Vj Penny Aanika Siri Ya Urembo Wake

Mtangazaji wa kipindi cha Harusi zetu Penniel Mungilwa maarufu kama Vj Penny amefunguka na kuweka wazi Siri ya urembo wake.

Vj Penny ambaye alijizolea umaarufu kutokana na mahusiano yake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, ameweka wazi kuwa anajipodoa sana ili kuficha matatizo.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Penny alisema mtu anaweza kukuona umependeza njiani na unanukia vizuri, akajua una mamilioni ya fedha kwenye pochi kumbe ni kujiweka vizuri tu ili kuficha shida zako.

Mimi naweza kupita njiani mtu akadhani nina fedha nyingi maana napenda kujiweka nadhifu kila wakati ili tu heshima yangu ibaki palepale. Siyo hata mtu ukifulia kila mtu ajue, hapana haipendezi. Unaficha matatizo yako kwa kutokelezea chicha”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.