“Tusiishi Kwa Chuki na Uadui Maana Hatujui Kesho Yetu Itakuwaje”- Ommy Dimpoz

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Omary Nyembo Maarufu kama Ommy Dimpoz amefunguka na kuongelea hali yake ya kiafya baada ya kuumwa kwa zaidi ya Miezi mitano.

Jana ilikuwa ni siku ya kuzaliwa ya Ommy Dimpoz ambaye alikuwa hoi mahututi kwa Miezi michache iliyopita baada ya kufanyiwa upasuaji wa koo nchini South Africa.

download latest music    

Akiwa anasheherekea siku yake ya kuzaliwa Ommy Dimpoz ameweka ujumbe mzito ambapo pia ameweka picha yake alipokuwa hoi taabani ICU.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ommy Dimpoz ameandika umuhimu wa kutokuwa na vinyongo wala chuki na watu maana hakuna anayejua sana wala siku ya kufa.

https://www.instagram.com/p/Bno_S2-gBcU/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=8ubavf33rhok

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.