Vannesa Kwenda Kutumbuiza Mbele ya Rais Wa Gabon
Mwanadada mashughuli katika muziki ana anaefanya vizuri sana katika tasnia hii Vannesa Mdee amepata dili tena lingine la kutumbuiza mbele ya raisi wa Gabon kwa heshima ya muziki alionao nchini humu.
Akizungumza na bongo 5 Vannesa anasema kuwa , kutakuwa na tamasha kubwa litakalohudhuriwa na wasanii wakubwa ndani na nje ya nchi akiwemo msanii Federic Gaccita na Harberto Gaccita ambao ni wasanii mashuhuli nchini humo.
Hata hivyo Vannesa Mdee anahistoria nzuri na nchini hiyo kwa sababu aliwahi kufanya kazi na Ali Bongo kutokana na kukutana kwao mwaka jana alipokuwa akifanya muziki wake na project yake ya African Queens aliyoifanya mwaka uliopita.
Katika Project hiyo, Vanessa aliwahi kufanya wimbo mmoja ambao haukutokana lakini kutokana na uwepo wake June 9 , inawezekana wimbo huo ukafanikiwa kutoka kwa mashabiki na kutumbuizwa jukwaani.