Inawezekana Ni Kweli Diamond Na Zari Mapenzi Yameisha

Tunakuwa na furaha sana katika kumbukumbu za sikukuu zetu za kuzaliwa  tena hasa tunapopata salamu za upendo kutoka kwa watu wetu wa karibu, kwa Dunia hii ya sasa ya utandawazi imekuwa ni kawaida kumtakia kheri ya sikukuu ya kuzaliwa mtu wako wa karibu kwa kuweka picha yake katika mitandao ya kijamii kama Facebook , Twitter lakini hasa hasa ni ukurasa wa Instagram ambao watu wengi kwa sasa  wanautumia.

Tarehe 2  October mwaka huu ilikuwa ni siku muhimu kwa msanii Diamond Platinumz kwa sababu alitimizia miaka kadhaa tangu kuzaliwa kwake,katika siku hiyo Diamond alifanya sherehe mfululizo siku tatu(pre-birthday party) akijumuika na baadhi ya ndugu na marafiki zake wa karibu.Lakini bado kunakuwa na utata kwa sababu tangu  kumeanza kwa shamrashamra hizo, mama mzazi wa watoto wa Diamond hajaonyesha muamko wowote wa kufanya lolote katika siku iyo ya kuzaliwa ya mpenzi wake.

Ikiwa ni kama wiki imepita tangu Zari afanye birthday party yake nchini Afrika ya Kusini , Diamond na team yake nzima ya Wasafi walisafiri na kwenda, je hii haikupaswa kutokea hata kwa Diamond ambae amefanya sherehe hii nchini Tanzania, je ni kweli Zari hakuona umuhimu wa kuudhulia sherehe hiyo , na je kama alikuwa amebanwa na kazi nyingi alishindwa kuonyesha upendo na furaha kwa mzazi mwenzie kwa kumpost katika ukurasa wake wa instagram ilhali akiendelea kupost picha zake? haya  ni baadhi ya maswali ambayo mashabiki wamekuwa wakijiuliza, au zile hasira za Diamond kuzaa na Hamisa Mobeto bado hazijaisha.

Ikumbukwe kuwa kusafiri kwa Diamond kwenda Afrika Ya Kusini ilikuwa ni moja ya vithibitisho kuwa wawili hao walishaweka mambo sawa, sasa je nini kinaendelea,hivi karibuni Zari na Diamond walikuwa katika majibizano ya mtandaoni kuhusu kosa la Diamond kuiri katika media kuhusu yeye kuzaa na video queen Hamisa Mobeto ilhali akikiri kuwa alikuwa anatoa hata matumizi kwa siri bila mzazi mwenzie huyo kujua chochote.

Hakuna aliyeamua kuweka wazi mpaka sasa kuhusu mahusiano yao, lakini kwa kuwa Diamond ni msanii na ana mashabiki pia, mashabiki wamekuwa na hamu kubwa ya kutaka kujua nini kinaendelea kati ya wazazi hao wawili ambao tayari walishaanzisha familia inayowahitaji sana.

Zari ajibu tetesi za Diamond kutoka na Dilish.

Kumezuka kwa tetesi katika mitandao ya kijamii kuhusu uhusiano mpya wa kimapenzi  kati ya msanii mkubwa kutoka Tanzania  Diamond platnumz na mrembo kutoka nchini Namibia ambae pia alishawahi kushinda shindano la Big Brother The Chase mwaka 2013 Dilish Mathew ,ambapo wawili hao walitumia mitandao yao ya snapchat kutuma baadhi ya picha na video zinazosadikika   kuwa walikuwa pamoja visiwani Zanzibar na walionekana kufikia hoteli moja na hata kupanda ndege moja wakati wa kurudi.Hata hivyo kimepita kimya kwa muda  bila hata mmoja kati ya wawili hao kuongea chochote.

Kupitia snapchat yake,Zari  aliamua kujibu tuhuma na tetesi hizo huku akionyesha kutokujali kabisa kuhusu maneno hayo na anasema yuko busy na kutafuta ela ‘Oh u dming to tell me how he cheated,…?so many just like so many on market.. like why do people think it all about fightin for..,’ ameandika Zari akimaanisha kuwa kwa upande wake hafikirii kugombania mwanaume , na watu wasikae kumsumbua kumtumia sms kuhusu mumewe anavyotemba na wanawake wengine.

Zari anasema kuwa katika vitu anavyoweweza kugombania kwa sasa ni ela na si kitu kingine,”honey i will fight for 1m not ..closed a deal worth this week “aliandika zari kwa kuongezea .

Zari amemtaja Ivan ,ambae alikuwa mumewe hapo awali , mumewe wa kwanza aliezaa nae watoto wa tatu kabla ya kukutana na diamond , Ivan ambae hivi sasa ni marehemu alifariki miezi michache , zari aliongezea kwa kusema kuwa Ivan amemuachi urithi mwingi ivyo hana haja ya kuangaika,”heading to my bed now, i dont get bedded for busness class ticket ,Ivan built a legacy for me that i can afford that any day , any time”

Zari na Diamond ni wazazi wa watoto wawili Tiffah na Prince Nillan ,wawili hao wamekuwa na skendo nyingi tangu kuanza kwa mahusiano yao, hata hivyo kumekuwa na tuhuma nyingi sana zinazosambaa zinazomtuhumu diamond kutoka na wadada tofauti na hivi juzi alikumbwa na kashfa ya kukataa mtoto wa kiume aliyezaliwa na video queen maarufu Hamisa Mobeto

Diamond na mamake walivyowasili Uganda kwasababu ya mazishi ya mamake Zari (Video)

Diamond Platnumz tayari amewasili nchini Uganda kumfariji mkewe Zari Hassan ambaye alimpoteza mamake mzazi Alhamisi asubuhi.

Mamake Zari – Halima Hassan aliaga dunia akiwa anapata matibabu katika Nakasero Hospital jijini Kampala. Mwendazake alifariki kutokana na maradhi ya moyo.

Staa huyu wa wasafi alisafiri Uganda na mamake Sanura Sandra Kassim na meneja wake Babu Tale. Tazama video hapo chini uone jinsi Diamond aliwasili Uganda.

 

Zari abadilisha jina la mtoto wake wa kike Tiffah

Kifungua mimba wa Diamond amebadilishwa jina na kupewa jina la mamake, Zari alidhibitisha haya kwenye mtandao wa Instagram.

Mtoto wa kike wa Diamond anajulikana kama Tiffah Dangote, jina hilo la pili ni ya babake ambaye alijibandika ‘Dangote’ kwasababu ya mafanikio yake kimuziki.

Hata hivyo Zari aliwajulisha watu kwa Tiffah sasa anaitwa Tiffah Hassan na sio Tiffah Dangote. Alisema hayo kwenye comment section kwa Instagram baada ya mtu kuita mtoto wake Tiffah Dangote.

Hatua ya Zari kubadilisha mwanawe jina umezua uvumi kuwa Zari amekosana na Diamond ndo sababu aliamua kutoa jina la Diamond (Dangote) na kumpa jina yake (jina Hassan).

Wambeya wanasema kuwa Diamond na Zari walikosana kwasababu Simba hajaenda kumwona mama mkwe wake ambaye alilazwa hospitalini huko Afrika Kusini. Na mbaka sasa Diamond hajamtumia mama mkwe wake salamu za heri.

 

 

Zari arudi Afrika Kusini baada ya kuruhusiwa kuishi kwa nyumba ya Ivan Ssemwanga

Kamati ya kuangalia jinsi mali aliyoacha Ivan inatumika ilibuniwa baada ya familia ya mwenda zake kugundua kuwa hakuwacha Will yoyote ambayo ingeeleza jinsi ambavyo mali yake ingegawanywa.

Wanachama wa kamati hio ni; Zari, Ritah Ssemwanga (dadake Ivan), George Ssemwanga Pinto (kakake Ivan), na Lawrence Kiyingi Muyanja maarufu kama King Lawrence (rafike yake Ivan).

Kamati hio iliamua kuwa Zari asimamie shule za Ivan huku Afrika Kusini. Katika kikao kilichoandaliwa Jumamosi, kamati hio pia iliamua kumpa Zari nyumba moja Afrika Kusini ambayo ataishi na wanawe watatu aliyowazaa na Ivan.

Zari aliondoka Uganda kuelekea Afrika Kusini baada ya kamati hio kuamua jinsi mali ya Ivan itakavyogawanywa. Kamati hio itabaki kuwa na mamlaka ya kuamua jinsi mali ya Ivan itatumika mbaka wanawe watatu watakapotimia umri ya miaka 18.

Sasa haijulikani kama Zari atabaki kuishi kwa nyumba ya Ivan Pretoria ama ataenda kuishi na wanawe watatu kwa nyumbo aliyonunua Diamond Platnumz kule Johannesburg.

“Mshipa wake wa kichwa ulipasuka” Zari aeleze kilichomuua Ivan Ssemwanga huku akipinga kuwa aliwekewa sumu

Kumekua na uvumi kuwa kifo cha aliyekuwa mume wa Zari – Ivan Ssemwanga kilisababishwa na kuwekewa sumu. Zari amepinga uvumi huu.

Akiongea na Ayo TV, Zari alisema kiharusi (stroke) aliyokua nayo Ivan kilisababisha mshipa wa kichwa chake kupasuka. Alisema kupasuka kwa mshipa huo kulisababisha damu kumwagika kwenye ubongo wa Ivan na hii ndo ilisababisha kifo chake.

“Ivan was never poison, Ivan alikua na high blood pressure na hajawai kupima na if alipima he’s never taken it serious that he needs to take his medication. So what happened alipata stroke, vile alipata stroke high blood pia ikapanda. Now during the stroke akawa paralyzed one side of the body which is the left. And during the stroke venye imempiga, imempiga vibaya akapasuka vein in his head…in his brain…mshipa right? That thing in the head ikamwaga damu in his brain so daktari wakaniambia most of the patients like him, 80% of those patients like they die immediately. Wakaniambia 20% wenye wamebaki usually they die within a month and the other 10% hao…if they come back, if they make it wanakua fully dependent yani kumvalisha pampers, kumogesha, kumkulisha and things like that. So nkamuuliza ‘doctor what’s going on with my patient I wanna know’ akaniambia ‘look we are only trying to see what we can…wakamfanya operation to reduce the pressure on the brain ya ile damu lakini the operation also wasn’t successful because during the operation pressure ilikua inapanda inashuka inapanda inashuka and then also during the same operation he over bled so they didn’t continue with the operation because he was going die immediately, wakamrudisha in the ward to try stabilize him so that they can see if they can perform a second operation. So during that time when they were supposed to go back hali yake ikawa it’s just getting down and then towards the last day wakanipigia simu ‘look it’s not good you need to come and say goodbye because tumeona blood pressure kwanza ilipanda sana 220, normal blood is about 120/125. Ivan alikua 220 ilikua so bad ikakataa, sasa vile imeshuka ikashuka to 36 which was really bad. So wakatuambia come and say goodbyes tukasema our goodbyes tukarudi nyumbani because that day imepita nothing happened. Usiku around 2 o’clock on am…was it Tuesday or Wednesday 2am wakanipigia simu your patient has passed on, lakini during the day they had already told us that he’s on the process of passing on, wakatuambia no more visitors let him pass on, let his soul go in peace. It’s not poison, amekufa kwasababu of a stroke which ruptured vein in his brain coz a lot of bleeding, it was bad.” Zari alieleza.

Tazama mahojiano aliyofanya Zari kwenye video hapo chini:

Simanzi nzito! Zari adondokwa na machozi kwa matanga ya Ivan Ssemwanga (Picha)

Aliyekuwa mume wa Zari – Ivan Ssemwanga alizikwa jana nyumbani kwao Kayunga, Uganda. Mwenda zake alisafirishwa kwao Jumatatu siku moja baada ya mwili wake kurudishwa Uganda kutoka Afrika Kusini.

Zari alihudhuria matanga hio kama mjane wa Ivan ingawa ndoa yao ilikua ishavunjika kitambo na ata Zari kuolewa na Diamond Platnumz.

Hata hivyo, Zari hakuweza kuficha uchungu aliyohisi kwa kupoteza baba wa watoto wake watatu, mrembo huyo adondokwa na machozi kwa matanga ya Ivan.

Wanawe wa kiume aliyowazaa na mwenda zake walijaribu kumtuliza lakini alishindwa kabisa kuzuia machozi kutiririka.

 

Zari awasili Uganda chini ya ulinzi mkali

Mkewe Diamond atamzika aliyekuwa mume wake Ivan Ssemwanga leo. Zari na wanawe watatu waliwasili Uganda kutoka Afrika Kusini Jumapili.

Ndege walioabiri kina Zari ndo pia ilibeba mwili wa mwenda zake. Zari alikua chini ya ulizi mkali alipowasili Uganda.

Mrembo huyo amekuwa akipigwa vita na familia ya Ivan huku wakidai kuwa anataka kupora mali ya mumewe wa kitambo.

Soma pia: Zari apigwa vita kwa maazimio yake ya kutaka kurithi mali ya aliyekua mumewe

Zaidi ya mabondia wawili walionekana wakimzingira Zari alipotua katika uwanja wa kimataifa wa Entebbe.

 

Diamond aeleza kwanini hajawai achia collabo na Zari

Je, unajua kuwa Zari Hassan alikua mwimbaji kabla ya kukutana na Diamond? Mashabiki wa Zari walitaka kujua kwanini Diamond hajamsaidia Zari kufanikiwa kimuziki kama anavyowasaidia wasanii wengine.

Akihojiwa katika kipindi cha the Trend ya NTV ya Kenya, Diamond alieleza kwanini hajampiga jeki mkewe kimuziki; swali hizo liliulizwa na mwanafunzi wa chuo kikuu cha Nairobi.

Simba alisema kuwa Zari alikuwa ashawacha kuimba walipokutana, alieleza kuwa kama Zari bado angekua mwimbaji labda hawagekuwa pamoja kwasababu ya songombingo ya muziki.

Tazama video hapo chini uone mahojiano yote:

Zari apigwa vita kwa maazimio yake ya kutaka kurithi mali ya aliyekua mumewe

Familia na marafiki wa Ivan Ssemwanga tayari wanampiga vita Zari Hassan kwa maazimio yake ya kutaka kurithi mali ya aliyekua mumewe.

Matukio haya yaliwekwa wazi na Big Eye ya Uganda ambayo ilimhoji mmoja wa marafiki wa Ivan. Chanzo cha habari hii kilisema kuwa Zari amevutana sana na Lawrence Kiyingi maarufu kama King Lawrence ambaye alitaka kupora mali ya Ivan.

King Lawrence ni mwandani wa Ivan na pia ni mwanachama wa kundi la Rich Gang ambayo ni maarufu sana nchini Uganda kwa kuhost parties za nguvu.

Rich Gang: King Lawrence (kushoto) na Ivan Ssemwanga (katikati)

Chanzo hicho kilieleza kuwa Zari and King Lawrence walitimuliwa hospitalini alipolazwa Ivan kwasababu walizua rabsha wakigombana kuhusu mali ya Ivan.

“At one point, these fights reached hospital and the two together with other family members had to be thrown out of hospital for the peace and sanity of the sick person. Ivan saw these fights, read some on Facebook but he just could not reply to anything. Someone had to hold the phone for him. And he had no reply just the hissing sounds. Deep down, he must have felt betrayed, used and abandoned by those he considered his closest,” Chanzo hicho kilisema.

Zari alionekana kwa video Instagram akigombana huku alisema kuwa mali ya mumewe wa kitambo ni ya watoto wake watatu aliyowazaa kama bado ni mke wa Ivan. Hii ilikua siku moja kabla ya Ivan kuaga dunia.

Zari na wanawe

Chanzo hicho pia kilisema kuwa Zari aliwaomba madaktari kuhairisha kutangaza kifo cha Ivan ili aweze kujipanga kable ya wanaomdulumu kuiba mali ya mume wake wa kitambo.

Mrembo huyo alitangaza mwenyewe kifo cha mumewe leo asubuhi baada ya kumaliza alichokuwa akifanya. Inasemekana Ivan aliaga dunia Jumanne asubuhi baada ya madaktari kudhibitisha kuwa viongo vyake kwa mwili vilifeli kufanya kazi.

 

 

Kwanini Diamond ameshindwa kupost chochote kumtakia hali aliyekuwa mpenzi wa zamani wa Zari

Mume wa Zari Hassan wa kitambo – Ivan Ssemwanga amelazwa hospitalini nchini Afrika Kusini. Ivan alikibizwa hospitalini baada ya kuugua ugonjwa wa Kiharusi (kwa Kiingereza stroke).

Siku chache zilizopita Zari aliwaomba mashabiki wake wamuombe mpenzi wake wa kitambo ambaye ni baba wa watoto wake watatu.

Soma pia: Zari awaomba mashabiki wake wamuombee mume wake wa kitambo – Ivan baada ya kulazwa hospitali kutokana na ugonjwa wa stroke

Zari alipoenda hospitalini kumwona Iva

Akiongea kwenye kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM, Diamond alieleza sababu zake za kukosa kupost chochote kumtakia hali Ivan Ssemwanga.

“Ni kweli mzazi wake Zari anaumwa, na yuko serious. Na kila siku huwa namuhimiza Zari akamuone mzazi mwenzie kwasababu najiuliza asingekuwa anaenda familia yangu ingemuonaje, kwa hiyo maskini dada wa watu kila siku huwa anaenda. Sijawahi mpigia simu kwasababu yuko serious sana na pia sikuweza kumpost kwasababu watu waneanza kusema labda natafuta kiki maskini ya Mungu kumbe wala,” Diamond alisema.

Diamond akiwa Clouds FM

 

Zari awaomba mashabiki wake wamuombee mume wake wa kitambo – Ivan baada ya kulazwa hospitali kutokana na ugonjwa wa stroke

Mume wa Zari Hassan wa kitambo – Ivan Ssemwanga amelazwa hospitalini nchini Afrika Kusini baada ya kuugua ugonjwa wa Kiharusi (kwa Kiingereza stroke).

Ugonjwa huwo hatari husababisha mwili kupooza kutokana na matatizo kwenye mishipa ya damu inayolisha ubongo.

Zari na Ivan walijaliwa kupata watoto watatu wa kiume kabla ndoa yao kusambaratika. Zari alidai kuwa Ivan alikua anamchapa na kumtesa akiwa mke wake – sababu ya yeye kumwacha.

Zari na wanawe

Ata hivyo Zari bado huzungumza na Ivan kwasababu ya watoto wao. Picha inayosambaa mitendaoni inaonyesha Zari akisimama kando ya Ivan ambaye amelazwa hospitalini.

Ivan akiwa hospitalini

Zari pia aliwaomba mashabiki wake kwenye Instagram wamuombee mume wake wa kitambo. Hakueleze zaidi kuhusu hasi ya Ivan.

Hii ndio picha ya Zari akiwa bado fukara ambayo imezubaisha wengi…hata Diamond Mwenyewe

Saa hii Zari ako kwenye mitandaoni akionnyesha manguo, magari na maisha kiistaarabu lakini hakuanzia hapo.

Kuna wakati alikuwa msichana wa kawaida tu..mweusi na mwenye mavazi na nywele za kawaida tu and watu wachache sana wangetmani wakati huo.

Also read: Zari aringia umbo lake miezi tatu baada ya kuzaa mtoto wake wa tano

Ameabadilika sana na kwa kweli alibleach uso wake ili kufanana na ma star wengine mpaka na wale wa marekani.

Ebu tazama hii picha:

Zari

Tazama jinsi Diamond alivyobaki akiduwaa baadaya ya Zari kupata vipuli visivyo vyake chumbani mwao

Diamond alinaswa na mke wake Zari Hassan walipokuwa wakionyesha bidhaa za Danube kwenye tangazo.

Tangazo hilo lilikua linaonyesha bidhaa za Danube zinazouzwa GSM Mall jijini Dar es Salaam. Diamond na Zari walitumiwa kuonyesha bidhaa hizo.

Hit maker huyo wa Marry Me alibaki akiduwaa baadaya ya Zari kupata vipuli visivyo vake chumbani mwao katika tangazo hilo.

Kiswahili cha Zari kimeimarika sana; Zari, mzaliwa wa Uganda, alizungumza Kiswahili mufti alipotokea kwenye tangazo hilo.

Diamond atapigwa na butwaa! Zari Hassan ajiandikisha kufanya mazoezi na bondia huyu

Mkewe Diamond Platnumz, Zari Hassan, amejiandikisha kufanya mazoezi na bondia fulani anayejulikana kama Tumiseeco.

Zari, ambaye ni mama ya watoto watano, ameweza kusitiri uzee kwa kufanya mazoezi ya kimwili na kula vyakula ambavyo hayaongezi mafuta mwilini.

Zari alitangaza kwamba amejisajili kufanya mazoezi ya kimwili na Tumiseeco wiki moja iliyopita. Bondia huyo ako na misuli kila sehemu ya mwili yake.

Zari na Tumiseeco

“Meet Tumiseeco a lifestyle coach, fitness trainer…. earlier this week I signed up with him. Can’t wait to see what he will do with this body of mine… DM him for your fitness routines and eating plan program…” Zari aliandika.

Tazama picha zake Tumiseeco hapo chini: