Wema Sepetu awatemea mate waliokuwa mashoga zake wa damu

Muna Alphonse ‘Muna’, Kajala Masanja na Wema Sepetu walikua marafiki wa dhati lakini warembo hawa walikosana na kila mmoja kuenda zake.

Wema amesisitiza kuwa hajawahi kuwakumbuka waliokuwa mashoga wake wa damu, hii ni baada ya madai kuwa staa huyo wa filamu za Bongo anawamiss rafiki wake.

Muna Alphonse

Akiongea na Star Mix, Wema alieleza kuwa hajawahi kuwakumbuka rafiki zake hao ambao huko nyuma walikuwa kama kumbikumbi.

“Sitaki kusema dhambi jamani sijawahi kuwamisi hawa watu (Muna na Kajala) kabisa naona kama niliwafuta kwenye kichwa changu maana najikuta kuna watu nawakumbuka lakini hao hapana,” alisema Wema.

Kajala Masanja