Ukizaa na Mwanamke Sio Lazima Umuoe- Yusuph Mlela

Msanii wa Bongo movie Yusuph Mlela amefunguka na kusema kuwa kama mwanaume akizaa na mwanamke haina maana ya kwamba lazima amioe mwanamke yule.

Siku za nyuma Yusuph Mlela alitengeneza headlines Baada ya kusema kuwa hawezi kumuoa mwanamke aliyezaa naye kwa sababu haendani naye na ilikuwa bahati mbaya tu wakapata mtoto.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Mlela amesema kuwa hakusema kuwa hawaendani au alimponda mama Watoto Wake bali alisema kuwa sio lazima kumuo mwanamke huyo.

Hapana, sikusema kwamba hatuendani, lakini siyo lazima mkizaa muoane, mnaweza tu mkazaa na mwisho wa siku kila mtu akaendelea na mambo yake na hiyo desturi siyo ya kwangu peke yangu ipo dunia nzima”.

Lakini pia Mlela alikataa kama alizaa na mwanamke huyo kwa makibaliano:

Haikuwa kwa makubaliano, lakini naweza kusema kwamba, ilitokea tu tukawa tumepata mtoto, lakini tabia zikawa tofauti kizuri tulikuwa hatujafunga ndoa wala kujitambulisha popote hivyo ilikuwa ni ruksa kuachana.

Atabaki kuwa mzazi mwenzangu ni mtu ambaye namheshimu kwa sababu amenizalia mtoto”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.