Uchebe Apongezwa Kwa Kumuachisha Pombe Shilole

Mume wa Msanii wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole, Ashraf Uchebe amepewa pongezi nyingi na wasanii mbali mbai Baada ya kuweza kumbadilisha mke wake.

Wasanii wa Bongo movie kama vile Jacob Steven ‘JB’, Steven Mengele ‘Nyerere’ na Single Mtambalike ‘Richie’ wamejikuta wakimpa ­pongeza shemeji yao, Uchebe kwa kumbadili na kumuweka kwenye maadili ya kidini tofauti na alivy­okuwa zamani.

download latest music    

Global Publishers wanaripoti kuwa tukio hilo la kumpongeza Uchebe lilichukua nafasi kwenye msiba wa msanii mwenzao Salome Nonge ‘Mama Abdul’ baada ya Shilole kuonekana kubadilika sana kwani hata mmoja wa wasanii alipommwagia pombe kwa bahati mbaya, alionesha kumaindi kuliko maelezo.

Jamani Uchebe hongera sana maana kazi uliyofanya sio ndogo, nakuambia ni kazi kubwa. Yaani dada yetu Shilole leo hii anaona pombe anaruka hivi? Shemeji yetu hongera, umetukosha“.

Shilole alifunga ndoa na Uchebe mwaka juzi na tangu afunge ndoa ameonekana akiwa kama mwanamke tofauti kama alivyokuwa awali na hata kuonekana akiwa ameanika dini zaidi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.