Q-Jay Akanusha Taarifa Za Yeye Kuwa Chizi na Kuokota Makopo

Msanii mkongwe wa Muziki wa Bongo fleva aliyewahi kutamba miaka ya nyuma Q-Jay ameibuka na kukana vikali taarifa zilizoenea Kwenye mitandao ya kijamii kuwa amerukwa na akili.

Taarifa Hizi zilisambazwa na msanii mwenzake anayejuliaka kama Makamua ambaye aliwaomba Watanzania wamchangie Q- Jay kwa madai ameathirika na madawa ya kulevya kiasi cha kuanza kuokota makopo.

Baada ya kusambaa kwa taarifa hizo Q Jay ameibuka na kuzikana vikali ambapo Kwenye mahojiano aliyofanya kituo kimoja cha habari amefunguka haya:

Habari hizo sio za kweli ila kitu kilichotokea ni kwamba nilipitia changamoto fulani Kwenye maisha lakini sio kwamba nilikuwa Chizi naamini hata wewe mwenyewe unaweza ukaona kuwa Chizi hawezi kuongea kama mimi”.

Lakini pia Q- Jay amelaani matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na kudai taarifa hiyo ilikuzwa kutokana na watu kutumia mitandao ya kijamii vibaya:

Kuna watu Wanatumia mitandao ya kijamii vibaya na kuna watu ambao unakuta hawakupendi ninachotaka Watanzania wajue mimi sio Chizi ninafanya kazi zangu vizuri na nimeamua kurejea kwenye muziki rasmi”.

 

Msanii Makamua Aanika Kuwa QJay Amekuwa Kichaa

Msanii mkongwe wa Bongo fleva Makamua ameweka wazi kuwa msanii mwenzake Q Jay aliyewahi kutamba na nyimbo kali kama vile ‘Sifai’ amepata kichaa.

Makamua amedai Msanii huyo ana hali mbaya na kichaa chake kiasi ya kwamba kwa hivi sasa anaokota makopo na hivyo amewaomba Watanzania wamsaidie.

Kwenye Interview aliyofanya na Bongo5 rafiki wa karibu na msanii huyo, Makamua amesema kuwa kwa sasa Q Jay yupo Bukoba na amekuwa kama chokaraa kwani amekuwa anaokota makopo na kuongea vitu visivyoeleweka.

Makamua ameweka wazi kuwa kilochosababisha mpaka Msanii huyo kupatwa na majanga ni matokeo ya kimaisha baada ya kuachana na Familia yake na ugumu wa kimaisha.

Makamua ameweka wazi kuwa wakati jitihada za kumsafirisha Bukoba kuja Dar Es salaam zinaendelea amewaomba Watanzania wamchangie pesa za matibabu kwani Madaktari wamemueleza kuwa anahitaji msaada wa ushauri na nasaha kutoka kwa watalaamu wa Saikolojia.