Ringtone Amchana Zari Baada Ya Tetesi Za Kurudiana na Diamond

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili kutoka 254 Kenya Ringtone Apoko amemjia juu Zari baada ya kuanza kusikika kwa tetesi kuwa amerudiana na Diamond.

Ringtone alishika headlines mwezi uliopita baada ya kukiri kumzimia Zari na kudai yupo tayari kumuoa na hata kumnunulia gari aina ya Range Rover mpya ambayo Zari aliikataa.

Lakini sasa Ringtone amerudi kumhoji Zari kuhusu Tetesi za yeye kurudiana man Diamond Ikiwa alishatangaza kuwa wameachana na hawezi kurudi kwake Tena.

Siku ya jana kuna Tetesi zilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa Zari na Baby dady wake staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz wamerudiana baada ya kutengana kwa takribani Miezi minne.

Ringtone amemtolea povu Zari kwa uamuzi wake wa kuamua kupasha kiporo na Diamond ambapo amempa maneno haya kupitia ukurasa wake wa Instagram:

Mpendwa Zari huwezi ukaendelea kusoma kurasa za kitabu kile kile kila siku ilihali unajua kitakavyoishia, ulioandoka Misri ukaenda Kanani itasikitisha kama utarudi tena.

Nini kitatokea kwa wasichana kibao uliowaambia sasa unamjenga Zari? Ushauri wangu ni kuwa hivi sasa mtafute Mungu kwa kufunga na maombi ili Mwenyezi Mungu akupe mwelekeo.

Lakini hivi sasa hatuna wasiwasi maana wote tunajua huwezi kurudiana na Diamond”.

 

 

 

Zari Ampa Za Uso Mwanaume Aliyetaka Kumuhonga Gari

Mwanamama mfanyabiashara maarufu na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zari The Bosslady amempa makavu ya Uso msanii wa nyimbo za Injili kutoka Kenya Ringtone Apoko.

Tangu Zari aachane na Diamond Msanii huyo amekuwa akiyuka mtandao wa kijamii kueleza kuwa anampenda sana Zari na yupo tayari kwenda kutoa mahari Uganda ili amuoe.

Lakini wikiendi iliyopita aliibuka na jipya baada ya kusikia Zari anaenda Kenya aliwatuhumu ajili ya Tamasha kwani alidai ameamua kumnunulia gari aina ya Range Rover Sport ambalo alienda nalo mpaka kituo cha redio alipokuwepo lakini alimkosa.

Baada ya kumkosa Kwenye studio hizo Ringtone aliandika Kwenye ukurasa wake wa Instagram kuwa Zari akachukue zawadi yake hiyo aliyomnunulia.

Baada ya taarifa hizo kusambaa sana Kwenye mitandao ya kijamii Zari alifunguka Kwenye mahojiano na Kiss Fm na kusema hamfahamu mtu huyo na hajawahi kuwasiliana naye hivyo hawezi kupokea kitu chochote kutoka kwake:

Simfahamu huyo Ringtone na sijawahi kukutana naye, ndio mara ya kwanza kusikia kitu kama hicho. Nina watu zaidi ya milioni 3.9 katika mtandao wa Instagram ambao wananifuatilia, siwezi kujua nani kunifuata na kwa wakati upi”.

Lakini pia Zari aliweka wazi kuwa hana shida ya Range Rover maana wiki iliyopita ametoka kujinunulia Range Rover Sport mpyaa hivyo yuko vizuri.

Msanii Ringtone Azidi Kumlilia Zari Atangaza Kumnunulia Range Rover

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili kutoka nchini Kenya Ringtone Apoko amezidi kulilia penzi la Zari The Bosslady ambapo siku ya jana ametangaza kumnunulia gari aina ya Range Rover.

Siku za nyuma Ringtone alishawahi kutangaza penzi lake kwa Zari na hata kuhahidi kumuoa huku akidai anahitaji mwanaume ambaye ni mcha Mungu na aachane na Diamond.

Siku ya jana Zari alitua nchini Kenya tayari kwa ajili ya kuhudhuria Tamasha la hisani linaloitwa Colour Purple Concert lililoandaliwa na litakalofanyika tarehe 12.

Baada ya Ringtone kupata taarifa kuwa Zari anatua nchini Kenya mara moja alimjulisha akifika atakuta gari lake Range Rover limeshanunuliwa na linamsubiri.

Siku chache zilizopita Zari alijinunulia Range Rover Sport lenye thamani ya shilingi milioni 175 lakini pia aliweka wazi kuwa kuna msururu mrefu wa wanaume wanaotaka kuwa naye.

Msanii Aliyejitolea Kumuoa Zari Ajitamba Kuwa Ana Pesa Kuliko Diamond

Msanii wa nyimbo za Injili kutoka Kenya anayejulikana kama Alex Apoko ‘Ringtone’ ameibuka tena na kudai ana pesa nyingi kuliko msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Ringtone amezidi kumtaja Zari akubali kuolewa naye kwani amemhakikishia kwa pesa nyingi alizokuwa nazo atamtunza vizuri sana kuliko hata Diamond ambavyo angeweza.

Ringtone alifunguka hivi karibuni kwenye mahojiano aliyofanya na Citizen Tv ambapo alijitapa kuwa kama mjasiriamali alitengeza milioni moja yake akiwa mwanafunzi alipoanza kuuza cd zake za muziki lakini pia amejitapa kuwa ana biashara zake kwenye sekta ya afya na nyinginezo.

Msanii huyo amejitapa ana pesa za kutosha za kuweza kumlea Zari pamoja na watoto wake wote na pia Zari ni mwanamke mzuri na wa gharama ndio maana Diamond ameshindwa kumuhudumia alijaribu kwa miaka mitatu lakini ameshindwa kuendelea lakini yeye yupo tayari.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ringtone alimuwekea Zari ujumbe huu:

Dear Zari Jesus loves you so much na amenitumia mimi leo kukwambia ana mipango poa na wewe. Mimi alinitoa from the streets mahala sikuwa na family, nyumba hata lishe buy now na magari, hela na magari ninavyo tele. Don’t waste time you never know tomorrow. I love you tha same way God loves you”.

 

Ray C hatimaye ampa jibu msanii kutoka Kenya – Ringtone aliyetaka kumoa

Mwimbaji wa nyimbo za Injili kutoka Kenya – Ringtone alitoa pendekezo akitaka Rehema Chalamila maarufu kama Ray C afunge naye ndoa.

Hii ilikua mwaka jana na Ray C hata hakumpa jibu. Ringtone ni msanii maarufu sana Kenya, amewahi fanya collabo ya nguvu na Christina Shusho. Wimbo wao ‘Tenda Mema’ bado ni hit kubwa sana.

Ringtone pia anadai kuwa msanii wa nyimbo za Injili mwenye utajiri mkubwa nchini Kenya. Ako na magari za kifahari na nyumba kubwa jijini Nairobi.

Ray C sasa amempa Ringtone jibu baada ya muda huo wote; akiongea na Mzazi Willy Tuva kenye kipindi cha Mambo Mseto ya Radio Citizen, Ray C alisema hawezi kubali Ringtone amuoe.

Ray C na Ringtone
Ray C na Ringtone

Mrembo huyo alikiri kuskia pendekezo la Ringtone kwenye mitendao lakini hakutaka kuongelea jambo hilo kwasababu hana haja nalo.

“Nilisoma hizo taarifa Kwa mitandao, namjua tu kama msanii kwanza wa Gospel, kwa hiyo nilishangaa sana ila ni mtu mzuri sana napenda anavyoshirikiana na wasanii wa Gospel wa Tanzania, ila hio haipo Kwenye ratiba yangu though,” Ray C alisema.

Ray C aliambia Mzazi Willy Tuva kuwa anampenda rais wa Kenya Uhuru Kenyatta and anaomba kukutana naye atakapoenda Kenya hivi karibuni.