Wasanii Wanasahau Kule Producers Tunapowatoa ;-Manecke

katika moja ya post alizowahi kuandika mtayarishaji wa muziki PANCHO LATINO  mwaka huu alisema kuwa watanzani wanasahau  thamani yako ukiwa hai mpaka pale utakapokufa, na hili limekuja kusema sana baada ya mtayarishaji huyo kupoteza maisha,

Kila mmoja ameangalia maneno hayo kwa mtazamo wake na moja ya walioongelea kwa uwazi zaidi ni huyo mtayarshaji mwenzake, maneke ambae anasema kuwa ni kweli wasanii wengi wamekuwa wakisahau  watayarishaji wanaowasaidia kipindi wanapoanza kufanya kazi mpaka wanainuka,

Maneke anasema kuwa hakuna pesa inaweza kulipa fadhila ya mtu bali ni ile heshima na kuonyesha kuwa unatambua mchango wake katika kazi zako tu ndio unaohitaji kiubinadamu,

Maneke anasema”Mpaka mtu anaona na anandika na hatushtuki, hata hawa wasanii tunaofanya nao kazi wapo wanaosahau kabisa  apreciation ya wasanii, watu wanasahau kuwa ulikesha na kuangaika kwa ajili yao.tunapokuwa hai hakuna anataka kukuzngumizia lakini inapotokea umekufa wanaanza kusema eeh maneke alifanya hivi na hivi, lakini sasa  kila mtu amekaa kimya.”