Shilole apata majibu kutoka kwa Dayna

Hapo awali kabla ya kuachia wimbo wake mpya Kigori alifunguka kudai kuwa sababu yake ya kukawia kabla kuachia wimbo mpya ni kwa sababu alikuwa amewapa wasanii wa kike muda kufanyap projects ambazo ni kali kushinda zake lakini, hakuna aliyeweza kumfikia.

Hata hivyo msanii Dayna Nyange amezungumza na E-Newz ya EATV ambapo alijibu ripoti ya Shilole kwa kusema;

“Mimi nafikiri yeye ndio anaweza kuwa majibu yote kwamba kwa nini amekuja kuchukua game yake, labda alikuwa kimya kwa muda mrefu akawa anaona bado nafasi yake ipo. Unajua kila mmoja ana riziki yake kwenye hizi kazi usitengemee kwamba Dayna atakuja kufanya kitu fulani nimpoteze mtu fulani, hapana kila mta na riziki yake na kila mja na wakati wake,”

Akaongeza kwa kusema;

“I think ni wakati wake kama alifanya kitu fulani akaona mafanikio yake lakini akaona huku bado kulikuwa na mafanikio yake au anahitaji zaidi, so ana haki ya kufanya, kusema anachuku game ni misamiti tu ya lugha zetu za kisanii,”

“Naachia ngoma moto” Shilole awahaidi mashabiki

Zuwena Mohammed anayetambulika sana kama Shilole anafuraha mingi baada ya kukamilika kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Hii inamtia msanii huyu furaha kwa sababu sasa anauwezo wa kuachia kazi zake mpya, kitu ambacho hangekifanya hapo awali kwa sababu ya kuhufadhi sheria za dini yake.

Akizungumza kwenye mahojiano,Shilole alisema kuwa ilimbidi kukaa kimya lakini kwa sasa akona mipango ya kuiachia kazi kubwa kubwa hivi karibuni, hivyo akiwaonya wanamuziki wenzake kujipanga.

Shilole alisema…

“Wanamuziki wajipange maana nina ngoma kali itakayotoka hivi karibuni, ikiwa ni baada ya kukaa kimya kwa muda kutokana na mwezi mtukufu, lakini kwa sasa umeisha hivyo nakuja kwa kasi ya ajabu.”

Huu ndio muonekano mpya wa Shilole baada ya kupata mchumba?

Shilole anaejulikana kama bad girl shishi amewaekea mashabiki wake picha mpya ambayo imetuacha tukijiuliza kama huu ndio muonekane wake mpya.

Kwenye picha hiyo, Shilole anaonekana kufanana na alikuwa muigizaji wa zamani wa Amerika Marilyn Monroe. Ingawa picha hiyo ilifanyiwa ukarabati kabla ya msanii kuiweka kwenye ukurasa wake wa Instagram na mashabiki wake wametii kuwa Shilole anaonekana mrembo kwenye picha hiyo.

Baada ya kuiweka picha hiyo Shilole aliandika kusema #stargirl? kudhibitisha kuwa pia yeye alikuwa amefurahishwa na picha hiyo.

Ikiwa haujaitazama bado, basi angalia hapa chini.

Shilole
Shilole

Hatimaye Shilole apata mwanaume wa kumuoa

Kuna fununu kwamba Shilole amepata mchumba kulingana na magazeti wanavyosema mitandaoni. Mrembo huyu ambaye ameweza kuwa na wanaume kadhaa bongo hatimaye amepata mtu ambaye anamtuliza kiroho na kiakili.

Kulingana na Global Publishers Shilole amempata mwanaume mchumba ni dereva wa bodaboda Kinondoni. Waliendelea kusema kuwa chanzo cha habiri hizi kilikiri kuwa Shilole na mchumba wake wanatarajia kufunga ndoa ya siri kabla ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kuanza.

“Shilole anatarajia kufunga ndoa na dereva bodaboda hivi karibuni kabla Waislamu kuingia kwenye Mfungo wa Ramadhan na itakuwa ya siri, nyie fuatilieni mtaujua tu ukweli,” kilisema chanzo.

Hata hivyo Shilole ambaye aliweza kuongea na wanahabari alisema kuwa ni kweli kuwa amepata mchumba lakini akikataa kumuweka wazi kwa sasa. Aliendelea kwa kusema kuwa Mchumba wake siyo siyo dereva wa bodaboda kama watu wanavyosema.

“Ni kweli nina mchumba, ila siyo dereva bodaboda, ni fundi magari, tuko kwenye utaratibu wa ndoa na nitawajulisha maana ndoa yangu haitakuwa ya siri, itakuwa ya wazi na itafungwa kwenye ndege,” alisema Shilole.

Shilole adai kuwa anatamani kuolewa ila hajapata wa kumuoa

Shilole ambaye ni mmoja wa wasanii maarufu Afrika Mashariki bado hajapata mtu ambaye anaweza kufunga ndoa naye. Iwapo ameonekana na wanaume kadhaa, hakuna ambaye alifika kiwango cha kuwa mume wake.

Hata hivyo, msanii huyu anatamani sana kuoleka kitu ambacho watu wengi hawajui. Akizungumza na Showbiz Xtra hivi karibuni, Shilole alisema kuwa ni wengi ambao wanamtakia mambo mazuri ya ndoa lakini bado anamsubiri yule ambaye mwenyezi mungu atamletea.

Kwa sasa anaamini kuwa siku yake itafika na ataolewa na kuvalia shela (vazi la mwamke siku ya ndoa yake) kama bibi harusi wengine wanavyofanya.

shilole
shilole

Mrembo huyu alisema,

“Natamani sana na mimi nivae shela ila naamini wakati bado, najua nitavaa tu na watu wataongea sana maana wengine wanajua siwezi kuolewa ila Mungu atanifanyia wepesi na ndoa yangu itakuwa si ya nchi hii,”?|