Rose Anaumia kwa Sababu Alishatafunwa na Mc pilipili:- Mwijaku

Jamaa ambaye alijapatia umarufu mkubwa kupitia tamthilia ya ‘Mahusiano’ Mwijaku ametia neno kwenye ndoa ya Mc Pilipili.Kwenye moja ya mahojiano Mwijaku alipoulizwa anazungumziaje ndoa ya Mc Pilipili ambaye wakati anavisha pete mpenzi wake alilia.

Hapo awali iliripotiwa kuwa mwanadada Rose ndauka anataka kufungua kesi mahakamani kwa ajili ya Mc pilipili baada ya kutangaza kuwa aliwahi kuwa na mahusiano nae ya kimapenzi jambo ambalo sio kweli.

Bila kuficha Mwijaku alijibu “Tukubali pale hakuna ndoa ila Mc pilipili anaolewa na yule dada na natambua Rose Ndauka ameumia kwani umri wake unaenda na ajaolewa kwahiyo kuona lile tukio ameumia na ukizingatia alishatafunwa na Mc Pilipili siku za nyuma”

Rose Ndauka Amtaka Mc Pilipili Afunguke Mahusiano Yao

Mwandada Rose Ndauka amefunguka na kumtaka mc pilipili kufunguka mbele ya hadhara kuweka wazi mahusiano waliyowahi kuwa nayo na hata walionayo sasa kwa sababu kumekuwa na habari mtaani kuwa moja ya watru walioumizwa sana na kitendo alichokifanya Mc pilipili wikiend hii cha kumvisha pete mchumba wake kimemuumiza sana.

Rose anasema kuwa yeye na mc pilipili wamekuwa marafiki na wafanyakazi kwa muda mrefu sana lakini hakuna mahusiano ya mapeniz kati yao kamavile watu wanavyosema katika mitandao ya kijamii,

Akitoa salamu za pongezi, rose alisema kuwa pamoja na kwamba anatoa salamu zake za pongezi lakini ukweli inabidi ujulikane kwa watu na kwamba hakuna mahusiano ya kimapenzi baina yao.

Rose ndauka aliandika “Hongera sana mshikaji wangu kwa kupata mwenza lakini naomba kama itakuwa vizuri siku moja kuweka ukweli maana msema kweli ni mpenzi wa mungu…jamani ni hivi haijawahi kutokea mimi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mc pilipili……. ”