Tunda Amefunguka Kuhusu Skendo Ya Kutoa Mimba na Uhusiano Wake na Diamond

Video queen maarufu Bongo, Tunda a.k.a the Bossbabe amefunguka kuhusu skendo inayomuandama kwa muda mrefu ya kutoa mimba mara kwa mara na hata kubeba ujauzito wa mwanamuziki Diamond Platnumz.

Tunda amezungumza kuhusu yale maneno yaliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii kwa wiki kadhaa sasa ambapo amedaiwa pia kutoka kimapenzi na mwanamuziki Diamond baada ya kuposti picha zake mara kwa mara na kuweka picha yake kama profile picha.

download latest music    

Tunda amefunguka kuhusiana na skendo hizo zinazomkabili kwa sasa kwenye mahojiano aliyoyafanya na Millard Ayo Tv ambapo amesisitiza kuwa hana uhusiano wa kimapenzi na Diamond kama watu wengi wanwvyozusha bali ni rafiki wa karibu na kaka yake;

Hizi stori za mimi kuwa mjamzito siyo za kweli kabisa sijawahi kubeba maishani mwangu bali nimeongeza tu nikawa tofauti, na kwa maana hivyo sijatoa mimba wala sijawahi kutoa mimba maishani mwangu mwote. Kuhusu kuweka picha za Diamond mtandaoni ni kuwa mimi namkubali sana Diamond ni kama kaka yangu nampenda. Nakubali kazi zake ni mtu wangu wa karibu kwa kweli sisi ni marafiki”.

Lakini pia Tunda amesisitiza kuwa ana mpenzi wake tayari ambaye sio staa wala msanii kwaiyo watu wengi hawamfahamu  lakini amesema siku akiwa tayari kumuweka wazi basi watu watamuona, pia Tunda amewaomba watu wasim-judge kwa kumuangalia kwenye mitandao ya kijamii kwani kila kitu sio serious kiasi hicho.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.