Wanja Umenipa Heshima na Kazi-Ebitoke
Mwanadada mchekeshaji kutoka timamu Ebitoke ameweka siri ya mafanikio yake katika kazi na kusema kuwa tabia yake ya kipekee na ubunifu wa kupaka wanja wa kuukoleza ndio uliompa kazi, jina na ajira katika tasnia ya maigizo.
Ebitoke anasea kuwa yeye hawezi kufanya make up kama watu wengine wanapokuwa katika lication kwa sababu wanja ndio kitambulisho chake kikubwa katika kazi yake, na kusem akuwa endapo atabadilisha aina ya kujiremba na kuanza kupaka tofauti basi atasahaulika kabisa.
Ninauheshimu sana wanja kwa sababu ndio ulionipa maisha ,hata akaunti yangu ya benki inafanya vizuri sana na nimetimiza ndoto zangu nyingi tu kwasababu ya huu wanja ingawa watu watakuwa hawauelewi.