu wa kukana tuhuma zinazomkabili yeye na kama yake za kumchafua Hamisa Mobetto.

Siku mbili hizi kuna taarifa zilienea Kwenye mitandao ya kijamii kuwa Hamisa Mobetto ameenda kwa mganga wa kienyeji kwa nia ya kuwatengeenezea dawa Familia ya Diamond impende na yeye aolewe na Diamond.

Lakini kuna taarifa nyingine ziliibuka kuwa voice note ambaye Esma na Mama Diamond walisema ilikuwa ni Hamisa Akiongea na mganga ilikuwa ya uongo na inasemekana voice note hiyo ilikuwa imepikwa na Mama Diamond kwa nia ya kumchafua na kumpoteza Mobetto.

Baada ya Tuhuma hizo Esma ameibuka na kudai kwamba yeye pamoja na mama yake hawawezi fanya kitu kama hicho kwa Mobetto.

Dada bora ukae kimya halafu unapata zambi kumshilikisha Mwenyezi Mungu ktk swala km hili kuongopa vitu mbona sie wenyewe tupo Kimya au ndio mnatapatapa embu mjitulize jamani hata MUNGU HAPENDI kwani ye ndio Muamuzi plz naomba msinitungie uongo wa kijinga jinga mlichokifanya wenyewe mnakijua na nafsi zinawasuta sipendi kuniingiza ktk uongo wa kijinga msijisafishe kutaka kuchafua watu. Huyo huyo mama mnaotaka awapende kutwa mnachamba na kumtungia uongo naombeni mkitaka kuweka uongo wenu bora mniweke mimi sio mamaangu. MLICHOFANYA MNAKIJUA
#temporarypost?#mfaMajiHamuishiKutapatapa”.

Lakini pia Esma aliongeza:

Katika maisha ni vema kukaa kimya pindi ukikosea na hasa ukijua wazi kuwa nimekosea ila ukijaribu kufuta au kusawazisha kosa kupitia njia za wasiogusa maisha yako ujue kosa linazaa kosa…Ungetulia maana watu wameshiba vielelezo na ushahidi 100%”.

 

Familia Ya Diamond Yamtuhumu Mobetto Kwa Uchawi

Familia ya staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz imerudi kwenye headlines kwa bifu lao na mzazi mwenza wa Diamond, Hamisa Mobetto.

Bifu la Hamisa na Familia ya Diamond lilianza baada ya Hamisa kuzaa na Diamond ambapo Hamisa alisambaza picha zake na Diamond na hata kuwaitia Shilawadu Mama Diamond na Esma.

Mama Diamond na dada wa Diamond, Esma wamekuwa wawazi juu ya chuki yao kwa Hamisa lakini siku mbili hizi pande Hizi mbili ziliingia kwenye mzozano mkali kwenye mtandao wa kijamii.

Mama Diamond na Esma wamemtuhumu Hamisa kwa uchawi ambapo wamedai kuwa Hamisa alienda kwa mganga kwa nia ya kumloga Mama Diamond na Esma ili wampende na aolewe na Diamond.

Inasemekana kuwa kuna voice note ambayo Hamisa alirekodiwa na mganga akiwa anaongea na kwa kuwa mganga huyo anafahamiana na Mama Diamond basi akamtumia.

Esma, Mama Diamond na Wema wameonekana kumtupia vijembe Hamisa kwa tuhuma za uchawi:

Hamisa hajakana wala kukubali tuhuma hizo za uchawi lakini kuna baadhi ya mashabiki zake wamekuwa wakidai kuwa skendo hiyo imetengenezwa na Mama Diamond na Esma ambao wamefoji Voice note.

Hatimaye Mama Diamond Amkubali Mtoto wa Hamisa Kuwa Mjukuu Wake

Mama mzazi wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi Sandra au maarufu kama Mama Diamond amemkubali mjukuu wake Dylan kwa mara ya kwanza hadharani.

Dylan ni mtoto wa mwisho wa Diamond aliyezaa na Hamisa kipindi bado yupo Kwenye Mahusiano ya kimapenzi na mama watoto wake aliyezaa naye watoto wawili Zarinah Hassan.

Kwa muda mrefu imekuwa ikonekana kama Mama Diamond hana mapenzi kwa mjuukuu wake Dylan kutokana na kuwaposti watoto wa Zari Tiffah na Nillan tu Kwenye mitandao ya kijamii.

Mama Diamond aliwahi kuweka wazi kuwa anamchukia Mama Yake na Dylan Hamisa Mobetto na hata kusemekana kumtembezea kipigo kizito na sababu ni Hamisa kumuita Mama Diamond Shilawadu.

Wikiend iliyopita ilikuwa Birthday ya Mama Diamond ambapo Diamond alimuandikia Mama yake ujumbe mzito akimtaka amsamehe Hamisa na amkubali mjukui wake Dylan na ampende kama wajukuu zake wengine.

Maneno hayo ya Diamond yameonekana kumuingia mama yake kwani Kwenye clip ya birthday yake ameonekana akipokea Keki kutoka kwa Dylan na akimuita Dylan mume wake na Kukiri kuwa anampenda.

 

Mama Diamond- Sitakubali Diamond Apotezwe na Mwanamke

Mama Mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi Sandra maarufu kama Mama Diamond ameweka wazi kuwa hataruhusu mwanaye apotezwe na wanawake wanabe.

Kauli hiyo ya Mama Diamond imekuja baada ya maneno maneno mengi kuzuka baada ya yeye kushangilia Diamond kurudiana na Zari huku akijua wazi kuwa yupo na Hamisa.

Mama Diamond ameweka wazi kuwa hamtaki Hamisa kama mkwe wake kauli iliyosababisha mashabiki kumjia juu kwa kitendo chake cha kutaka kumchagulia mtoto wake mke.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mama Diamond amesema wazi kuwa hawezi kukubali kuona Diamond anapotea na yeye kama mzazi yupo kwa ajili ya kumuweka katika njia iliyonyooka:

Kisa Esma , Mama Diamond Asota Polisi Masaa 6

Wikiend iliyopita mama mzazi wa Diamond Platinumz amejikuta akiingia matatani na kushinda kituo cha polisi baada ya mtoto wake wa kike esma platinumz kukamatwa na polisi baada ya mamlaka inayohusika na kukagua madawa vyakula na vipodozi kumkata mwanadada huyo.

Esma alitiwa mbaloni na polisi baada ya maafisa ya TFDA kugundua kuwa anauza vipodozi vyenye kemikali na kwamba kuna vingine haviruhusiwi kabisa kuuzwa katika saluni yake iliyopo sinza afrika sana jijini dar.

Taarifa zilielezea kuwa esma alikamatwa baada ya maafisa hao kupita katika mduka mbalimbali wakifanya msako wa kuwakamata watu wanoendelea kuuza vipodozi vyenye kemikali ndio mama yake alipoambata na Petit Man ambae ni mume wa Esma mpaka kituoni hapo kwa ajili ya kumnasua mikononi mwa polisi.

Mama diamond ambae alikuwa akionekana kulumbana na polisi ili mwane kuachiwa aliambiwa  na polisi kuwa sio jukumu lao kumtoa Esma mpaka watakapopata amri kutoka kwa maafisa wa TFDA kwanza ndio waweze kumuachia.

Hata hivyo mpka siku ya jumamosi mchana mwanadada huyo bado alikuwa akishikiliwa na polisi kityuoni hapo na maswala mengine ya kisheria yakiendelea.

 

Baada Ya Kupewa Kichapo na Mama Diamond, Hamisa Afunguka

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara Hamisa Mobetto amefungukia skendo ambayo imekuwa ikimzunguka kwa siku kadhaa sasa ile ya kupewa kichapo na Mama Diamond.

Kuna habari zilisambaa siku chache zilizopita ambazo zilikuwa zinadai kuwa Mama Diamond alimpa kipigo cha mbwa koko Hamisa baada ya kumkuta nyumbani kwa Diamond Madale.

Mama Diamond alithibitisha taarifa hizo Baada kuwaambia Global Publishers kuwa hampendi Hamisa na kila atakapokutana naye basi atampiga tena kwa kudai amekosa adabu na hataki mtoto wake awe naye.

Kwenye mahojiano na waandishi wa habari, Hamisa alikataa kuliongelea  jambo hilo na kudai ni  binafsi zaidi ila kugombana kwa binadamu ni kitu cha kawaida.

Hilo siwezi kuliongelea, yeah!. is too person, is too private, is too family. Hata vikombe kwenye kabati vinagong’ana, so sisi binadamu vinaweza kutokea”.

Lakini pia Hamisa aliulizwa nini Mahusiano Yake na Mama Diamond ambaye yeye alisema kabisa kuwa hampendi, alifunguka;

Sina kinyongo na mtu, sina bifu na mtu, mimi am just fine, may be yeye mwenyewe sio upande wangu wa kuweza kuelezea”.

Sakata hilo linasemekana kuleta sintofahamu kati ya Diamond na mama yake kwani kwa hivi sasa Diamond yupo Kwenye Mahusiano na Hamisa.

Mama Diamond Athibitisha Kumpa Kipigo Cha Mbwa Mwizi Hamisa Mobetto

Mama mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi. Sandra au maarufu kama Mara Diamond amethibitisha kumpa kipigo cha mbwa mwizi mkwe wake Hamisa Mobetto.

Mwanzoni mwa wiki hii kuna stori ilisambaa kuwa Mama Diamond kampa kipigo kizito Hamisa baada ya Kumekuwa nyumbani kwa Diamond Madale hadi kuacha wigi lake.

Mama Diamond amethibitisha habari hizo kwenye mahojiano aliyofanya na Globa Publishers ambapo ameweka wazi kuwa hampendi na hataki hata kumuona nyumbani kwake:

Ni kweli nilimpiga na wigi nikamvua na hayo  mambo ya kumfuata mzazi mwenzie ni huko, pale Madale ni kwangu na simtaki nyumbani kwangu kabisa.

Mama Diamond aliulizwa sababu gani hasa ilimfanya amchukie Mobetto na alifunguka haya:

Kitendo cha kuniitia mimi Shilawadu (kipindi cha udaku cha Televisheni ya Clouds) kilinikera sana halafu nikaanza kutukanwa kwenye mitandao ya kijamii.

Lakini pia Mama Diamond aliweka wazi kuwa baada ya kumtembezea kipigo Hamisa alimvua wigi ndipo Diamond alikuja kumuamulia:

Mama Diamond ameweka wazi hamtaki Mobetto na  kama mwanaye atakuwa na Mahusiano naye basi hawataelewana:

Kwanza tu siyo mwanamke wa kuoa (wife material) hajui kutandika hata kitanda wala kufanya tu usafi ni shida.

Yaani atajua yeye mwenyewe maana mimi ndiyo nimemzaa Diamond na siyo yeye sasa sijui nani ana nguvu hapo.

Siwezi kukanyaga kwenye  harusi yao hata siku moja watasherekea wenyewe”.

Mama Diamond ameweka wazi kuwa anataka Mwanayr amletee mwanamke mwingine anayejiheshimu na sio Mobetto.