TID Atangaza Kulikacha Jina La ‘Mnyama’

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Khaleed Mohamed maarufu kama Top in Dar ‘TID’ ameibuka na kuweka wazi kuwa kuanzia Hivi sasa hataki kutumia jina la ‘Mnyama’.

Kama utakumbuka siku za nyuma moja ya majina ya TID (a.k.a’s) ilikuwa ni jina la Mnyama Lakini TID aliingia kwenye mgogoro na baadhi ya wasanii huku kisa kikiwa ni jina hilo.

download latest music    

TID amewahi kugombania jina na Diamond Platnumz ambaye alikuwa anajiita simba Lakini pia aligombania jina na Dudubaya ambaye anajiita Mamba Lakini pia aligombania jina Mr. Blue.

Lakini hatimaye TID kaweka siku zake za kugombania jina nyuma yake kwani ametangaza Kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa kuanzia Hivi sasa hataki hata kulisikia jina hilo:

Proudly Tanzanian music straight from the roots of Bongo fleva…..Naitwa TID kuanzia leo sitaki kuitwa mnyama kila mtu kawa mnyama sasa hivi sina unyama wowote I am a changed person…Niiteni Top tu kama zamani please tusije gombana mimi sio mnyama wowote ni binadamu wa kawaida tu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.