Tumekoma Hatuwezi Kurudia Tena Makosa-Babu Tale

Meneja wa Kampuni ya Wasafi (WCB) Babu Tale amekiri kuwa adhabu waliyopewa wasanii wake Diamond na Raymond Mwakyusa’ Rayvanny kufungiwa miezi miwili, imewafundisha na hawatarudia tena.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la mwananchi, Babu Tale ameweka wazi kuwa adhabu waliyopata Diamond na Rayvanny imekuwa somo kwao wote na hawatorudia tena makosa.

download latest music    

Kwa kweli kwa muda wote ambao wasanii wetu walikuwa wamefungiwa pamoja na kusitishwa kwa tamasha letu la Wasafi, tumejifunza mengi, hatuna budi kuishukuru BASATA na serikali kwa ujumla tunachowahaidi ni kwamba tumrjifunza mengi na hatutarudia tena”.

Diamond na Rayvanny walifungiwa mwaka jana Desemba 15 na kuzuiwa kufanya maonyesho ya nje na ya ndani hata hivyo Wiki chache zilizopita BASATA Ilitangaza kuwafungulia rasmi.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.