Tanzia: Muigizaji Mkongwe, Mashaka Afariki Dunia

Ramadhani Mrisho Ditopile maarufu kama ‘Mashaka’ aliyewahi kuigiza katika kundi la Kaole Sanaa group miaka ya nyuma amefariki dunia katika Hospitali ya Amana iliyopo Ilala jijini Dar es Salaam leo asubuhi Jumamosi, Oktoba 20, 2018.

Abdallah Ditopile ambaye ni mtoto wa marehemu amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kusema baba yake aliugua ghafla usiku ndipo wakamkimbiza hospitali kwa ajili ya matibabu na Ilipofika asubuhi hali yake ikabadilika, madaktari walitupatia rufaa ya kumpelekea katika Hospitali ya Muhimbili Tawi la Mloganzila, wakati tukijiandaa kuita ambulance, akakata roho, baba ametutoka katika hospitali ya Amana jijini Dar es salaam.

download latest music    

Mashaka alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Presha pamoja na kisukari ambapo jana alizidiwa gafla na kukimbizwa hospitali ya Amana, madaktari walifanikiwa kumpa huduma ya kwanza na matibabu ikiwa pamoja na kumuwekea mashine ya kupumulia ya oksijeni.

Mashaka amezikwa siku ya Jumapili oktoba 21 Katika makaburi ya Kinyerezi jijini Dar Es Salaam.

Mwenyezi Mungu Ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi Amina.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.