“Wanawake Wenye Mapenzi Ya Dhati Tunaonewa Sana”-Shamsa Ford

Muigizaji wa Bongo movie staa Shamsa Ford Ameibuka na kutoa ujumbe wenye utata na kusababisha minong’ono juu ya ndoa yake na mfanyabiashara Chiddi Mapenzi Kuzidi.

Kama utakumbuka siku za nyuma kidogo Chiddi Mapenzi alikamatwa hadharani na mke we Shamsa Baada ya kuchepuka na mrembo wa Instagram na kusababisha mtikisiko katika ndoa yao.

download latest music    

Lakini baadae kidogo Shamsa aliweka wazi kuwa ameamua kumsamehe mume Wake na hata kusema hadharani kuwa hawezi kumuacha mume Wake Kisa ana wanawake wa kando.

Na kwa muda mrefu kumekuwa na tetesi za kutokuwa na maelewano kati ya Shamsa na mumewe kutokana na maneno ya utata anayoweka kwenye Mitandao ya kijamii yenye mafumbo.

Siku ya jana Shamsa ameibua tena gumzo na kusababisha watu kuhoji labda huenda mume Wake Chiddi amechepuka tena ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram, Shamsa aliandika maneno haya:

Wanawake ambao tuna mapenzi ya dhati huwa tunaonewa sana, Wanawake ambao tunaishi maisha ya Uhalisia huwa tunaonekana washamba, Lakini wale Wanawake wachunaji ndio huwa wanapewa kipaumbele na kuthaminiwa”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.