Vanessa ana thamani kubwa kwangu- Jux

Msanii wa RnB nchini Juma Jux anayetamba na wimbo wake mpya wa “Utaniua” amefunguka juu ya uhusiano wake na mwanamuziki wa hapa nchini Vanessa Mdee, Kuwa kwake kwanza ni familia yake kisha Vanessa.

Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake na Vanessa alisema, “Nampenda Vanessa kuliko msichana yoyote niliyewahi kuwa naye kwenye mahusiano na sitegemei kumuachia aende hivi hivi hata familia yangu inajua mapenzi yangu kwa Vanessa.

download latest music    

“Nikiwaga mbali na Vanessa kitu cha kwanza nikiamka asubuhi naingia Instagram namuangalia halafu nampigia simu, Siwezi kumpigia Simu bila kuangalia picha zake kiufupi ninampenda sana Vanessa”.

Kuhusu kuwa na Mtoto Jux alifunguka kuwa ” Sasa hivi natamani kupata mtoto na nina mpango huo, kwa sasa najipanga vizuri Mungu akinijalia basi hivi karibuni ntapata mtoto na nitapenda kumuita Karim na si jina jingine zaidi ya hilo.

Jux na mpenzi wake huyo Vanessa waliachana miezi michache iliyopita lakini Jux ameweka wazi kuwa bado a na mp end a.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.