Magufuli apiga marufuku Brookside Dairy – kampuni linalomilikiwa na rais wa Kenya

Brookside Dairy ni miongoni mwa kampuni 20 kutoka nchi jirani ya Kenya ambazo zimepigwa marufuku Tanzania siku mbili zilizopita.

Ubishi kati ya Kenya na Tanzania ulianza Aprili 2017 baada ya serikali ya Kenya kupiga marufuku gesi na ngano kutoka Tanzania.

Serikali ya Rais John Magufuli ililipisha kisasi kwa kuweka vikwazo kwa ununuzi wa sigara na bidhaa za maziwa kutoka Kenya.

Hatimaye Waziri wa Mambo ya Nje kutoka Kenya na Tanzania – Amina Mohamed na Augustine Mahiga walifanya mazungumzo Nairobi wiki jana na kuamua kutatua mvutano huo.

Waziri wa Mambo ya Nje kutoka Kenya na Tanzania – Amina Mohamed na Augustine Mahiga wakifanya mazungumzo Nairobi

Hata hivyo serikali ya Tanzania lilirejea hatua ya awali ya kuweka vikwazo kwa bidhaa kutoka Kenya. Kampuni 20 kutoka Kenya zimepigwa marufuku kufanya biashara Tanzania.

Brookside Dairy, kampuni inayohusishwa na familia ya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, ni miongoni mwa kampuni zilizopigwa marufuku.

Rais Uhuru Kenyatta na John Pombe Magufuli

Rais Magufuli hakupenda jinsi Brookside inaendesha shuguli zake Tanzania tangu achukue mamlaka 2015. Rais Magufuli alilaumu kampuni za Kenya zinazonunua maziwa Kaskazini mwa nchi akisema wafanyabiashara wa Tanzania wanaweza kufanya kazi hiyo. Alisema kampuni za Kenya zinawadhulumu wafugaji wa Tanzania.

Kampuni hiyo – Brookside Dairy ina matawi matatu Tanzania, moja Arusha, Mwanza na Dar es Salaam.

 

Rais wa Kenya azua utata kwa kunywa glasi moja ya bia kabla ya kuhutubia wananchi (Picha)

Rais Uhuru Kenyatta amezua utata baada ya kunywa glasi moja ya bia akiwa katika shuguli za kampeni jijini Kisumu siku ya Jumatano.

Uhuru alihudhuria ufunguzi wa kiwanda ya kutengeza pombe linalomilikiwa na kampuni ya East African Breweries Limited (EABL).

Rais huyo wa Kenya aliwekewa bia kiasi kwa glasi kuonja lakini yeye alisema ajaziwe glasi nzima ya pombe hio aina ya Senator Keg.

“Hiyo ni kidogo sana, ongeza ijae,” Uhuru aliambia mhudumu aliyekua akimwekea pombe.

Uhuru alimpea mhudumu huyo shilingi elfu mbili ya Kenya/ elfu Arobaini na tatu pesa ya Tanzania kwa kumhudumia.

Hatua ya rais Uhuru kunya pombe hadharani umezua utata kwani kuna wale wanasema rais hafai kunywa pombe hadharani.

 

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na wasanii kutoka Kenya watuma salamu za rambirambi kufuatia vifo vya wanafunzi 32 Arusha

Wakenya wametumama salamu za rambirambi kufuatia vifo vya wanafunzi 32, walimu 2 na dereva walifariki baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutumbukia korongoni kwenye eneo la Rhotia wilayani Karatu.

Wanafunzi na walimu hao walikuwa wanaenda kwenye shule iitwayo Tumaini kwa ajili ya kufanya mitihani wa ujirani mwema.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta and wasanii kadhaa wametumama salamu za rambirambi kufuatia vifo vya wanafunzi na walimu hao.

Uhuru Kenyatta – Rais wa Kenya

Rais Kenyatta alituma pole kwa Rais John Magufuli alipokuwa akifanya kampeni zake, aliomba watu wasimame kwa dakika moja kuomboleza wanafunzi walioaga.

Mzazi Willy Tuva – Radio presenter radio Citizen

Tunaungana na ndugu na dada zetu wa Tanzania kwa Msiba uliowasibu Jumamosi kwenye ajali iliyotokea Arusha na kusababisha vifo vya wanafunzi 32, walimu wawili na dereva wao .

Mola wape nguvu wazazi, ndugu, dada, jamaa, marafiki na Watanzania wote na tuwaombee waliotuacha .

Inauma sana. Inatia majonzi sana. Tanzania hamko peke yenu, tuko pamoja wakati huu mgumu .

#TanzaniaTukoPamoja

Bahati – mwimbaji wa nyimbo za Injili

REST IN PEACE ? Just to send my condolences to Our Neighbour’s Tanzania Wamewapoteza Watoto 32 Wa Primary School kwa ajali mbaya ya Gari la Shule huko ARUSHA… We pray for Strength kwa Family zote Waliowapoteza Wapendwa. Mungu awalaze Mahali Pema!

Nyota Ndogo – mwimbaji

Mimi sina raha kabisa yani hata sioni nikiposti kitu chengine MUNGU wangu waeke pema peponi.wazazi wanalia mpaka nami nalia yani mpaka uzazi unaniiuma.watanzania poleni sana

Nameless – mwimbaji

My condolences to my brothers and sisters in Tanzania for the loss. Mola na awalaze pema watoto wetu.

#TutaonanaBaadaye

Mercy Masika – mwimbaji wa nyimbo za Injili

The loss of a child can never be replaced but our hope is in the knowledge of the one who holds our lives. Poleni sana Tanzania. Mungu anayajua haya na awape amani kwa hiki kipindi kigumu kwa wazazi marafiki na nchi yote .

Pole zetu ziwafikie , Mungu ana mpango mzuri na ni salama kwetu sababu yu hai . Amani . Arusha st vincent #MunguMfarijiWetu #RIP WATOTO WA TANZANIA.