Vj Penny Afunguka Jinsi Alivyokwepa Matusi Kwenye Mitandao Ya Kijamii

Mtangazaji wa Magic Swahili, Penniel Mungilwa maarufu kama VJ Penny amefunguka na kueleza jinsi alivyoweza kuukimbia kabisa umaarufu kwenye mitandao ya kijamii na kuwa kimya.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Penny alifunguka kuwa kuna kipindi alikuwa gumzo sana midomoni mwa watu kila kukicha ambapo aliamua kujificha ili wamsahau na kweli alifanikiwa na hiyo ilimsaidia kufanya mambo yake mengine ya maendeleo zaidi.

download latest music    

Unajua kuna wakati watu wanaweza kukuzungumzia mpaka ukaogopa kabisa kukatiza mitaani na ndiyo iliyonitokea nikaamua kujificha na kuachana na maisha ya kujiachia klabu au sehemu za starehe, hii imenisaidia kwani wamenisahau na siku hizi wanajadili mambo mengine”.

Miaka minne iliyopita Penny alikuwa maarufu sana kwenye mitandao ya kijamii ambapo hiyo ilikuwa Baada ya kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na Diamond Platnumz.

Lakini Penny alitoka kabisa midomoni kwa watu Mara Baada ya kuachana na Diamond na kuamua kukaa mbali na mitandao ya kijamii na hivyo kutoongelewa sana na mashabiki.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.