Kulia Sio Dhambi ,Nitalia Hata siku ya Harusi :-Mc pilipili

Mc maarufu nchini Mc pilipili amefunguka tena kwa mara nyingine huku akijitahidi kutetea sana swala lake la yeye kulia siku mbayo alikuwa akimvisha pete ya uchumba mpenzi wake.

Mc pilipili anasema kuwa kwake yeye haoni kama kulia ni kosa ila ni swala la kuwa mkweli na hisia zake hivyo haoni kama hiyo ni shida zaidi sana anaona hata siku yake ya harusi atalia tena kutokana na hisia za mapenzi alizonazo kwa mke wake huyo mtarajiwa.

Mc pilipili aanaendela kusema kuwa “mimi nikiwa nalia huweiz sema kuwa ni matumizi mabaya ya machozi kwa mtoto kama yule, siku ya ndoa ninaweza kujisikia tena kulia tu , mimi sina zile za kiume eti wewe mwanaume sijui jikaze , mi  sina. mimi niko real na hata siku ya harusi ntaangusha kilio fresh”

Ikumbukwe kuwa Mc Pilipili alilia siku ya engagement na kuzua maneno mengi katika mitandao ya kijamii kuwa sio haki kwa mwanaume kumlilia mwanamke bali mwanamke ndio ulia.

Aliyekuwa mpenzi wa Nandy afunguka kuhusu uhusiano wao wa sasa

Nandy kwa kweli ni mwanamke ambaye ameumbwa akaumbika. Kwa sababu hii ni wengi ambao wanatamani kuwa na uhusiano wa kimapenzi na yeye ila kwa hivi sasa mrembo huyo ametulia na kufocus kwenye muziki wake.

Hata hivyo aliyekuwa mpenzi wake hapo mbeleni Emmanuel Mathias ambaye anajulikana Kama MC Pilipili alifunguka kuelezea uhusiano wao wa sasa ni wa aina gani.

Akizungumza na Bongo 5 mchekeshaji huyo alidai kuwa bado anawasiliana na Nandy kuonyesha kuwa ingawa wameachana, bado wawili hao ni marafiki. Alisema,

“Mimi na Nandy bado tuna wasiliana vizuri tu, nimerudi kutoka Marekani nimemletea zawadi ya Perfume, hata hivyo yeye yupo Kenya amenicheki kunijulisha kuwa yupo huko na ninaona picha anazopost akiwa huko, unajua mimi na Nandy tumeachana sio kwa ubaya, ila tulifanya hivyo kwa sababu Nandy alikuwa anataka afanye kazi zake kwa uhuru zaidi,”

Aliongeza kuwa

” Kuachana na Nandy hapakuwa na kosa, sikutaka kumpa stress (mawazo)ni makubaliano yetu yalikuwa ni hayo, sio kwa ubaya ni kwa wema kabisa. Sikutaka kuzima ndoto zake kwani ningeshindwa kuwa mume wake ningekuwa nimezima ndoto zake za kufika hapo alipo.”