Tanzia: Producer Pancho Latino Afariki Dunia
Mtayarushaji wa muziki wa Bongo fleva kuyoka B Hits maarufu kama Pancho Latino Amefariki dunia kwa ajali ya kuzama majibu wakati anaogelea katika visiwa vya Mbudya.
Taarifa za awali zimedai Pancho alikuwa anaogelea katika fukwe za visiwa vya Mbudya aliingia Kwenye maji kwa nia ya kuogelea lakini kwa Bahati mbaya alizama na mpaka kuja kiokolewa hali yake ilikuwa tayari mbaya na kuwahishwa hospitali ambapo aliaga dunia.
Wadau mbalimbali wa sanaa na burudani wameanza kutoa pole kwa ndugu jamaa na marafiki kufuatia msiba huu mzito.
Bwana ametoa Bwana Ametwaa Jina la Bwana lihimidiwe, Amina.