Tanasha Azidi Kujiamini na Penzi la Diamond

Mpenzi wa staa wa Bongo fleva na Mkurugenzi wa WCB Diamond Platnumz, Tanasha Donna Oketh ameonekana kuweka maneno ya watu pembeni za kuzidi kukolea Kwenye Penzi na Diamond.

Tangu Diamond aweke hadharani kuwa yupo kwenye mahusiano na Tanasha mwaka jana mwishoni ni wazi kuwa hawajapita njia nyepesi kwani Penzi Lao linapingwa sana hasa kwenye Mitandao ya kijamii.

download latest music    

Lakini Diamond na Tanasha wameonekana kupuuzia maneno ya watu na kufanya mambo yao na inaonekana wazi kuwa Tanasha amekolea kwenye Penzi na Mbongo fleva huyo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Tanasha ujumbe ambao ni mfupi Lakini unabeba maneno mazito kuhusiana Penzi lake na Diamond:

Kujiamini ya kweli huwa haina chumba cha chuki, ni pindi unapofahamu kitu kizuri hauna sababu ya kuchukia”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.