Matonya Afungukia Tetesi za Kuuza Madawa Ya Kulevya

Msanii mkongwe wa Bongo fleva Matonya amefunguka na kukataa kata kata skendo za yeye kujihusisha na kuuuza na kusambaza madawa ya kulevya huku akiziita ni fununu tu.

Kipindi cha nyuma kuna stori za Matonya kuuza madawa ya kulevya zilisambaa sana hadi kuna muda kuna taarifa zilidai kuwa aliwahi kukamatwa nchini China akiwa anasafirisha.

Sababu kubwa iliyopelekea taarifa hizo kuenea hivyo ni sababu ya maisha aliyokuwa anaishi kwani alikuwa hafanyi mziki kwani alikuwa hana nyimbo yoyote iliyokuwa inahit kwenye redio wala Tv na hata shoo alikua hafanyi lakini bado alikuwa anaishi maisha mazuri.

Alikuwa mtu wa kuishi maisha ya hali ya juu alikuwa anaendesha magari makali alikuwa ana nyumba ya kifahari lakini pia kuna taarifa zilienea kuwa alikuwa anaishi na mwanamke huko Moombasa ambaye alikuwa anamuweka mjini lakini baadae akapata bonge la skendo la kutumia madawa ya kulevya.

Matonya amefunguka taarifa hizo Kwenye mahojiano aliyofanya na Enews ya East Africa Tv na kukataa habari na kusema mambo ya madawa ya kulevya zilikuwa ni fununu tu:

Kiukweli hata mimi nasikitika kwani sio mimi tu hadi familia yangu hasa mama yangu kipindi hicho cha iyo vurugu alikuwa ana wasiwasi alikuwa ananipigia simu kila saa na haamini kama ni mimi kwani watu waliharibu kila mahali watu walizusha kuwa nimeshikwa China nataka kunyongwa lakini kikubwa ninachotaka kukisema kuwa hizo ni stori tu za mtaani ni fununu”.

Lakini pia Matonya amefunguka kuhusu taarifa za yeye kuwa na bifu na Ali Kiba ambazo amedai ni stori tu ambazo watu wamekaa wametunga kwani yeye hana bifu na mtu.

“Mimi naibiwa haki yangu vipi?” Matonya adai wimbo mpya ya Diamond umeibwa kutoka kwake

Diamond na wasanii wote wa Wasafi waliachia wimbo mpya ‘Zilipendwa’ Ijumaa Agosti 25. Wimbo huo umezua utata kwani msanii Matonya anadai kuwa wimbo huo uliibwa kutoka kwake.

Matonya alitoa malalamiko yake kwenye mtandao wa Instagram ambapo alidai kuwa ana haki zake katika jina hilo la ‘Zilipendwa’. Staa huyo aliwai toa ngoma la jina hilo hilo zamani.

“Nduguzangu wasafi / Nawapongeza sana kwa kazi mzuri mnazo zifanya / Nilifurahi Sana mlichokifanya kwa saida karoli dadaetu/ mlimuita mkamshirikisha akawapa Baraka zake/ kwangu mlishindwa nini? Sina shida Ya Pesa nina shida Ya heshima cose najua dunia ni mapito/ kama mimi naibiwa haki yangu vipi wasanii wachanga? Basata mkowapi? Wadau Wa muziki mkowapi? Usipo ziba ufa tajenga kuta!! Khaaa tena Bila woga???? lakini haki itafata mkondo wake,” Matonya aliandika.

Tazama wimbo huo hapo chini:

Matonya aeleza sababu ya kuhamia Kenya

Matonya amepinga uvumi kuwa alitoroka Tanzania kwenda Kenya kwasababu anatakikana na polisi kuhusu kesi ya utumizi wa dawa za kulevya.

Hit maker huyo ambaye anajulikana kwa nyimbo kali kama ‘Vaileti’ na ‘Anita’ alidhibitisha kuwa amehamia Kenya akizungumza na vyombo vya habari nchini humu.

Matonya alieleza kuwa yeye hajatoroka mkono mrefu wa serekali kwani yeye hatumii dawa za kulevya na wanaodai hivyo wanamchafulia jina tu.

“Sijatoroka Tanzania kwasababu hiyo, unaona hata listi ambayo imetajwa Matonya hakuwa pale. Matonya ni mtu safi na hizo ni stori zinakuwa kwa ajili ya kuniharibia jina,” Matonya alisema.

Matonya alieleza kuwa alihamia Kenya kwasababu anajihusisha na biashara kadhaa ikiwemo biashara ya kununua na kuuza gari.