Ujumbe Wa Diamond Kwa Ali Kiba Baada Ya Kuoa

Msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz ameweka bifu pembeni na kumpongeza msanii mwenzake Ali Kiba baada ya kufunga ndoa siku ya jana.

Diamond na Alikiba wamekuwa kwenye bifu la muda mrefu ambapo lilisababisha kugawa mashabiki zao lakini hivi katibuni Diamond aliweka wazi kuwa hana bifu na Ali Kiba.

download latest music    

Jana ilikuwa siku ya shamra shamra kwa Alikiba kwani alifunga ndoa mjini Mombasa Kenya na mkewe Bi. Amina na ilikuwa ni harusi iliyozua gumzo sana Kwenye mitandao ya kijamii.

Diamond hakuona hiyana kumpongeza Ali Kiba na alimtumia ujumbe wa pongezi Kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo aliandika:

Wadau nimeambiwa King Kiba kaoa leo mumfikishie salamu zangu za ndoa njema na maisha yenye furaha Amani na baraka tele”.

Baada ya kumtumia ujumbe huo pia Mama mzazi wa Diamond na familia yake wote walimposti Ali Kiba na kumpongeza.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.