Nuh ataja sababu itakoyomfanya amchukue mtoto wake baada ya kuwachana na mke wake

Nuh ameweka wazi kuwa ameachana na mke wake lakini msanii huyu hakutaja sababu za kuachana.

Hata hivyo amemruhusua alikuwa mke wake kumlea mtoto wao wa kike aitwaye, Anyaghile. Lakini akizungumza na 5Selekt ya EATV hivi karibuni Nuh alisema kuwa aliyekuwa mke wake ashaolewa tena lakini ameapa kuwa hakuna kitakacho mfunga yeye kumchukua mwanawei wapo atafanyiwa vitu ambavyo si sawa.

“Mtoto still yupo na ningetamani sana kukaa naye tangu akiwa mdogo lakini nashindwa kufanya hivyo kwa sababu ya umri lakini nikiona mwanangu wanamfanyia vitu ambavyo si sawa nitaenda kumchukua na kukaa naye mimi mwenyewe,”

Aliongeza;

“Kwa hiyo nampa muda nione, nikienda nikakuta mwanangu amenenepa, ana furaha, yupo poa ataishi naye mpaka umri utakapofika lakini nikienda nikakuta mwanangu amepungua nambeba na kuondoka naye.”