Tunda akanusha tetesi za kutoa ujauzito

Yule mwanadada anaetikisa jijini Dar Es Salaam  hasa katika upande yeye  wa kuwa moja kati ya  video vixen bora na amekuwa  akionekana katika video nyingi za mastaa wakubwa nchi , Tunda Sebasita anafahamika kwa jina la umaarufu kama Tunda  leo amefunguka na kukanusha stori zilikuwa zikisambaa katika mitandao kuwa alikuwa mjamzito kipindi cha nyuma  na sasa ameitoa mimba iyo, hata hivyo kuenea kwa tetesi izo kunasababishwa na mrembo huyo  (Tunda) ambae amekuwa akipost picha huku akionyesha sehemu za  tumbo lake ambapo watu walianza kujudge na kusema  kubwa  mrembo huyo atakuwa ni mjamzito, lakini bado hata muda ulipopita bila kuona maendeleo yoyote  basi tetesi zilibadilika na kusemekana kuwa  ametoa mimba iyo.

Hata hivyo Tunda amekanusha tuhuma hizo zinazoendelea katika mitandao ya kijamii na kusema kuwa kwa upande wake taarifa hizo ni ngeni, na wala hakuwa na mimba na katika maisha yake hajawahi kupata mimba kabisa.

download latest music    

Akizungumza na waandishi wa habari wa kituo cha EATV, Tunda anasema kuwa sababu za yeye kuwa na  tumbo ni kitambi tu kilichokuwa kinakuwa sababu ya yeye kunenenpa maana yaye ana asili ya tumbo ila kwa sasa anafanya diet na ndio maana watu wanaona tumbo linaisha.

“Sina mimba na sijawahi kupata ujauzito hilo tumbo limeongezeka tu nina asili ya tumbo nikinenepa na tumbo linaongezela hizo tetesi za kutoa mimba ndo nazisikia kwako sijawahi kupata wala kutoa mimba kabisa.”

Tunda ni moja ya video vixen maarufu hapa nchi na amekuwa akitokea katika video za wasanii wakubwa maarufu nchi.baaadhi  ya video zake ambazo ameshawahi kutokea ni pamoja na “Salome”  ya Diamond Platinumz, pamoja  na “Furaha” wa Young Dee

Tunda ni mmoja kati ya video queen mwenye drama nyingi sana za kwenye mitandao kutokana na picha anazoposti katika ukurasa wake wa instagram, na katika historia yake mrembo huyo alishawahi kutoka kimapenzi na msanii wa Bongo Fleva Young Dee  mwenye kibao kipya cha “Utani utani”

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.