Wasafi Festival Kuwashusha Wizkid na Mr. Eazi

Mkurugenzi wa WCB Diamond Platnumz amethibitisha ujio wa staa wa muziki kutoka Nigeria  Wizkid kwa ajili ya kuperfom katika tamasha la Wasafi Festival.

Diamond Platnumz  amethibitisha hilo kupitia ukurasa wa Instagram baada ya ku-comment kwenye post ya Rayvanny ambayo alipost video fupi ikiwaoyesha Diamond na Wizkid muda mfupi baada ya kumalizika kwa tamasha kubwa la muziki la One African Music Festival lililofanyika Dubai wikiendi iliyopita.

download latest music    

Kwenye video hiyo Diamond alithibitisha kuwa atamshusha msanii huyo mkubwa Afrika kwenye tamasha hilo litakalofanyika Dar Es Salaam baada ya kuzunguka mikoa mingine.

Lakini pia na msanii Harmonize ameamua kuweka wazi meseji zake alizokuwa anawasiliana na msanii kutoka Nigeria akiomba kuja kushiriki angalau katika moja ya tamasha la Wasafi Festival Tanzania.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.