Ujumbe wa Gabo kwa Diamond na Wasanii Kuelekea Wasafi Festival

Msanii wa bongo movies, gabo zigamba amefunguka na kuandika ujumbe kwa wasanii wanaoenda kufanya show katika tamasha la Wasafi festival kuwa tamasha hilo linaonekana kuwa la kisasa sana hivyo na wao pia inawabidi kufanya mazoezi kwa muda mrefu na umakini ili kuweza kuwahudumia vizuri mashabiki wao.

Gabo pia anasema kuwa Diamond ni mkombozi wa wasanii na muda wa kufanikisha hayo ndio sasa ingawa wapo watu watakaofanya figisu ili kuweza kudidimiza jitihada zake lakini hapaswi kujali hayo zaidi ya kuangalia kile anachotaka kukifanikisha.

download latest music    

binafsi ninajua kuwa wazo lako ni zuri kulio wazo lenyewe, lakini pia ninaamini kuwa upande wa bongo fleva’ Freedom is coming tommorrow‘, ila wapo watwana watakaovijika uungwana  ili wanyanganye kidogo chetu twana na kusema kuwa lengo halisafishi njia…hao ni wapuuzi tena wakupuuzwa na kushindwa zao dhamiri,  wasiweze kusimama.pasi na shaka stage ni ya kisasa  basi pls wasanii mfanye mazoezi ya kukonga nyogo za mashabiki  zenu maana kuimba ni swala jingine na show ni swala jingine.

Tamsha hilo linatarajiwa kuanza november 24 mwaka huu na kuanzia mkoa wa mtwara ambapo wasanii wa WCB pamoaja na wasanii wengine watapata nafasi ya kukutana na kufurahia pamoja na mashabiki wao.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.