Uongozi wa Ommy Dimpoz Wakanusha Taarifa Mbaya Kuhusu Msanii Wao

Uongozi wa msanii Ommy dimpozi umekanusha na kukemea vikali taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii zikidai kuwa msanii huyo alikuwa katika hali mbaya na kupatwa na umaauti kutokana na maradhi yaliyokuwa yakimsumbua.

Uongozi huo unasema kuwa taarifa hizo sio za kweli kwa sababu msanii wao mpaka sasa anaendelea  poa na kwamba hali yake inazidi kuimraika na kubadilika siku hadi siku sio kama ile aliyokuwa nayo hapo awali.

Msanii huyo ambae aliwahi kuripotiwa zaidi ya mara moja kuwa mgonjwa sana, amekuwa akirudihswa hospitali mara kwa mara kwa ajili ya kuangaliwa hali yake ingawa kuna kipindi aliwahi kuonekana kuwa imara zaidi kutokana na kuanza kuonekana katika mitandao ya kijamii.

Uongzio huo umewatoa wasiwasi mashabiki wa msanii huyo huku ukiwataka kuwa na maombi kwa ajuli ya msanii wao ili aweze kutoka katika majaribu hayo.

 

Hali ya Ommy Dimpoz Yasemwa Kuwa Mbaya, Arudishwa Hospitali Ujerumani.

Msanii Ommy Dimpoz ambae miezi kadhaa iliyopita aliwahi kuripotiwa kuwa na hali mbaya lakini baadae alikuja kuonekana yuko sawa inasemekana kuwa amerudishwa tena hopsitali hivi karibuni baada ya hali yake kubadilika na kuwa kama ilivyokuwa awali.

Msanii huyo ambae hali yake inasababishwa na hali aliyokuwa nayo mwanzoni baada ya kufanyiwa upasuaji wa koo na alitakiwa kurudi nchini  Afrika ya Kusini kwa ajili ya vipimo na kukutwa kuwa bado yuko na shida hivyo anapaswa kurusi hospitali nchini Ujerumani.

Mpaka sasa inasemekana kuwa msanii huyo yuko nchini Ujerumani kwa ajili ya kukutana na daktari wake ili kurekebisha baadhi ya sehemu ambazo zinaonekana zitaleta shida.

 

Ommy Dimpoz Awatolea Uvivu Wasanii Wanaotoa Nyimbo Mbaya

Mwanamuziki wa Bongo fleva Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz amewatolea uvivu wasanii wenzake na kusema wanatoa nyimbo mbaya na wasanii wengine wanaogopa kuwachana.

Ommy Dimpoz amefunguka hayo Kwenye mahojiano na Magic Fm ambapo amedai wasanii wengi wanatoa nyimbo mbaya na hawajui:

Kuna nyimbo za wasanii wenzangu na nyingine unaona huu wimbo gani na unaona mwana anakomaa na ma-Interview”.

Lakini Pia Ommy Dimpoz amedai saa nyingine inakuwa ni vigumu kumtobolea na kumwambia mshkaji wako kuwa nyimbo ni mbaya kwa sababu anakuwa ameshawekeza.

Na siku zote wasema ukweli wanachukiwa, kuna siku niko na washikaji jamaa anamwambia mwana lakini ule wimbo wenu mnaenda ku-shoot video?, mbona ngoma mbaya, nikasema unatoa wapi ujasiri wa kumwambia mtu hivyo”.

Hivi sasa Ommy anafanya vyema kabisa na ngoma yake ya Yanje aliyomshirikisha msanii Seyi shay kutoka Nigeria.

Nyimbo hiyo imekuwa ikishika chati za juu tangu ilipotoka wiki iliyopita Kwenye mtandao wa Youtube.

Baba Dimpozi Afananisha Malezi ya Ommy na Tatizo la Wema

Baba mzazi wa Ommy Dimpoz ambae juzi alifunguka na kusema kuwa hataki kusikia wala kumuona mwanae huyo akija katika mazishi yake siku ya kifo chake kwa sababu mtoto huyo amekuwa hamjali hata kidogo kipindi cha uhai wake ilhali mtoto huyo sasa hivi ana hali nzuri kimaisha na anashindwa kumkumbuka baba yake.

Swala la wazazi kulalamika kuhusu watoto wao hasa wasanii limekuwa sio swala geni katika tasnia kwa sababu tatizo hilo limekuwa likiibuka kila kukicha na kama utakumbuka ni hivi juzi juzi tu baba mzazi wa msanii mkubwa Dimaond Platinumz alitamka maneno ya hasira sana kwa mtoto wake huyo wa kiume.

Baba Ommy Dimpoz anasema kuwa pamoja na kwamba anahisi kosa lake ni kutokujihusisha na malezi ya Ommy Dimpozi kipindi cha ukuaji wake lakini anaamini kuwa hata swala la kumleta Duniani tu ilikuwa ni swala tosha la mtoto huyo kumjali na kuheshimu.

Hata hivyo baba Ommy Dimpoz anasema kuwa amekuwa akisikia jinsi Wema Sepetu ambavyo  anahangaika kupata mtoto lakini mwisho wa siku unaweza kukuta mtoto huyo  akashindwa kumsaidia mama yake lakini hiyo haibadilishi swala ya yeye kuwa mzazi.

mfano kama nikifa leo wala asije kunizika au kukanyaga Tabora , kwanza akija atasema nani amefariki, watampiga maana kipindi niko hai tu wala hanijali.Ni kama Wema Sepetu sasa hivi anavyohangaika kutafuta mtoto siku hakimpata hata kama hawezi kumsaidia lakini bado atamshukuru Mungu tu na mimi ni hivyohivyo, huwa namshukuru Mungu kuwa nimemleta Ommy Duniani.-Alifunguka baba huyo.