Timbulo Aamia Kwa diamond, Mashabiki Wamshangaa

Msanii ambae kwa sasa amekuja na kibao chake kipya kinachojulikana kama vibaya , timbulo ameamua kufunguka yale anayo-feel kwa msanii mwenzie mkubwa duniani Diamond Platinumz huku akisema kuwa moja ya nyimbo za Diamond ulikuwa umefanana sana na wimbo wake ambao aliacha kuutoa baada ya kuona msanii huyo ameutoa.

Timbulo anasema kuwa alikuwa akiupenda sana wimbo wa Utanipenda ambao na yeye pia alitaka kuutoa lakini aliumi sana alipoona wimbo hio Diamond ameutoa, lakini ilikuwa ni copy yake.

download latest music    

Mimi niliwahi kumtamani Mond katika wimbo wa Utanipenda ,nilikuwa nimepotea kwenye game sijatoa ngoma muda mrefu sana , nilivyomsika jamaa kitu amekifanya kwenye ule wimbo ni copy ya  kile kitu na mimi pia nilikuwa nimeimba na kutamani kukifanya , kwanza nilipenda sana lakini baadae niliumia kwa sababu it was my sort.

Kwanza kwa namna kubwa sana  kuanza story sasa nikaanza kupita na meleody zangu  lakini ile story yenyewe aliyoimba yeye  alafu ukija kitu alichokuja  kukifanya kwenye  video, melody, maandiko kila kitu cha kwenye ule wimbo  it was perfect kwa upande wangu

Hata hivyo baada ya msanii huyo kuyaongea hayo mashabiki wake na mashabiki wa Diamond ambao wanajua muziki wa wasanii wote wawili wamemjia juu Timbulo na kuwambia kuwa aache kutafuta kiki kupitia mgongo wa Diamond kwa sababu hawezi kujifananisha na Diamond hata kidogo na hizo habari za wimbo wa Utanipenda sio kweli kuwa Diamond anaweza kufanya copy yake hata mara moja.

Mashbaiki hao waliendelea kusema kuwa wamekuwa wakimshangaa msanii huyo kwa sababu hivi karibuni alikuwa akisema kuwa Diamond kufanya kolabo na wasanii wa nje  sio kitu kizuri na kinaua muziki wa bongo , iweje leo aseme kuwa alikuwa anaupenda sana wimbo  Utanipenda wa msanii huyo huyo tena.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.